nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
na Jovither Kaijage, Ukerewe
MKUU wa Mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro, ameshangazwa na kushitushwa na jiwe la ajabu lililopo katika Kijiji cha Nyamanga katika Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe, linaloimbiwa na kucheza na kuahidi kulitangaza ili liweze kuchangia pato la taifa.
Ahadi hiyo aliitoa juzi baada ya kutembelea jiwe hilo vikiwemo vivutio kadhaa vya utalii vilivyopo katika Wilaya ya Ukerewe ambapo pia aliziagiza halmashauri za wilaya mkoani humo kutambua na kutunza vivutio hivyo kwa faida ya vizazi vijavyo.
Akiwa eneo la jiwe hilo lililo kando ya Ziwa Victoria, Kandoro alishuhudia jiwe hilo linalokadiriwa kuwa na uzito wa tani 2,000 likiimbiwa na kucheza, kitendo ambacho kilishangaza wengi waliofika kushuhudia maajabu hayo. Mmoja wa wana ukoo wa Rwakatimba wanaotunza mila na desturi ya jiwe hilo, mzee Magesa Makolokolo (90), mbali ya kueleza historia yake pia ndiye mwenye jukumu la kuimbia jiwe hilo licheze. Katika taarifa yake pia aliomba serikali imsaidie gharama za uendeshaji na kutunza mila hiyo, kwa kuwa kila mwaka linafanyiwa tambiko linaloghalimu sh 300,000 na wakati mwingine hushindwa kutimiza sharti hilo kwa kukosa fedha.
MKUU wa Mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro, ameshangazwa na kushitushwa na jiwe la ajabu lililopo katika Kijiji cha Nyamanga katika Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe, linaloimbiwa na kucheza na kuahidi kulitangaza ili liweze kuchangia pato la taifa.
Ahadi hiyo aliitoa juzi baada ya kutembelea jiwe hilo vikiwemo vivutio kadhaa vya utalii vilivyopo katika Wilaya ya Ukerewe ambapo pia aliziagiza halmashauri za wilaya mkoani humo kutambua na kutunza vivutio hivyo kwa faida ya vizazi vijavyo.
Akiwa eneo la jiwe hilo lililo kando ya Ziwa Victoria, Kandoro alishuhudia jiwe hilo linalokadiriwa kuwa na uzito wa tani 2,000 likiimbiwa na kucheza, kitendo ambacho kilishangaza wengi waliofika kushuhudia maajabu hayo. Mmoja wa wana ukoo wa Rwakatimba wanaotunza mila na desturi ya jiwe hilo, mzee Magesa Makolokolo (90), mbali ya kueleza historia yake pia ndiye mwenye jukumu la kuimbia jiwe hilo licheze. Katika taarifa yake pia aliomba serikali imsaidie gharama za uendeshaji na kutunza mila hiyo, kwa kuwa kila mwaka linafanyiwa tambiko linaloghalimu sh 300,000 na wakati mwingine hushindwa kutimiza sharti hilo kwa kukosa fedha.