Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

GOAL! Vinícius fires the equaliser quickly! Real Madrid 1-1 Arsenal (agg 1-4)

CgAGVmgAFA-AECP0ACOyO88b7qY034.gif
 
Tujipange tu kwa msimu ujao, ninadhani itakuwa bila Ancelloti.,
Kama tulivyosema nyakati nyingi hapa,timu kwa ujumla inahitaji mabadiliko makubwa sana,kuanzia eneo la beki hadi katikati pale,beki za kati na pembeni zipo hoi,haswa za pembeni,kaumia Carvajal basi kila mahali ni tobo hakuna muongozaji wa eneo la ulinzi,katikati hapo Valverde nafikiri ni uchovu sana na kuhamishwahamishwa namba,Tchoumeni na Ceballos ni wafangakazi hewa,hata Camavinga pia...hili eneo linahitaji mabadiliko makubwa sana...babu Modric huu uwe msimu wa mwisho kwake,hawa madogo kama hawaaminiwi basi watolewe...eneo la kati kwa maana ya namba 6 tunahitaji watu katili kweli kweli wenye uwezo wakunusa hatari na wanaoweza kujitoa kwa timu,huyu Fran Garcia kashindwa hata kuchukua kadi nyekundu kwa faida ya timu hata iwe draw..benchi la ufundi nalo litoke tu maana mbinu zao zimeshapitwa na wakati.

Yote kwa Yote,tuonane msimu ujao,huu kwetu umeshakwisha kwa aibu..tutarudi tukiwa imara msimu ujao.
 
Back
Top Bottom