Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Hii ndio maana halisi ya Ligi ya Mabingwa, huwa ninakuwaga na amani sana pindi tu tunapopangiwa kukipiga na hao wakali, ina maana unapata kipimo sahihi mapema, so ukifanikiwa kupita hapo hata morale ya wachezaji inakuwa juu sana.
Ninakumbuka baada ya kuwatoa PSG Modrić alisema kuwa hii ni mpaka final, kwamba kuvuka pale haikuwa rahisi, so hawakuoana tena team ya kuwasimamisha.
Ni kweli, pia vijana waliopata nafasi msimu uliopita hawakutuangusha, hiyo inatupa mwanga hata Modric na Benzema wakiondoka bado tutakuwa na watu wenye uzoefu na haya mashindano.

Niwe muwazi, katika vijana wetu wote Vinicius amenishangaza hasa kuanzia msimu uliopita.
 
Tumeshinda ila kwa mbinde vini Lucas toni under perform
Ninadhani baada ya Casemiro mtu atayefuata kuondoka inawezekana ikawa Toni Kroos., ilitegemewa kuwa mwaka huu angeongeza mkataba ila alighairi, so sitashangaa kusikia anataka kuondoka msimu ujao, suala la msingi ni Ancelotti aendelee kumpa nafasi Camavinga ili iwe rahisi kwenye hiyo transition.
 
Jana nilishindwa kuangalia game yetu, hata kwa simu tu ilishindikana., ninafurahi kusikia kama kijana anaendelea vizuri., kiukweli amekuja wakati muafaka.
Madogo wakiendelea vile aise tuna timu..
Game ya jana ilikua mchaka mchaka haswaaa.. Tilikosa utulivu tu kwenye umaliziaji.. Ila madogo wanajua kupeleka timu mbele..
 
Tumeshinda 2 kwa 1 Ila tunaruhusu sana magoli
Nimeangalia kipindi cha pili tu, ni kweli karibia kila game tunaruhusu goli sijui shida ni nini, japokuwa tumecheza na team ngumu, Betis wanacheza vizuri sana, tumewafunga kwa uzoefu, ila walikuwa poa, sijui kipindi cha kwanza kilikuwa vipi.
Muhimu ni point 3 na tumezipata, suala la msingi ni Mwalimu kurekebisha makosa kulipo na mapungufu.
 
Kweli, kwa kipindi cha pili nilichoangalia, jamaa sijui ana shida gani, ninadhani hajiamini, pia kiungo kidogo tulikuwa slow sana,
Nadhani ni muda sahihi sasa Alaba aende kushoto Rudiger aingie kati.
Kwenye kiungo mzee baba tangu kipindi cha kwanza tunastruggle labda hatukutegea ule upinzani. Pia Betis ni wa 2 kwenye msimamo na wanafundishwa na Pelegrin kwahiyo wanaonekana wamejipanga msimu huu.
 
Nadhani ni muda sahihi sasa Alaba aende kushoto Rudiger aingie kati.
Kwenye kiungo mzee baba tangu kipindi cha kwanza tunastruggle labda hatukutegea ule upinzani. Pia Betis ni wa 2 kwenye msimamo na wanafundishwa na Pelegrin kwahiyo wanaonekana wamejipanga msimu huu.
Ancelotti anadai kuwa hawezi kufanya majaribio wakati ana combination iliyobora na iliyemletea kombe, ila huko tuendako ni lazima atafanya hayo mabadiliko., ninadhani anasubiria Rudiger azoee mazingira, bado jamaa ninadhani anajiona kama bado anacheza Chelsea hivi, hajatulia,
Kwenye kiungo jamaa walikuwa wengi halafu na sisi ukabadili wetu haukuwa wa kasi so kuzidiwa ilikuwa dhahiri, ila alipoingia Valverde speed iliongezeka ndio tukapata goli la pili.
 
Back
Top Bottom