Roger Sterling
JF-Expert Member
- May 10, 2015
- 13,010
- 23,653
Bundi anatafuta tawi atue. Katika team ambazo hazitakiwi kabisa kulalamikia waamuzi ni Madrid
Madrid mnatakiwa mjue last season kilichokuwa kinawaokoa ni come backs, tena nyingine mlipata kwa msaada wa refer na wachezaji wenu work rate yao ilikuwa kubwa.
Mfano. Goals za dk za mwisho za Ramos peke yake ziliipa Madrid points 11 laliga
Lakini msimu huu, kutokana na sababu ambazo mnazijua ninyi, come backs zimeshindikana kabisa, at least for now
Mnakumbuka mechi za champions league dhidi ya Bayern, Madrid mlianza kufurukuta baada ya kiungo wa Bayern kutolewa kimakosa
Red kadi ya Marcelo ya kwenye league msimu huu ni ujinga wake mwenyewe. Huwezi ukampiga mateke mchezaji mwenzako halafu ukabaki uwanjani. Marcelo ana ushamba fulani hivi utadhani hachezi Madrid, mara nyingi ana tabia ya kupiga mateke wachezaji wenzake na kuprotest innocence, kama mnakumbuka classico ya mwisho ya league alimtoa Messi meno kwa kumpiga elbow ya makusudi kabisa, bahati kwake referee hakuona
Ramos ni sikio la kufa, tabia yake mbaya uwanjani inafahamika vyema miongoni mwa mashabiki wa Madrid
Kuhusu kutopewa spot kicks, huo ni uongo wa mchana kweupe. Hakuna penart ya halali ambayo wamenyimwa, labda tuamue kuweka ushabiki.
Kwanza nakubali kuwa Madrid haitakiwi kulia kuhusu waamuzi, matokeo ya mechi zetu tunayaamua wenyewe, ndio maana ya kuwa club kubwa na bora ya muda wote. Na hakuna mtu kutoka Real Madrid aliyelalamika, hizo ni ripoti tu za waandishi.
Mengine mengi ni hisia zako, na uzoefu unanikumbusha kuwa kwenye mambo yanayoihusu Madrid, ni bora kujadiliana na jiwe kuliko shabiki wa barcelona.