GE2025 RC Kihongosi aongoza Wananchi wa Arusha kumdhamini mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia

GE2025 RC Kihongosi aongoza Wananchi wa Arusha kumdhamini mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Kenani Laban Kihongosi leo Jumanne Agosti 12, 2025 amewaongoza wananchi na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Arusha kujitokeza kwenye Ofisi za Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Arusha, kumdhamini Mgombea Urais wa Chama hicho Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Rais wa awamu ya sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wananchi walioambatana na Kihongosi ni kutoka makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo wajasiriamali, mama lishe na baba lishe, Vijana wanajishughulisha na usafiri wa bajaji na pikipiki maarufu kama Bodaboda pamoja na wananchi wengine, wakitangaza rasmi kumuunga Mkono Dkt. Samia kutokana na mafanikio makubwa yaliyoshuhudiwa Mkoani Arusha kwa kipindi cha Miaka minne ya Uongozi wake.

Zoezi la kupata wadhamini wa Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Samia Suluhu Hassan linafuatia mara baada ya kuchukua fomu ya kuwania Urais kwenye Tume huru ya Taifa ya uchaguzi INEC Agosti 09, 2025, Tayari kwa kutetea nafasi yake katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 akiambatana na Mgombea mwenza Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi.
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Kenani Laban Kihongosi leo Jumanne Agosti 12, 2025 amewaongoza wananchi na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Arusha kujitokeza kwenye Ofisi za Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Arusha, kumdhamini Mgombea Urais wa Chama hicho Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Rais wa awamu ya sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wananchi walioambatana na Kihongosi ni kutoka makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo wajasiriamali, mama lishe na baba lishe, Vijana wanajishughulisha na usafiri wa bajaji na pikipiki maarufu kama Bodaboda pamoja na wananchi wengine, wakitangaza rasmi kumuunga Mkono Dkt. Samia kutokana na mafanikio makubwa yaliyoshuhudiwa Mkoani Arusha kwa kipindi cha Miaka minne ya Uongozi wake.

Zoezi la kupata wadhamini wa Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Samia Suluhu Hassan linafuatia mara baada ya kuchukua fomu ya kuwania Urais kwenye Tume huru ya Taifa ya uchaguzi INEC Agosti 09, 2025, Tayari kwa kutetea nafasi yake katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 akiambatana na Mgombea mwenza Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi.
Screenshot_20250703-140259~2.png
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Kenani Laban Kihongosi leo Jumanne Agosti 12, 2025 amewaongoza wananchi na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Arusha kujitokeza kwenye Ofisi za Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Arusha, kumdhamini Mgombea Urais wa Chama hicho Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Rais wa awamu ya sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wananchi walioambatana na Kihongosi ni kutoka makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo wajasiriamali, mama lishe na baba lishe, Vijana wanajishughulisha na usafiri wa bajaji na pikipiki maarufu kama Bodaboda pamoja na wananchi wengine, wakitangaza rasmi kumuunga Mkono Dkt. Samia kutokana na mafanikio makubwa yaliyoshuhudiwa Mkoani Arusha kwa kipindi cha Miaka minne ya Uongozi wake.

Zoezi la kupata wadhamini wa Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Samia Suluhu Hassan linafuatia mara baada ya kuchukua fomu ya kuwania Urais kwenye Tume huru ya Taifa ya uchaguzi INEC Agosti 09, 2025, Tayari kwa kutetea nafasi yake katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 akiambatana na Mgombea mwenza Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi.
Wamepewa elfu 10 kila mmoja, yaani wananuliwa wahuni nchi hii
 
Back
Top Bottom