Rev. Mtikila Confirms Hosting FDLR Commanders in Dar es Salaam

Rev. Mtikila Confirms Hosting FDLR Commanders in Dar es Salaam

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,356
Nilikuwa nasoma ripoti ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusiana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) iliyowakilishwa kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa January 2014. Ripoti inaongelea masuala mengi, lakini nimeona siyo vibaya ku-share nanyi sehemu inayohusiana na Mchungaji Mtikila kukubali kuwa-host rebels wa FDLR nyumbani kwake Dar Es Salaam na masuala mengine kuhusiana na Tanzania.

Pia ripoti inadai kuwa vyombo vya usalama vya Tanzania vilimweka under house arrest Dar Es salaam mmoja ya viongozi wakuu wa FDLR anayejulikama kama Stanislas Nzeyimana (Bigaruka). Kwa wale wafuatiliaji wa mambo kwenye eneo la maziwa makuu watakumbuka kuwa kiongozi huyo alikuwa amepigwa ban ya kusafiri.

Serikali ya Tanzania ilipoulizwa na kundi hilo la wataalam wa Umoja wa Mataifa kuhusiana Bigaruka kusafiri na kukaa Tanzania, ilidai haikuwa na taarifa za kiongozi huyo kusafiri na kuishi Tanzania na hatimaye kupotea kwake ghafla. Inasemekana mpaka sasa hajulikani alipo kiongozi huyo huku taarifa nyingine zikidai kuwa wamekamatwa na serikali ya Rwanda. Wataalam hao wa Umoja wa Mataifa wanaendelea kuchunguza kuhusiana na kutoonekana kwa Bigaruka. Kwa wale ambao siyo wavivu wa kusoma, link ya ripoti nzima ya UN ipo hapo chini.

============================================

m_Tanzania-politician-admits-hosting-FDLR-commanders-in-Dar-es-Salaam.jpg


A UN photo of Reverend Christopher Mtikila's residence in Dar Es Salaam, Tanzania, where FDLR second in command, Gen. Deogratias Nzeyimana, alias Bigaruka, stayed.

Reverend Christopher Mtikila has on several occasions hosted senior commanders of Rwandan FDLR rebels transiting through Dar es Salaam Tanzania in efforts to link them up with the outside work, the UN and the politician himself have confirmed. While in Dar es Salaam, they stayed at the personal residence of Rev. Mtikila which is identified in the photo above. According to UN Group of Experts report on DRC released on 24 January 2014, Reverend Mtikila confirmed to them that he had indeed hosted the FDLR political and military officials.

Disappearance of sanctioned FDLR leader Stanislas Nzeyimana (Bigaruka)

Early in February of 2013, one of the FDLR commanders from DRC disappeared. The UN experts say that while FDLR officers and intelligence sources from the region had told the Group that Rwandan officials were detaining Bigaruka, other FDLR sources alleged that Tanzanian security services placed Bigaruka under house arrest in Dar Es Salaam. The UN Group attempted to confirm this allegation with the Tanzanian authorities, which told the Group they were not aware of Bigaruka's travel and stay in Dar Es Salaam, and had no information about his disappearance or whereabouts.

The UN Group however documented Bigaruka's travel to Tanzania in violation of the travel ban imposed upon him. Three individuals, including Joseph Nzabonimpa (see S/2012/843, para. 101; Annex 40), told the Group that they – along with Faustin Murego – travelled to Dar es Salaam in January 2013 and met Bigaruka to discuss demobilization and disarmament as well as the issue of child soldiers (see annex 41).

At the beginning of his stay in Dar es Salaam, Bigaruka stayed in the house of Tanzanian reverend Christopher Mtikila, which the reverend acknowledged to the UN Group (see annex 42). In early February, after these meetings, Bigaruka disappeared. The Group continues to investigate the matter.

Source: United Nations Official Document

Ufafanuzi. Hii habari niliikuta allafrica.com ambao walisema wameitoa News of Rwanda. Nikatafuta News of Rwanda na kuikuta hiyo habari. Hata hivyo, News of Rwanda haikuwa primary source ya hiyo habari kwa sababu nao wenyewe wamesema kuwa wameitoa kwenye ripoti ya Wataalam wa Umoja wa Mataifa nchini Congo iliyochapishwa mwezi uliopita.

So, I had to find the actual report ya hao wataalam na kuisoma na kukuta kwamba actually News of Rwanda wamekopi sehemu ya hiyo report ku-justify habari ambazo wamekuwa wakiandika huko nyumba kuhusuana na suala hili. Kwa hiyo, the primary source ya hii habari siyo News of Rwanda, bali ni ripoti ya wataalam wa Umoja wa Mataifa nchini Congo iliyowasilishwa na kupitishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Tutofautishe kati ya primary source and secondary source.

Nilijua haya yatajitokoza na ndiyo maana niliweka mpaka link ya inapopatikana hiyo ripoti kwa ajili ya wale ambao siyo wavivu wa kusoma ripoti ndefu. Hata hivyo, wapo ambao wamedai kuwa kuwa link yenye hiyo ripoti haifunguki. Inawezekana kwa sababu ni ripoti ndefu kidogo ( ni PDF file lenye ukubwa wa zaidi ya 22MB), maana hata mimi ilinibidi nikatafute kinywaji kwanza wakati nikisubiri ripoti ifunguke.

For the avoidance of any double, badala ya kutoa link tuu, nime-download hiyo ripoti na kui-attach hapo chini. I hope sasa itafunguka. Riporti ina jumla ya kurasa 277. Kama ni mvivu wa kusoma au huna muda wa kuisoma ripoti nzima, nenda moja kwa moja kwenye ukurasa wa 27 hadi 28 (paragraphs 109 -110) na utaikuta hiyo habari kama ilivyonakiliwa na News of Rwanda.

Kuhusina na hiyo picha ya nyumba ya Mchungaji Mtikila pia News of Rwanda wameinakili kutoka kwenye hiyo ripoti. Picha inapatikana kwenye annex 42 iliyoko kwenye ukurasa wa 134 wa hiyo ripoti.

Kuna suala ambalo nilitegemea wachangiaji wangehoji lakini so far hakuna hata mmoja amefanya hivyo. Sijui kama ni usahaulifu au ni ignorance. Kama mtakumbuka hawa wataalam wa Umoja wa Mataifa walishawahi kutoa ripoti nyingine iliyoishutumu Rwanda kujihusisha na mgogoro huko DRC. Katika speech yake moja (ipo Yutube), Rais Kagame aliiwakandia sana hao wanaojiita "experts on the ground" na kuhoji wako accountable kwa akina nani. Kimsingi, aliitupilia mbali ile ripoti na experts wenyewe because they lacked accountability.

Lakini katika ripoti hii, inaonekena Rwanda wanakubaliana moja kwa moja baadhi ya findings za "experts" wale wale ambao Kagame aliwakandia na kuhoji uhalali na utaalam wao. How come ghafla, wamekubaliana na findings za hao "experts on the ground"? Ina maana sasa accountability ya hawa experts imebadilika tokea watoe ile ripoti ya awali?

Kwa upande mwingine, kabla ya shambulio la kigaidi la Westgate, kuna group la wataalam wengine wa Umoja wa Mataifa nafikiri on the Horn of Africa walitoa ripoti ndefu iliyokuwa na taarifa kuhusina uwezekano shambulio la kigaidi maeneo ya Afrika Mashariki. Katika ripoti hiyo, watalaamu hao walifanikiwa kuwahoji baadhi ya wapinganaji wa Al-Shabaab. Hata hivyo, inaonekana hapa Afrika Mashariki hakuna aliyehangaika na hizo findings za hiyo ripoti na shambulio la kigaidi Westgate lilitokea miezi michache tuu baada ya ripoti hiyo kuchapishwa.
 
Kwa uzoefu wangu kiasi niseme wazi ningekuwa Kikwete nisingejiingiza ktk hizi mishemishe za matatizo ya nchi za Maziwa Makuu wakati muda wangu unaisha na kama nchi hatuna sera rasmi kuhusu migogoro ya muda mrefu ktk eneo hilo. Kwa Mtikila kusema hivyo ni kucover face ya Watawala. Mtikila atamwalika vipi na kumwingiza nchini mtu anayekabiliwa na vikwazo vya UN?

Na niseme hiki kibarua anachotumika Mtikila sasa, na kampeni yake ya kuchochea chuki kwa Watutsi sitashangaa akimaliza maisha yake ktk jela za UN!
 
Mtikila sio Mchungaji,huyo kajivika tu,huyo ni mtafutaji pesa,aliwahi kuwatisha wahindi,wakamchangia pesa,mchungaji amiliki hekalu kama hilo. nyie pigeni blabla tu,mnaliwa na wanasiasa.subirini muanze kuuana zaidi ya sasa ya utekaji ya wakina Kileo
 
EMT cc jmali, rushasha aka mume wa shetani, mokala 1989 aka majeshi 1981 aka (foot soldier wa bigaruka)
 
Last edited by a moderator:
Asante sana kwa taarifa mkuu. Nilisoma hii ripoti mahali fulani. Pia nikasoma kuwa kuna wana "usalama" wa Tanzania wali-demand US$5million for the "general" Bigaruka wakanyimwa, dau likashuka mpaka $3million. Inasemekana amekamatwa na DMI agents akiwa Kigoma. Hongera sana Pres Kagame na DMI yako makini kwa kumkamata gaidi huyu hatari kwa usalama si tu wa Rwanda bali pia eneo la maziwa makuu. Ushauri wa bure, moja Mtikila achukuliwe hatua kwa kuwakirimu magaidi wa FDLR na kutetea mauaji ya halaiki. Pili, Tanzania tusikubali ardhi yetu itumiwe na hawa wauaji wa FDLR.
 
Usiwashushe watanzania kiasi hicho mkuu.
Hiyo ni nyumba ya kawaida sana

Usijidai na wewe ni Mtanzania unayefahamu maisha yetu. Hilo jumba la Mtikila hapa karibu na shule ya msingi Ushindi Mikocheni B nalifahamu zaidi ya miaka 20. Alifanani kabisa na anavyotaka kujionyesha kwamba yeye ni mtu mnyonge. Anaweza danganya malofa tu waliokuja mjini ukubwani!
 
Usijidai na wewe ni Mtanzania unayefahamu maisha yetu. Hilo jumba la Mtikila hapa karibu na shule ya msingi Ushindi Mikocheni B nalifahamu zaidi ya miaka 20. Alifanani kabisa na anavyotaka kujionyesha kwamba yeye ni mtu mnyonge. Anaweza danganya malofa tu waliokuja mjini ukubwani!
Ni nyumba ya kawaida, mkuu.
 
Ni nyumba ya kawaida, mkuu.

Hilo ghorofa nalifahamu sana hakuna Mtanzania wa kawaida anaweza jenga tena miaka hiyo. Huyu jamaa yako kaanza mishemishe muda mrefu sana. Akabanwa,akakata tamaa mpaka walipokuja wapiga deal akina RA ndipo akaanza kufufua gofu lake!
 
Back
Top Bottom