Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Leipzig wana speed ya kutosha, tulianza game vibaya wakatuadhibu, ila kwa dakika hizi za mwisho team imerudi kwenye mstari, ninaona Rüdiger na Nacho wamebadilishana post, sijui ni maelekezo ya Ancelloti ama ni wao wenyewe, ila kiukweli hayo mabadiliko yametupatia ahueni.
 
Leipzig walicheza vizuri sana, waliweza kuona madhaifu yetu wakatuadhibu,
Kwa upande wetu vijana walijitahid, ila kuna haja ya kuongeza umakini na morale ya ushindi kwa vijana wetu., kuna muda ninatamani Vinicius apate ule userious kama wa Rodrygo mbele ya goli la mpinzani., ila ni bahati mbaya huwezi kupewa vyote, ila anahitajika kujitahidi.,
Anapoteza nafasi nyingi sana kiukweli.,
 
Leo tulikua wabovu juu ya ubovu, defence yote chali, line up haikuwa nzuri.

Rw hakuna alichofanya asensio mara 1000 ya Valverde. Vin anatupoteza sana
Set up ya defence yetu haikuwa sahihi, ndio maana Rüdiger na Nacho walibadilishana majukumu kati kati ya mchezo., goli la tatu pia ni matokeo ya kutojipanga, ule up and e alikuwa anacheza Kroos, kucover hilo eneo endapo Nacho amepanda, ila baada ya kutoka Camavinga hakuenda kucover lile eneo, na Rüdiger hakufanya hivyo pia, so tukaacha nafsi kubwa sana kule upande wa kushoto,
Ni vizuri kufanya makosa katika hatua hizi, tunapata muda mzuri wa kurekebisha, kuliko kuja kupata shida kama hizi kwenye hatua ya mtoano.

Vinicius anacheza vizur akiwa na Benzema tu, sijui anamuheshimu ama ni vp, ila kiukweli sikumbuki ni lini alimtengenezea Rodrygo nafasi., ila Rodrygo alishawahi kumtengenezea nafasi., ajitafakari.
 
Hazard anashida gani huyu jamaa?
Anahitaji kupata muda mwingi zaidi kucheza ili angalau arudi kwenye nusu ya kiwango chake, hapo Madrid hawezi kupata hiyo nafasi, kama nilikuwa mshauri wake, ningemshauri atafute team ya daraja la chini, atapata huo muda wa kucheza bila presha ya kutakiwa kuonyesha kiwango chake cha zamani.
 
Back
Top Bottom