Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Oyaaaa nyie matakataka Kuna ambaye hajacheki mechi Jana?? ...basi tunaombea iludiweee iludiweee ili muone mpira mwingi hamjapata ona..

Chelsea Champions UEFA,...

Msimu ujao jipangeni Kama tukikutana tusiwabamize Tena bao nyingi..
Hahahahah
 
Uzi sijaukubali kabisa wadau
realmadrid_1622581574606637.jpg
realmadrid_1622581574606463.jpg
realmadrid_1622581574606106.jpg
 
Carlo Bernabeu ni nyumbani reappointment yake nmeipenda
Sure, mwenyewe ninadhani amependa kurudi., acha aje atujengee tena team ya ushindani, na amekuja muda muafaka Kabisa, sijui atafanya vp ila ni matumaini yangu kuwa atatutengenezea kikosi bora cha ushindani.
Nimeona pia atamrudisha yule coach wetu wa viungo Antonio Pintus na Alvaro Arbeloa atakuwa Assistant coach
 
Ancelotti ninaona hataki shida, ni chap ameshaanza kazi kutengeneza bench lake la ufundi, acha tuone kama this time kweli amedhamiria kurekebisha alichokosea kipindi kile ama amekuja tu kwa kuwa amehitajika na Real Madrid
 
Kwa kumfuatilia vizuri Carlo pale Everton naona kama mbinu zake zinaelekea mwisho wa matumizi maana sikuona chaajabu alichofanya na usajili alioufanya ulikuwa wa wachezaji wazuri kwa level ya everton...... Madrid kwanini mmeamua kucheza kamari nyingine?
 
Hii timua rudisha hii, kwa upande mwingine itazidi kutuaminisha kuwa timu ndiyo yenye mapungufu na sio makocha waondokao na kurudishwa kila leo. Japo kwa namna moja ama nyingine inaweza kutoa fursa ya kurekebisha makosa yaliyopita kwa pande zote.
 
Oyaaaa nyie matakataka Kuna ambaye hajacheki mechi Jana?? ...basi tunaombea iludiweee iludiweee ili muone mpira mwingi hamjapata ona..

Chelsea Champions UEFA,...

Msimu ujao jipangeni Kama tukikutana tusiwabamize Tena bao nyingi..
Hahahahah
We kima rudi kwenye jukwaa lako hili ni maji marefu na ki club chenu ulichoaanza kukijua Jose morinho alipoanza kuwa manager.
Usivamie uzi wa club kubwa ambayo hata robo ya vikombe vyake vya kimataifa hamjawai ifikia
 
Ancelotti ninaona hataki shida, ni chap ameshaanza kazi kutengeneza bench lake la ufundi, acha tuone kama this time kweli amedhamiria kurekebisha alichokosea kipindi kile ama amekuja tu kwa kuwa amehitajika na Real Madrid
Huyu ancelloti huyu mtamkumbuka Zidane.
 
We kima rudi kwenye jukwaa lako hili ni maji marefu na ki club chenu ulichoaanza kukijua Jose morinho alipoanza kuwa manager.
Usivamie uzi wa club kubwa ambayo hata robo ya vikombe vyake vya kimataifa hamjawai ifikia
Sasa mkuu hutaki kukubaliana na ukweli? Hii Madirid kuja kubeba uefa tena ni baadae miaka kumi uko, hutaweza tena kujenga kikosi cha ushindani kama mile cha Cr7. Kwa sasa clabu za England zitatawala soka la Ulaya. Huku zikiongozwa na mfalme wa London CHELSEA.
sasa basi uwezekano wa Carlo kuwin ndani ya Madirid ni kama hauko vile ..
Bado unayo nafasi ya kuweza kuchagua either timu moja wapi kati zile NNE pale England.
#CFC
 
Sasa mkuu hutaki kukubaliana na ukweli? Hii Madirid kuja kubeba uefa tena ni baadae miaka kumi uko, hutaweza tena kujenga kikosi cha ushindani kama mile cha Cr7. Kwa sasa clabu za England zitatawala soka la Ulaya. Huku zikiongozwa na mfalme wa London CHELSEA.
sasa basi uwezekano wa Carlo kuwin ndani ya Madirid ni kama hauko vile ..
Bado unayo nafasi ya kuweza kuchagua either timu moja wapi kati zile NNE pale England.
#CFC

Sawa zile tatu mfululizo zinatutosha sana tupumzike kwanza tukirud kama kawaida yetu mtakuwa mnaisoma namba tu
 
Kwa kumfuatilia vizuri Carlo pale Everton naona kama mbinu zake zinaelekea mwisho wa matumizi maana sikuona chaajabu alichofanya na usajili alioufanya ulikuwa wa wachezaji wazuri kwa level ya everton...... Madrid kwanini mmeamua kucheza kamari nyingine?
Mbinu zake bado zipo poa, hata pale Everton alifanya vyema tu, shida ya Ancelotti ni moja tu, huwa anapenda kuwa na kikosi kidogo na hilo ndio mara nyingi huwa linamletea shida, kwa mfano pale Everton James akiwa nje kwa majeruhi basi walikuwa wana yumba, na hata ule msimu wa mwisho kwetu kilichomletea shida ni kikosi kidogo alichokuwa nacho, Sasa na juzi nimesikia akisema tena kuwa anataka apunguze wachezaji, ninaona anaelekea kule kule.
Ila acha afanye anachoweza kwasasa club inamwandaa Raúl,
 
Back
Top Bottom