Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Kwa muda mrefu nimekua nikisikiliza wachambuzi wa vipindi vya michezo Tanzania, wengi wao kama sio wote hua hawaikubali Madrid kama inaweza kuchukua kikombe chochote.

Hata zile back to back to back wachumbuzi wengi walikua hawaisemi wala kuipa nafasi Madrid na hata mechi dhidi ya Atalanta na Liverpool wachambuzi wa Tanzania walisema tutaondolewa kwenye michuano.
Ni kwamba hawaujui ubora wa Madrid au mahaba yanawapa Upofu?
Mashabiki wa EPL hao.. Ni kuwapotezea tu.. Madrid inawapa maumivu sana, hawawezi isifu wala kuipa nafasi kitu ambacho ni kizuri pia, maana inawaongezea maumivu juu ya maumivu
 
Ukiwapa jina la wachambuzi utakuwa unawapa cheo kikubwa sana, ni wasimuliaji wa matukio yaliyotokea uwanjani, ila hawapo technical na hawapo well informed, sana sana wanachoweza ni kuzungumzia team za Uingereza kwanza kishabiki. Kwahiyo usitegemee kupata technical analysis kutoka kwao haswa kwenye team za nje ya England.
Unamsikiliza mtu anaongea unaamua kuzima radio kwa kuwa unaona unajua kuliko yeye., ninataka waendelee hivi hivi ku underate team yetu ili wajifunze kufuatilia mambo.
 
Ramos watamuacha tu, kwa umri wake hana nguvu tena kwenye negotiation table. Ronaldo aliondoka sababu waliona kwa umri wake hastahili tena mshahara mnono sembuse Ramos ambae rahisi kabisa kumreplace. Kroose na Modric hawana longo longo sababu wanajua kwa walipofikia hawana nguvu ya kutaka mambo makubwa tofati na Ramos ambae haishi kwenye uhalisia.
Ramos utaifa ndo unambeba pale. Wanamtengenezea ulegend pale.
 
Ramos utaifa ndo unambeba pale. Wanamtengenezea ulegend pale.
Ramos, kroose na Modric bado wanaanza sababu Madrid inajenga uwanja hivyo inabidi wawakamue hawahawa ila kama mchezaji mwenyewe anajipandisha gharama hawana haja tena ya kubaki nae hata kama ni mhispaniola. Tena Ramos ni rahis zaidi kumuondoa sababu ni beki ambae yupo above average kidogo ( kundi moja na pique) kinamchomtofautisha na wengine ni uwezo wa kufunga kwa kichwa, sasa kwa timu beki kufunga huwa ni bonas tu.
 
Ramos, kroose na Modric bado wanaanza sababu Madrid inajenga uwanja hivyo inabidi wawakamue hawahawa ila kama mchezaji mwenyewe anajipandisha gharama hawana haja tena ya kubaki nae hata kama ni mhispaniola. Tena Ramos ni rahis zaidi kumuondoa sababu ni beki ambae yupo above average kidogo ( kundi moja na pique) kinamchomtofautisha na wengine ni uwezo wa kufunga kwa kichwa, sasa kwa timu beki kufunga huwa ni bonas tu.
Si tuna Alaba tayari..
Kuna wachezaji nadhani mwisho wa msimu watauzwa ku fund manunuzi ya Heeland na Mbape..
Jovic, Isco, Varane, Ramos, Bale, Mariano, Odriozola na Marcelo.. Hawa wanaweza kuondoka. Kama deal la Mbape au Heeland au wote wawili litakaa sawa.
 
Si tuna Alaba tayari..
Kuna wachezaji nadhani mwisho wa msimu watauzwa ku fund manunuzi ya Heeland na Mbape..
Jovic, Isco, Varane, Ramos, Bale, Mariano, Odriozola na Marcelo.. Hawa wanaweza kuondoka. Kama deal la Mbape au Heeland au wote wawili litakaa sawa.
Hatuwezi kuwapata wote hao kwenye dirisha moja kwanza anaweza asije yeyote sababu kuna viungo inabidi wanunuliwe ambao ni muhimu kwa sasa kuliko hao, pia vinicius alinunuliwa ili kuepuka hizo gharama za mastar plus kuna Hazard tayari.
 
Hatuwezi kuwapata wote hao kwenye dirisha moja kwanza anaweza asije yeyote sababu kuna viungo inabidi wanunuliwe ambao ni muhimu kwa sasa kuliko hao, pia vinicius alinunuliwa ili kuepuka hizo gharama za mastar plus kuna Hazard tayari.
Hazard hamna kitu hapo.. Huyo mwenyewe anaweza ondoka.. PSG wenyewe sahizi washaanza kujiandaa na mbadala wa Mbape..

Tukifanikiwa kuwauza hawa mmoja wapo au wote wawili wanaweza chukuliwa.
 
Hazard hamna kitu hapo.. Huyo mwenyewe anaweza ondoka.. PSG wenyewe sahizi washaanza kujiandaa na mbadala wa Mbape..

Tukifanikiwa kuwauza hawa mmoja wapo au wote wawili wanaweza chukuliwa.
Hao wachezaji uliowataja hata wakiuzwa wote bado hawajafika bei ya mchezaji mmoja na hapo bado mshahara. Mapato yamepungua na bado tunajenga uwanja. hao wachezaji sio tu madrid bali wanaweza wasipate timu yoyote msimu huu inayoweza kuwanunua. Kumbuka tukiuza hao wachezaji unaosema lazima wanunuliwe wengine kuziba nafasi, bado Kunahitajika mbadala wa modric na kroose.
Hazard hawezi kuuzwa bila kumpa muda apandishe kiwango ili bei iwe nzuri sokoni. Me sioni madrid ikisajili yeyote kati yao.
 
Hao wachezaji uliowataja hata wakiuzwa wote bado hawajafika bei ya mchezaji mmoja na hapo bado mshahara. Mapato yamepungua na bado tunajenga uwanja. hao wachezaji sio tu madrid bali wanaweza wasipate timu yoyote msimu huu inayoweza kuwanunua. Kumbuka tukiuza hao wachezaji unaosema lazima wanunuliwe wengine kuziba nafasi, bado Kunahitajika mbadala wa modric na kroose.
Hazard hawezi kuuzwa bila kumpa muda apandishe kiwango ili bei iwe nzuri sokoni. Me sioni madrid ikisajili yeyote kati yao.
Tusubiri muda utaongea.
 
Hao wachezaji uliowataja hata wakiuzwa wote bado hawajafika bei ya mchezaji mmoja na hapo bado mshahara. Mapato yamepungua na bado tunajenga uwanja. hao wachezaji sio tu madrid bali wanaweza wasipate timu yoyote msimu huu inayoweza kuwanunua. Kumbuka tukiuza hao wachezaji unaosema lazima wanunuliwe wengine kuziba nafasi, bado Kunahitajika mbadala wa modric na kroose.
Hazard hawezi kuuzwa bila kumpa muda apandishe kiwango ili bei iwe nzuri sokoni. Me sioni madrid ikisajili yeyote kati yao.
Natamani na natumaini Mbappe atue kwetu atatuongezea nguvu sana
 
Upo sahihi sana,hawa wasimuliaji wa matukio akili yao siku zote na wakat wowote wanajua timu za uingereza ndio bora wakat ukwel siyo,cha pili mara zote madrid huwa haipewi nafasi yakushida kwa sababu wanaongozwa na mihemko hawaangalii ubora wa timu ya madrid wanaangalia namna gan timu inayocheza na madrid inavyofunga magoli bila kuangalia namna gan madrid inaweza kuzuia nakufunga,na hiki ndio kilichowapata Juventus,Atletico and Liverpool na pia ndio kitachowatokea ambao tutaingia nao fainal.

Sent from my SM-A715F using JamiiForums mobile app
Mchambuzi pekee ambae hayuko bias sana ni George Ambagile tu. Wengine hamna kitu.
 
Kikosi cha leo kimekaaje. Nimepata habari majeruhi ni wengi kiasi kwamba watu wanamnanga ZIZOU kwamba leo itabidi nae aingie uwanjani acheze kwani ameruhusu youngstars wengi muhimu kuuzwa au kuwekwa kwenye mikopo. Sasa leo sijui itakuwaje.
HALLA MADRID
 
Kikosi cha leo kimekaaje. Nimepata habari majeruhi ni wengi kiasi kwamba watu wanamnanga ZIZOU kwamba leo itabidi nae aingie uwanjani acheze kwani ameruhusu youngstars wengi muhimu kuuzwa au kuwekwa kwenye mikopo. Sasa leo sijui itakuwaje.
HALLA MADRID

Starting line-up: Real Madrid

Courtois; Odriozola, Militao, Victor, Marcelo; Modric, Rodrygo, Isco, Asensio, Vinícus; Mariano
 
Hii game leo tukipona bahati.. Defensive errors zimekua nyingi sana
Mpaka sasa Courtois ndio ametuweka mchezoni laa sivyo tungekuwa tumeshaoga sio chini ya goli 3.
Ila makosa ya kwenye beki yetu ni lazima yawepo, hapo kati yupo Militao na huyo dogo wa Castilla, beki za pembeni yupo Marcelo na Ordiozola ambao tunajua sio wakabaji, kiungo yupo Modric na Isco, Modric ndio anacheza role ya Casemiro akitegemea msaada WA Isco kwenye kumcover ila mwenzie ana kazi ya kudhurura uwanjani zaidi hiyo kazi anaifanya DOGO Rodrygo, ndio ninaona anajitahidi kwenda kuzuia na kushambulia, kule mbele amesimama Mariano, nguvu nyingi akili kisoda, muda wote anadondoka, hapa ni Vinincius na mwenzie Rodrygo wa step up labda ndio tutapata goli
 
Tumepoteza point kwenye sehemu muhimu sana ya Ligi ila ni Sawa tu kwa kweli kutokana na hali ya team tuliyonayo, ni bahati tu hatujafungwa, ni Getafe tu wajilaumu kwa kweli, acha tuangalie mbele sasa dhidi ya Cadiz, baadhi ya vijana watakuwa wamerudi.
 
Back
Top Bottom