Acha utani jamaa angu pale madrid wale viungo wenu kina Tchouameni na Camavinga sio wa kumuweka Rodri nje au eti Rodri agombanie nao namba.
Na suala la umri pia uongo tu mbona mmemsajili Bernado Silva miaka 31 wakati Rodri 30?
Mpaka hapo haujagundua kwamba tupo frequency tofauti?
Hauoni unachokazania wewe na ninachomaanisha Mimi ni vitu viwili tofauti.
Baernado alikua free,Rodri ana mkataba hauoni utofauti hapo?
Ni kweli Real Wana shida ya kiungo mkabaji ila Kwenye project za Mda mrefu target yao ya kwanza hua Kwa vijana wadogo ambao watatoa huduma Kwa muda mrefu na Ikitokea wamekosekana basi hata hao wenye umri wa Rodri ambao wapo Kwenye kiwango kizuri ila tu wawe tayari kucheza sio majeraha ya mara Kwa mara Kwa sababu Wao wanatumiwa Kwenye project ya muda mfupi
tu.
Sasa swali Rodri msimu uliopita katoa huduma Gani Kwenye club yake? Hajacheza hata nusu ya mechi za msimu, kajakupona kacheza mechi 7sijui 8 za word cu na bado karudi kufanyiwa tena operation.e
Sasa unataka Perez atoe Hela ndefu Kwa kamari kama hiyo? Carvajal kastaafu hapa juzi tu akiwa bado anahitajika je tatizo lilikua kiwango, umri au majeraha?
Majeraha kwanza Kisha umri, Sasa hata rodri vivyo hivyo, yawezekana ana kiwango kizuri kweli ila vipi akifika akae nje tena msimu mzima Huku kasaini mkataba wa miaka miwili tu?
So Mimi Sina tatizo na ubora wake nitafurahia akija ataongeza upana wa kikosi.
Ila Nina wasiwasi na afya yake, kwahyo Kitu kikubwa backup ya kina Camavinga na tcho isiondoke kwanza.. Kwa sababu afya yake haieleweki inaweza kuchochea majeraha ambayo yatafanya asicheze au acheze bila kutoa kiwango stahili.I
Ndomana nikasema Anaogopa kuanzia benchi.
Itokee Camavinga gari limewaka, Tcho Gari limewaka ni sawa na Rodri akiwa mgonjwa?
Sema natumia nguvu nyingi sana kuelekeza Mwana Barca wengi Wao ni Vilaza Hawa hahahaha.