Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Amesema kuwa changamoto hiyo siyo matokeo ya ukosefu wa fedha, bali inasababishwa na kukosa mipango ya muda mrefu.
“Nataka niwathibitishie kuwa wanafunzi kukaa chini siyo ukosefu wa fedha, bali ni ukosefu wa mipango,” amesema RC Chalamila.
Hayo ameyaeleza Februari 12, 2026, alipokuwa katika ziara yake Wilaya ya Kinondoni, ambapo alikagua miundombinu katika Shule ya Sekondari Tarimba Abbas ambayo inajengwa.
Ikumbukwe kwamba baadhi ya wadau wamekuwa wakiripoti changamoto ya wanafunzi kukaa chini kutokana na uhaba wa viti kwenye baadhi ya Shule Dar es salaam. Katika baadhi ya shule, iliripotiwa kuwa wanafunzi wanalazimika kwenda na mifuko kwa ajili ya kukalia kama mbadala wa madawati.