HII NDIO INAITWA TEAM WORK
Hongera sana CHELSEA FOOTBALL CLUB, leo ngoja niongelee kile nilicho kiona kwenye mchezo wa jana kwa mchezaji mmoja mmoja.
THOMAS TUCHEL : Nikianza na kocha, aisee huyu jamaa yuko poa sana. Jana kaingia na mbinu tofauti kabisa ata Zidane alishangaa sana kuona tuko vile. TT alikubali Madrid wamiliki mpira vile watakavyo ila shida ilikuwa ni jinsi gani wanaweza kuzifungua beki za Chelsea na kupata goli. Unajua ni kwann TT hutumia mfumo wa 3-4-3? We kwenye akili yako ama kuona utaona ni mabeki 3 ndio wanazuia lakini ukweli wa mambo ni mabeki 6. Hii imekuwa ngumu sana kwa timu pinzani kupata goli ndio maana Chelsea mara nyingi wanaondoka na clean sheet, ama ikitokea akafugwa basi atafungwa goli chache tu. Jana TT kaingia kwa kuzuia na kushambulia kwa kushtukiza, pindi Chelsea akiwa na mpira alikuwa anafika kwenye lango la Madrid kwa upesi sana. Madrid wao waliona ni kheri kupiga pasi tu. Big up sana TT
EDOUARD MENDY : Huyu jamaa kadri siku zinavyo zidi kuja ndio anazidi kuwa bora zaidi, moja ya magolikipa bora kabisa Duniani. Zile saves alifanya jana na kwenye game ya Fulham unabaki unajiuliza huyu ni mtu kweli.! Mimi ndio maana huwa namuita JINI, kipa anajiamini sana huyu. Mendy ana kila sifa ya kuwa golikipa bora, ana 16 clean sheet za epl huku uefa akiwa na 8.
CHRISTENSEN : Huyu dogo kuna kipindi tuliona hafai ila now days kabadilika sana. Dogo anazuia vizuri sana huyu, kuna kipindi nisipo muona kwenye kikosi naumia kabisa. Jana kacheza poa sana, kuna kipindi alipokonya mpira kisha alie kuwa na mpira akabaki anavuta soksi tu aisee nilicheka. Dogo anakuja vizuri sana
SILVA : Daah! Wengi walitucheka sana kuhusu usajili huu ila huyu jamaa amewaacha midomo wazi wamebaki na aibu zao tu. Beki mmoja mtulivu asie na papara kwenye maamuzi, Benzema alishikwa vilivyo.
RUDIGER : What a Player.! Huyu jamaa kwa anacho kifanya kwa sasa unaweza kuamini yale maneno yalio kuwa yakizagaa mitaani kuwa alianzisha mgomo ili Lampard atoke. Rudiger amebadilika sana anazuia vizuri sana mbaya ama nzuri zaidi anashamhulia pia. Kinacho nifurahisha zaidi anaelewana sana na mabeki wenzake akipanda basi Silva na Christensen wako nyuma kuweka ulinzi. Huyu jamaa ndio injini pale nyuma kwe safu ya ulinzi. Jana Madrid hawakuweza kufurukuta kabisa.
AZPILICUETA : Siku zote ukiwa kiongozi basi inabidi uwe mfano kwa watu wako. Hicho ndio alikifanya jana Captain wetu, kacheza vizuri sana kunakipindi wapinzani walikuwa wakifika kwake wanaamua kurudi waliko toka maana kulikuwa hakupitiki kabisa, Hazard mpaka unamuonea huruma alivyo shikwa na Captain wetu.
KANTE : Huyu hana maelezo mengi kila mmoja anamjua.
Pain killer naomba aje amuelezee kwa kina zaidi.
MOUNT : Huyu dogo ule u haraka wake kwenye kupokea mpira kisha kushambulia unaweza hisi mpira ni kazi rahis sana. Kila mmoja anamjua vizuri tu hana maelezo mengi huyu dogo.
WERNER : Naona kaanza kurudi kwenye ubora wake
KAI : Huyu dogo bado naona hajakaa sawa pamoja na kucheza false 9 lakin inapaswa atumie vizuri zile nafasi anapata. Fainali asilete uzembe wa namna ile
Yote kwa yote kwa sasa Chelsea ni timu tishio sana Duniani we bisha tu lakini ukweli ndio huo.