Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Madrid to Moscow


DoWVZWBWsAYXsAF.jpg


DoWVZWIXkAEsMWD.jpg
 
Bado mtazamo wangu naamini ni sahihi...tunahitaji mtu wa kiwango cha juu kusimama mbele katka mtazamo wakibiashara lakini pia morali na nidhamu pale mbele irudi...huwez mtegemea bale ambaye iko gonjwa muda wote...benzema anayehitaji nafasi 12 za wazi ili afunge goli moja...hawa watoto bado hawajakomaa kimaamuzi...bado hawajajua uchungu haswa wakupoteza nafasi...tunahitaji mtu ambaye thamani yake inamsuta kila akigusa mpira
Ni sahihi kabisa, ila inaonekana management ya club hawataki kununua tena mchezaji kwa gharama kubwa plus kuna vijana wadogo wamenunuliwa na wanatakiwa waingie moja kwa moja kwenye team, mfano ni huyu Vinicius Jr na mwenzie RodrigoGoes wote hawa ni foward,sasa club ikinunua itabid hawa vijana watolewe kwa mkopo kitu ambacho ninaona hawapo tayari kufanya, club ingeweza hata kumnunua Icardi, ila gharama plus project ya hao vijana ninaona wakaamua kuachana naye.
Ni umakini tu vijana wetu wanakosa ila tutakuwa sawa kadri muda unavyosonga, haswa kama coach atamwamini Mariano. Kesi ya Benzema imekuwa yakudumu sasa
 
Madrid hatuwezi kudumu na striker 9 "kamili" wa kufunga magoli tu, kila striker akija wa kukaa mbele peke yake tutaishia kumtukana.

Kwasababu mfumo wa Real Madrid tunacheza kiteam zaidi siku hizi, tofauti na enzi za kina Raul Blanco, sasa hivi kuanzia midfield mpaka mabeki ni wafungaji sio striker peke yake. Halafu namba 9 wa madrid anatakiwa awaweke bussy mabeki wa timu pinzani ili wasitoke nyuma, kutengeneza nafasi ili ma winger wafunge na kuruhusu midfiled wetu waweze kuzunguka na kushambulia muda wote. Ndio maana moratta hakuweza kukaa, japo alikua anafunga ila hakuweza kuwachezesha kina Ronaldo na Bale na viungo, alikua anawaza kukaa mbele na ndio maana alikua rahisi kufichwa kwenye match.

Natamani hao vijana wetu wadogo wawe wasumbufu sana kama big benz, huyu jamaa ndio alikua anamchezesha Ronaldo, na Ronaldo alikua anampenda sana kucheza nae. Pia vijana wawe wanarudi mpaka nyuma kukaba na kupandisha timu mbele, ila wakitaka wacheze kwa kufunga tu magoli na kukaa mbele hawata dumu, au mfumo ubadilishwe kabisa wa timu.
 
REAL MADRID STARTING XI:

• Navas; Carvajal, Varane, Nacho, Reguilon; Ceballos, Casemiro, Kroos; Vazquez, Benzema, & Asensio.
 
WHAT A START BY CSKA MOSCOW!

THEY HAVE SCORED WITH IN A MINUTE!
 
CLOSE! Casemiro drove a low, powerful shot from long range but it crashed off the post. VAMOS REAL!
 
Hili bus si la kawaida, yaani lile la Diego Simeone cha mtoto.
 
Siku hizi ndio hivi, tunafungwa magoli ya kibwege sana, kisha wanarudi nyuma wanapaki bus tunahaha mpaka tunachanganyikiwa
 
Dani Carvajal is replaced by Odriozola due to an injury.
 
Back
Top Bottom