Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Casemiro kuondoka kwa mimi naona ni sawa,kwa sababu ameshinda kila kitu kwa ngazi ya club akiwa madrid hapa,ni wakat muafaka wa yeye kutafuta hela sasa zakustafu...huyu Mariano sijui kwa nini huwa tunamuweka kikosini,awekwe sokoni.
Mkuu Mariano ni tatizo kubwa, yule jamaa ni mbinafsi sijawahi ona, kinachomfanya abaki clubini licha ya kutopewa nafasi ni mshahara wake man, hataki kulipwa pungufu ya mshahara anaopata kwasasa, msimu uliopita club ilifikia makubaliano na Rayo Vallecano, ila jamaa akachomoa kwa kuwa jamaa hawakuwa tayari kumpa mshahara anaolipwa kwasasa.,
Akisema apunguze mshahara tu, kesho atapata club, so ninaona anazuga ili mkataba wake uishe ili achague sasa sehemu ya kwenda.
 
Ukiangalia Casemiro ameshafika kwenye peak na kwa club yetu hakuna ambacho hajashinda,so kind hata ile morali inakuwa imeshuka...lakini pia kwa misimu miwili hii ukiangalia vizuri utaona hata kiwango chake kimeshuka kias flan...ni wakat muafaka kwa yeye kuondoka lakini pia ili club iweze kuwatumia hawa vijana waliosajiliwa vizuri,tuna kundi kubwa sana la vijana ambao wanaweza cheza namba yake.
Ni kweli kabisa, Hata Ancelotti atakuwa amemwelewa kwenye angle hiyo, kuwa hakuna dalili ya yeye kupiga tena mpunga mrefu siku za usoni,ndio maana akashindwa kuchomoa hii nafasi aliyoipata.
Kwa kiwango kushuka ni kweli kabisa, msimu uliopita lawama zilikuwa nyingi sana, ndio maana hata club ikaamua kufanya usajili kwenye nafasi yake, ila kama msimu huu nimeona amekuwa wa moto sana, labda ni baada ya kuletewa mbadala.,
Nimtakie kila la kheri,
 
Real Madrid bought Casemiro for only €6M in 2013 from Sao Paulo, since then:

Played 336 games.
Scored 31 Goals.
Gave 29 assists.
Won 18 trophies (5 of them are UCL).
Gave everything on the pitch.

A true legend of Real Madrid. And they sold him for 70 Million.
what a Business
 
Umewahi kuiona madrid yenye claude makelele au ulisimuliwa. Tuliofanikiwa kuiona ngoja tukae kimya utuambie wewe.


Wakati Real anakula kipigo cha mbwa koko na cha aiabu kutoka kwa Juventus ya akina del Piero na Nedved je Makelele hakuwepo kwenye timu muda ule?
kile kipigo ndicho kilichomaliza ubabe wa real ulaya kwa zama zile.
 
Wakati Real anakula kipigo cha mbwa koko na cha aiabu kutoka kwa Juventus ya akina del Piero na Nedved je Makelele hakuwepo kwenye timu muda ule?
kile kipigo ndicho kilichomaliza ubabe wa real ulaya kwa zama zile.
unaizungumzia ile mechi moja je baada ya kumuuza makelele nini kilifuata. Na kabla hajauzwa moto wa real madrid uliuona.
 
unaizungumzia ile mechi moja je baada ya kumuuza makelele nini kilifuata. Na kabla hajauzwa moto wa real madrid uliuona.

moto wa real uliishia kwneye kile kipigo, haikuogopewa tena baada ya pale.

Na Huyo Makelele hakua starter kwenye timu kwa zaidi ya miaka mitatu tu, alianza kucheza baada ya kuondoka kwa redondo kwenye timu.
 
Don Carlo ameanza na vijana hawa.,
1661022826604.png
 
Bado tuna tatizo la ku control mchezo.
Mkuu, ku control mchezo kwetu ina maana kufunga, ama kupata magoli, ishu ya umiliki wa mpira wala sio ishu sana kwa Ancelotti., kila game huwa ana namna ya kuingia, Hawa Celta ni watundu sana kwenye kuchezea mpira haswa wakiwa kwao, so ili kuenda nao Sawa ina maana ni kuwafunga.
 
Na ndio huwa kipindi chetu cha ushindi
Hazard ndio tu katuangusha, tulitakiwa tuwapige jamaa Tano kabisa.
Mchezo ulikuwa mzuri, wale vijana wa Kifaransa wamefanya vizuri tu kiukweli,Valverde na Mendy na Militao ndio kidogo walikuwa hawapo kwenye mchezo muda wote., ila wamejitahidi, sio rahisi kuwafunga Celta kwao..
 
Babu modric anazeeka na utamu wake katupia chuma Cha pili
Kwa umri alionao na vitu anavyofanya uwanjani ni hatari sana, unatamani aendelee kucheza tu., ile pasi ya goli la Vinicius Jr ni hatari sana., bado anahitajika sana ndani ya kikosi, acha tuendelee kufurahia kipaji alichopewa.,
 
Mkuu, ku control mchezo kwetu ina maana kufunga, ama kupata magoli, ishu ya umiliki wa mpira wala sio ishu sana kwa Ancelotti., kila game huwa ana namna ya kuingia, Hawa Celta ni watundu sana kwenye kuchezea mpira haswa wakiwa kwao, so ili kuenda nao Sawa ina maana ni kuwafunga.
Mkuu uliangalia mechi? Especially kipindi cha kwanza?
 
Back
Top Bottom