Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Mendy hapana bora Marcelo ni mzigo kwenye team ile penalty ya kizembe kabisa alf jamaa ni mzito in short hana kiwango cha kucheza RMA aondoke tu anajua hana speed harafu ana panda tukipigwa counter attack anachelewa jana Couture kafanya saves nyingi kwa uzembe wake
 
Mendy hapana bora Marcelo ni mzigo kwenye team ile penalty ya kizembe kabisa alf jamaa ni mzito in short hana kiwango cha kucheza RMA aondoke tu anajua hana speed harafu ana panda tukipigwa counter attack anachelewa jana Couture kafanya saves nyingi kwa uzembe wake
Mkuu penalty moja ndio awe mzigo kwenye team!? Kiukweli Mendy ameimarika sana kwasasa tofauti na msimu uliopita, makosa kwenye mpira yapo, kama uliangalia mpira vizuri mashambulizi mengi ya Valencia yalipitia upande wa kulia na wala sio kushoto kwa Mendy.
Kuna utofauti kati ya Mendy na Marcelo, Mendy sio mzuri kukaa na mpira ama kwenye mbele kusaidia mashambulizi (japokuwa jana alishirikiana vyema sana na Vinicius), uwepo wake uwanjani unasaidia kubalance team kwenye ulinzi, ila Marcelo akiwa uwanjani tegemea mashambulizi mengi kutoa kwake (japokuwa na yeye siku hizi hayupo poa) , ila anaacha nafasi kubwa sana ya kulinda, zamani Casemiro ndio alikuwa ana cover nafasi yake wakati anapanda kwenye kushambulia, ila kwasasa vijana wetu wamechoka, sio rahisi ku-cover eneo kubwa sana kihivyo, hapo ukizingatia Casemiro inabidi alinde kati kati kisha arudi kulia kumsaidia Vasquez kwenye aerial balls, hapo vuta picha yupo na Marcelo ndani, utaona namba team inavyopata shida kwenye Ulinzi.
Marcelo a nafasi kucheza kwenye zile team wanazobaki nyuma kukaba, hapo atatusaidia sana kwa kuwa ni mzuri kwenye kushambulia na wakati huo huo hatuna threat kubwa sana ya adui kutushambulia.
 
Kila siku zinavyozidi kwenye huyu Jr anazidi kupevuka na anapata utulivu wa akili
Kijana kiukweli amepevuka, anajitahid sana, nilipoona kuwa ameajiri kocha wake binafsi kwa ajili ya mazoezi ya viungo nilijua tu kuwa amedhamiria kuwa Sawa na kufocus kwenye mpira, ana mwili wa kiasi ila ana stamina ya kutosha, pia upigaji wake wa mpira umebadilika sana,
Ninatamani na mwezie Rodrygo apate kocha wake binafsi haswa wa viungo, dogo akipigwa push tu anaenda, akijijenga na yeye plus a Mbappé kama atakuja tutakuwa na team ya vijana wadogo nzuri sana.
 
Afadhari Theo Hernandez arudi
Theo hawezi kurudi, halafu kwanza hatuna shida na beki wa upande wa kushoto, tuna shida na beki wa upande wa kulia, Carvajal anaumia mara kwa mara sana, so ni afadhali Hakimi arudi kwa upande wangu ninavyoona kuliko Theo, japokuwa wote hawana dalili za kurudi (labda Hakimi kwa kuwa bado ana nia ya kuvaa uzi mweupe, kijingi kipo kwa club anayoitumikia kwasasa).
 
Mkuu penalty moja ndio awe mzigo kwenye team!? Kiukweli Mendy ameimarika sana kwasasa tofauti na msimu uliopita, makosa kwenye mpira yapo, kama uliangalia mpira vizuri mashambulizi mengi ya Valencia yalipitia upande wa kulia na wala sio kushoto kwa Mendy.
Kuna utofauti kati ya Mendy na Marcelo, Mendy sio mzuri kukaa na mpira ama kwenye mbele kusaidia mashambulizi (japokuwa jana alishirikiana vyema sana na Vinicius), uwepo wake uwanjani unasaidia kubalance team kwenye ulinzi, ila Marcelo akiwa uwanjani tegemea mashambulizi mengi kutoa kwake (japokuwa na yeye siku hizi hayupo poa) , ila anaacha nafasi kubwa sana ya kulinda, zamani Casemiro ndio alikuwa ana cover nafasi yake wakati anapanda kwenye kushambulia, ila kwasasa vijana wetu wamechoka, sio rahisi ku-cover eneo kubwa sana kihivyo, hapo ukizingatia Casemiro inabidi alinde kati kati kisha arudi kulia kumsaidia Vasquez kwenye aerial balls, hapo vuta picha yupo na Marcelo ndani, utaona namba team inavyopata shida kwenye Ulinzi.
Marcelo a nafasi kucheza kwenye zile team wanazobaki nyuma kukaba, hapo atatusaidia sana kwa kuwa ni mzuri kwenye kushambulia na wakati huo huo hatuna threat kubwa sana ya adui kutushambulia.

Acha kumtetea Mendy huyo jamaa ni wa ovyo kabisa
 
Theo hawezi kurudi, halafu kwanza hatuna shida na beki wa upande wa kushoto, tuna shida na beki wa upande wa kulia, Carvajal anaumia mara kwa mara sana, so ni afadhali Hakimi arudi kwa upande wangu ninavyoona kuliko Theo, japokuwa wote hawana dalili za kurudi (labda Hakimi kwa kuwa bado ana nia ya kuvaa uzi mweupe, kijingi kipo kwa club anayoitumikia kwasasa).

Mkuu una tatizo sehemu, Mendy ndio mchezaji mbovu zaidi uwanjani
 
1642009542499.png
 
Naam., Ni usiku mwingine tena wa Kabumbu, Leo ikiwa ni El Classico kwenye Super Cup de Espana., ila game ya leo itapigwa huko Riyadh, Saudi Arabia.
Line up yetu ya leo ni kama ilivyo hapo juu.
 
Back
Top Bottom