BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,120
Waziri wa Fedha na Mipango Dk Mwigulu Nchemba amesema bungeni jiji Dodoma kuwa mradi huo ni miongoni mwa miradi 48 ambayo serikali inakusudia kuiendesha kwa ubia na sekta binafsi.
Benki ya Dunia na wadau wengine imebainisha jumla ya miradi 48 inayoweza kutekelezwa kwa utaratibu wa ubia na sekta binafsi.
Miradi mingine ni Reli ya Mtwara-Bamba Bay; Uendeshaji wa Reli (Rolling stocks); Uendeshaji wa Barabara ya haraka (expressway) kutoka Igawa-Tunduma; Barabara za 38 kupunguza msongamano katikati ya Jiji la Dar es Salaam (Inner and Outer Ring Roads); Barabara za haraka kutoka Kibaha Chalinze - Morogoro hadi Dodoma na kuunganisha Jiji la Dodoma na Dar es Salaam kwa barabara za haraka; Bandari kavu katika eneo la Kisiwa/Mgao – Mtwara; na Kuboresha na Upanuzi wa bandari katika Ziwa Victoria - Mwanza na Nansio - Ukerewe.
Mwigulu amesema utaratibu huo ni sehemu ya mpango wa kimkakati wa serikali kushirikisha sekta binafsi ambayo ilipewa jukumu la kugharamia asilimia 17 ya bajeti karibu Sh trilioni 21.