RAIS wa Real Madrid, Florentino Perez ameonekana kushikilia mpango wa kumsajili supastaa wa Chelsea, Eden Hazard hivyo ameamua kumchunia kocha, Antonio Conte.
Kulikuwa na hofu kama Real Madrid wataamua kumchukua kocha, Conte kwennda kurithi mikoba ya Julen Lopetegui, basi jambo hilo linaweza kutibua kwenye mipango yao ya kumchukua Hazard.
Hazard na Conte wameripotiwa kuingia kwenye uhusiano mbaya mwishoni mwa msimu uliopita ambapo staa huyo alicheza chini ya kiwango na hivi karibuni alionenkana kusifu mipango ya kocha mpya huko Chelsea, Maurizio Sarri na kuponda ya mtangulizi wake. Kutokana na hilo, Florentino ameamua kumfungia milango Conte ili kuweka hai mipango ya kumchukua Hazard.
Mpango wa Real Madrid ni kumchukua Hazard kwenye dirisha la Januari na hilo lipo wazi, hivyo Conte acha aende kwingineko,” ilibainisha taarifa juu ya suala hilo.
Kwa sasa, Los Blancos ipo chini ya kocha Santiago Solari, akiwa kocha wa mpito baada ya Lopetegui kufunguliwa mlango wa kutokea kufuatia kipigo cha mabao 5-1 kutoka kwa Barcelona.