Ni vigumu sana kumsajili Dybala Mkuu, kwanza sio mashabiki wa Real Madrid, pili huo upande kama tukimkosa Mbappé basi atabaki Rodrygo na Asensio, ila tunahitaji Winger mmoja either wa kulia ama wa kushoto hapa inategemea na hatma ya Eden Hazard, kisha Striker mbadala wa Karim, jamaa umri unaenda ila plan ya club ni kumtumia jamaa mpka mkataba utapoisha hapo mwakani June 2023., ndio maana hata ishu ya usajili wa Haaland umekuwa mgumu kwa kuwa club kuanzia msimu wa 2023/2024, wakati yeye anataka kuanza msimu ujao wa 2022/2023.
Wakati huo huo tunahitaji mbadala wa Casemiro, na kijana aliye sokoni kwasasa ni yule dogo wa Monaco Aurelien Tchouameni, ila huyo ninadhan dau lake litakuwa kubwa, kwasababu Club kibao zinamfuatulia na yeye ameshaaga ndani ya club kuwa anataka kuondoka, Sasa sijui kama tutashtukizwa na club kama ilivyokuwa kwa Camavinga ama ndio itabidi tumlinde Casemiro na tumpandishe Antonio Blanco ama tutacheza na double pivot, kama tulivyo fanya dakika za mwisho na 30 za nyongeza dhidi ya Manchester City kwa kumchezesha Camavinga na Valverde ama itakuwaje, majibu ni kuanzia Mwezi wa Sita.