Richard spencer
JF-Expert Member
- Feb 22, 2021
- 1,301
- 2,126
Ni kweli, pia vijana waliopata nafasi msimu uliopita hawakutuangusha, hiyo inatupa mwanga hata Modric na Benzema wakiondoka bado tutakuwa na watu wenye uzoefu na haya mashindano.Hii ndio maana halisi ya Ligi ya Mabingwa, huwa ninakuwaga na amani sana pindi tu tunapopangiwa kukipiga na hao wakali, ina maana unapata kipimo sahihi mapema, so ukifanikiwa kupita hapo hata morale ya wachezaji inakuwa juu sana.
Ninakumbuka baada ya kuwatoa PSG Modrić alisema kuwa hii ni mpaka final, kwamba kuvuka pale haikuwa rahisi, so hawakuoana tena team ya kuwasimamisha.
Niwe muwazi, katika vijana wetu wote Vinicius amenishangaza hasa kuanzia msimu uliopita.