Nimesoma michango ya wadau wengi humu juu ya team yetu na namna inavyochelewa kwa ujumla.
Niseme tu hivi, tunacheza vile kutokana na aina ya wachezaji tulionao na experience ya team kwa ujumla, team yetu bado ipo kwenye transition, tuna team ya vijana wadogo wanaokuja, tunaona wanafanya makubwa uwanjani ila bado hawajakomaa kihivyo, kufanya makosa kwao ni jambo la kawaida, sasa kocha usipokuwa makini unaweza kujitukuta unapoteza kazi kijinga.
Ancelotti anachofanya ni kutumia silaha alizonazo vizuri kufanikisha malengo yake, na hapo ninamuelewa vizuri sana.
Anajua ana vijana wazuri kwenye kuzuia ana kiungo mzuri kwenye kufanya transition na ana washambuliaji wazuri na wenye speed, so yeye anatembea na hiyo falsafa yake, maana yake atabadilika kutokana na mpinzani atayekutana nae.
Anajua akicheza na City ama Barcelona hawa silaha yao ni kumiliki mpira mara nyingi, sasa yeye haendi kushindana nao kumiliki mpira, ila anaenda kuangalia namna ya kuwapiga kwenye udhaifu wao., ukisema sie tucheze kama fulani utapotea.