Habarini madridstas wenzangu...naamini wote wazima humu ndani, hii mechi ya Leo Na Betis imenisikitisha sana vijana wetu hawakuwa makini kabisa na Kwa mantiki ya wazi kabisa Kwa Gap la point 7 mapema kabisa katika LaLiga Table in a TWO TEAMS RACE(with Barca) Tayari Tumepoteza 80% za kutwaa ubingwa(ingekuwa ni EPL sawa na sio kwa spain) tena mapema sana mwa msimu huu mpya...Kwa sababu ili tuwe nao sawa tu kwenye msimamo na sio kuwazidi inabidi wapoteze games 2 na kutoa draw game 1 au wapoteze game 1 na kutoa suluhu 4 na kama ni suluhu tupu watoe draws 7, na hii kimantiki si kitu kizuri kwenye harakati za kuwania ubingwa maana tutakuwa watumwa katika kila matokeo ya ushindi Wa wenzetu tukiomba wapoteze kila wanapocheza...Kwa maana nyengine WE LOST ABOUT 80% FOR CHANCES OF CLAIMING LALIGA-TITLE IN 2017/2018...Sijui tutafidia vipi hili Gap infact kiubinadamu hatuwezi kushinda mechi karibia zote zilizo mbele yetu maana lazima ata suluhu zitahusika tu...'am feeling really bad for this!!!
At least kuna shabiki wa Madrid anaongea kitu kinacholeta maana.
Juzi kabla ya kwenda anoeta nilimwambia mwenzenu
PAGAN kuwa kupoteza point kizembe laliga hata mwanzoni mwa msimu itakugharimu msimu mzima akabisha. Kilichotokea jana ni mambo mawili
1. Madrid waliingia wakiwa na pressure kubwa ya kuhitaji ushindi ili kupunguza gap la point na kurudisha imani kwa mashabiki baada ya sare mbili mfululizo nyumbani. Hii iliwafanya wapaniki hata nafasi alizoweza kutengeneza walishindwa kuzitumia kwa kukosa utulivu-kuna diagonal balls kama mbili za ukweli zilipigwa beki wenu wa kulia zote alishindwa kuzi-control na zote kwa siku nyingine ni magoli ya wazi
2. Ronaldo. Hakuna chembe ya shaka kuwa ni mchezaji wa pili kwa ubora baada ya Messi lakini anaigharimu team, kwa uchezaji wake wa sasa wa kusubiri cross, kufanya ujanjaujanja ili apate penart haisaidii team. Ndio maana wale mabeki walikuwa wanaacha isco na modric wanacheza watakavyo maana mwisho wa siku wanajua mpira utaenda either kwa Marcelo au upande wa kulia itapigwa cross wanazuia .
Kwa team inayocheza kitimu, ambayo hakuna nafasi ya shambulizi la kushitukiza, Ronaldo anakuwa mzigo tu hasa kwa umri wake kwa sasa
Pia Ronaldo aliingia akiwa na pressure ya kuonesha kuwa amerudi na anatakiwa yeye aonekane ameibeba Madrid baada ya yeye kutokuwepo na team ikawa imepoteza point nne (4).
Zidane alitakiwa aanzishe kikose kilichoenda anoeta,inawapa confidence wachezaji, alikuja kumwingiza assensio ikiwa ni too late, isco keshachoka, Marcelo hoi, modric hatamaniki.
In short, it was a chaos, kwa mara ya kwanza Madrid walitaka kucheza 12 uwanjani wakashitukiwa na refa ikabidi wamtoe modric