RC Kafulila: Rais Samia ni shujaa mpya wa Afrika anayechomoza kwa kasi ya ajabu

Jabali la Siasa

JF-Expert Member
Jul 10, 2020
2,542
2,172


Akiwa katika maadhimisho ya Siku ya Mashujaa, Rc Kafulila ameifananisha kasi ya maendeleo inayopigwa na Rais Samia inafanana kabisa na ile ya mashujaa wetu,

" Kumbukumbu ya Mashujaa inatukumbusha historia yetu,

inatukumbusha historia ya wazee wetu na mchango wao wa damu kumkabili mkoloni Tanzania na Afrika;

Kuhakikisha Tanzania huru dhidi ya kila aina ya uvamizi ikiwemo uvamizi wa Idd Amin!

Wazee wetu walifanya Taifa letu kuwa Kitovu cha ukombozi wa Bara la Afrika , tulikua Taifa Kiongozi wa Agenda ya Afrika zama hizo.

Hivyo kumbukumbu hizi sio tu zinatukumbusha historia bali kumbukumbu hizi zinatukumbusha WAJIBU wetu na hasa kizazi cha milenia kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa Taifa Kiongozi katika Agenda ya Afrika kila zama.

Ndio sababu tunampongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa mkakati mkubwa wa kujenga diplomasia yetu na kurejesha Tanzania katika jukwaa la Kimataifa.

Rais wetu anafanya kitu kikubwa sana chenye tafsiri ya kukumbuka mashujaa wetu kwani lengo Lao ndio lengo bado; Kujenga Tanzania kubwa yenye nafasi muhimu kimataifa, kujenga Taifa kiongozi kwa bara la Afrika"- David Kafulila, wilayani Bariadi katika kumbukumbu za mashujaa!.
 
Duuh.

Unajua ukisifia sana mpaka anayesifiwa anashtuka anaanza kujiuliza huyu mtu anataka nini??

Mtu ukipewa mamlaka fanya kazi.

Kazi yako itaonekana tu, hakuna haja ya kupiga kelele sana.
 
Duuh.

Unajua ukisifia sana mpaka anayesifiwa anashtuka anaanza kujiuliza huyu mtu anataka nini??

Mtu ukipewa mamlaka fanya kazi.

Kazi yako itaonekana tu, hakuna haja ya kupiga kelele sana.
Mkuu dunia tuliyonayo sio ya kukaa kimya, alichokifanya Kafulila ndio kinapashwa kuigwa na Viongozi wote wa Serikali ili kuipa nafuu CCM 2025
 
View attachment 2306439

Akiwa katika maadhimisho ya Siku ya Mashujaa, Rc Kafulila ameifananisha kasi ya maendeleo inayopigwa na Rais Samia inafanana kabisa na ile ya mashujaa wetu,

" Kumbukumbu ya Mashujaa inatukumbusha historia yetu,

inatukumbusha historia ya wazee wetu na mchango wao wa damu kumkabili mkoloni Tanzania na Afrika;

Kuhakikisha Tanzania huru dhidi ya kila aina ya uvamizi ikiwemo uvamizi wa Idd Amin!

Wazee wetu walifanya Taifa letu kuwa Kitovu cha ukombozi wa Bara la Afrika , tulikua Taifa Kiongozi wa Agenda ya Afrika zama hizo.

Hivyo kumbukumbu hizi sio tu zinatukumbusha historia bali kumbukumbu hizi zinatukumbusha WAJIBU wetu na hasa kizazi cha milenia kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa Taifa Kiongozi katika Agenda ya Afrika kila zama.

Ndio sababu tunampongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa mkakati mkubwa wa kujenga diplomasia yetu na kurejesha Tanzania katika jukwaa la Kimataifa.

Rais wetu anafanya kitu kikubwa sana chenye tafsiri ya kukumbuka mashujaa wetu kwani lengo Lao ndio lengo bado; Kujenga Tanzania kubwa yenye nafasi muhimu kimataifa, kujenga Taifa kiongozi kwa bara la Afrika"- David Kafulila, wilayani Bariadi katika kumbukumbu za mashujaa!.
Mama nakuja juu Sana, Tumwombee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom