Noti mpya tz
JF-Expert Member
- Mar 23, 2011
- 974
- 244
Naomba niwashirikishe jf habari hii ya mkuu wa mkoa wa arusha ambayo imeandikwa na Mwananchi leo.
Friday, 11 November 2011 21:26 0digg
Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mboye
Peter Saramba, Arusha
MKUU wa mkoa wa Arusha, Magessa Mulongo jana alitumia kikao chake na viongozi, watendaji na wawakilishi wa makundi mbalimbali katika Manispaa ya Arusha kujibu mapigo ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe huku akiahidi kupambana nao iwapo wataendelea kuvuruga amani na usalama mkoani mwake.
Mulongo alikejeli falsafa ya nguvu ya umma na maandamano inayotumiwa na Chadema kiasi cha kuchafua hali ya hewa ya kikao hicho baada ya madiwani na viongozi wa Serikali za Mitaa waliopata nyadhifa zao kupitia udhamini wa chama hicho cha upinzani kususia na kutoka nje.Viongozi hao walisema wasingeweza kuendelea kumsikiliza mkuu huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani hapa.Mulongo aliitisha kikao hicho kwenye Ukumbi wa Bwalo la Polisi ili kujadili na kupeana mikakati ya maendeleo kwa viongozi na watendaji wa Manispaa ya Arusha.
Kuna mtu (Mbowe), juzi alikuja hapa na kuhoji hivi Mkuu wa Mkoa (Arusha) ni nani hadi atishe watu? Sasa leo nimewaiteni hapa kuwaambia mkuu wa mkoa ndiye mimi. Sikupendezwa sana na maneno hayo, lakini sitaki kuingilia mambo hayo kwani wazee wetu walitufundisha kuwa ukioga ziwani, akaja kichaa akachukua nguo zako nawe ukichomoka kumfukuza, utaonekana kichaa ni wewe, alisema Mulongo.
Alihoji pia uwezo na ujasiri wa Mwenyekiti huyo wa Chadema kutoa masharti kwa Serikali kuhusu mkutano wao wa hadhara uliofanyika Jumatatu iliyopita.
Mbowe alikuwa ameonya kuwa angeendesha maandamano
ya siku saba mfululizo na kuvuruga ziara ya Mtoto wa Malkia wa Uingereza, Prince Charles aliyetembelea Arusha karibuni.
Hivi anatoa wapi uwezo na ujasiri wa kuitisha Serikali na kuipa masharti? Narudia tena leo, tena mbele ya hadhara tofauti na juzi nilipozungumza na waandishi wa habari pekee kwamba, nikiwa mhimili wa ulinzi, amani na usalama mkoa, sitakubali kushuhudia mtu anavuruga amani tena Arusha. Kibaya zaidi wengi wao wanatoka nje ya mkoa wetu. Imetosha ! Tumechoka.
Mkuu huyo wa mkoa alikejeli maandamano ya mara kwa mara ya Chadema: Haya mambo ya maandamano sawa kwa sababu wanaruhusiwa kisheria. Lakini yakishazoeleka na kukolea, wanaweza kujikuta wanaandamana hata
baada ya kuingia madarakani. Si wameshazoea kuandamana?
Alisema mgogoro wa Arusha hauwezi kutatuliwa kwa matumizi ya nguvu ya dola lakini akahoji nia halisi na uthabiti wa Chadema katika suala hilo wakati walikataa kusikiliza hata ushauri wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Alisema Pinda alikuwa amewaasa kutofikia hatua ya kuwatimua waliokuwa madiwani wao waliolalamikiwa kwa kuingia muafaka bila ridhaa ya uongozi wa taifa.Hivi tukiamua kurejea uchaguzi wa Meya Arusha ambayo wanadai ndilo chimbuko la matatizo Arusha, watashindaje wakati tayari wamewafukuza madiwani wao watano?
Maneno hayo yalionekana kuwakera madiwani na viongozi wa Serikali za Mitaa kupitia Chadema ambao waliamua kususia na kutoka nje.Wakizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa kikao, viongozi hao wa Chadema walitangaza mgogoro na Mkuu huyo wa mkoa na kuapa kutoshirikiana naye kutokana na kuonyesha dharau kwao, chama na viongozi wao wa kitaifa.
Leo (jana) tumeitwa hapa kwa barua zinazoonyesha RC atazungumzia mikakati na mipango ya maendeleo Arusha. Lakini badala ya kujikita katika misingi hiyo anageuza kikao jukwaa la kuishambulia Chadema na viongozi wake. Kwa mtindo na kasi hii aliyoanza nayo, Arusha itamshinda. Tunamshauri ahame kabla mambo hayajamharibikia, alisema Mwenyekiti wa Mtaa wa Kambi ya Fisi, Hillary Monyi.
Wakati viongozi hao wa Chadema wakitoka nje ya ukumbi, Mulongo alilazimika kunyamaza kidogo na kuendelea: Hata siku Rais anazindua Bunge kule Dodoma hawa wenzetu walitoka nje, lakini waliporudi hawakutueleza. Naamini nao (waliokuwa wakitoka nje) watarudi.
Katika kikao chake na waandishi wa habari muda mfupi kabla ya kujisalimisha polisi Jumatano iliyopita, Mbowe alihoji kitendo cha Mulongo kutumia vyombo vya dola kuwatishia viongozi, wanachama na wafuasia wa Chadema.
Alilalamika akisema hana mkuu huyo wa mkoa mamlaka ya kuwatisha waliochaguliwa kwa kura nyingi za umma wakati yeye (RC) ameteuliwa na mtu mmoja (Rais).
Friday, 11 November 2011 21:26 0digg
Peter Saramba, Arusha
MKUU wa mkoa wa Arusha, Magessa Mulongo jana alitumia kikao chake na viongozi, watendaji na wawakilishi wa makundi mbalimbali katika Manispaa ya Arusha kujibu mapigo ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe huku akiahidi kupambana nao iwapo wataendelea kuvuruga amani na usalama mkoani mwake.
Mulongo alikejeli falsafa ya nguvu ya umma na maandamano inayotumiwa na Chadema kiasi cha kuchafua hali ya hewa ya kikao hicho baada ya madiwani na viongozi wa Serikali za Mitaa waliopata nyadhifa zao kupitia udhamini wa chama hicho cha upinzani kususia na kutoka nje.Viongozi hao walisema wasingeweza kuendelea kumsikiliza mkuu huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani hapa.Mulongo aliitisha kikao hicho kwenye Ukumbi wa Bwalo la Polisi ili kujadili na kupeana mikakati ya maendeleo kwa viongozi na watendaji wa Manispaa ya Arusha.
Kuna mtu (Mbowe), juzi alikuja hapa na kuhoji hivi Mkuu wa Mkoa (Arusha) ni nani hadi atishe watu? Sasa leo nimewaiteni hapa kuwaambia mkuu wa mkoa ndiye mimi. Sikupendezwa sana na maneno hayo, lakini sitaki kuingilia mambo hayo kwani wazee wetu walitufundisha kuwa ukioga ziwani, akaja kichaa akachukua nguo zako nawe ukichomoka kumfukuza, utaonekana kichaa ni wewe, alisema Mulongo.
Alihoji pia uwezo na ujasiri wa Mwenyekiti huyo wa Chadema kutoa masharti kwa Serikali kuhusu mkutano wao wa hadhara uliofanyika Jumatatu iliyopita.
Mbowe alikuwa ameonya kuwa angeendesha maandamano
ya siku saba mfululizo na kuvuruga ziara ya Mtoto wa Malkia wa Uingereza, Prince Charles aliyetembelea Arusha karibuni.
Hivi anatoa wapi uwezo na ujasiri wa kuitisha Serikali na kuipa masharti? Narudia tena leo, tena mbele ya hadhara tofauti na juzi nilipozungumza na waandishi wa habari pekee kwamba, nikiwa mhimili wa ulinzi, amani na usalama mkoa, sitakubali kushuhudia mtu anavuruga amani tena Arusha. Kibaya zaidi wengi wao wanatoka nje ya mkoa wetu. Imetosha ! Tumechoka.
Mkuu huyo wa mkoa alikejeli maandamano ya mara kwa mara ya Chadema: Haya mambo ya maandamano sawa kwa sababu wanaruhusiwa kisheria. Lakini yakishazoeleka na kukolea, wanaweza kujikuta wanaandamana hata
baada ya kuingia madarakani. Si wameshazoea kuandamana?
Alisema mgogoro wa Arusha hauwezi kutatuliwa kwa matumizi ya nguvu ya dola lakini akahoji nia halisi na uthabiti wa Chadema katika suala hilo wakati walikataa kusikiliza hata ushauri wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Alisema Pinda alikuwa amewaasa kutofikia hatua ya kuwatimua waliokuwa madiwani wao waliolalamikiwa kwa kuingia muafaka bila ridhaa ya uongozi wa taifa.Hivi tukiamua kurejea uchaguzi wa Meya Arusha ambayo wanadai ndilo chimbuko la matatizo Arusha, watashindaje wakati tayari wamewafukuza madiwani wao watano?
Maneno hayo yalionekana kuwakera madiwani na viongozi wa Serikali za Mitaa kupitia Chadema ambao waliamua kususia na kutoka nje.Wakizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa kikao, viongozi hao wa Chadema walitangaza mgogoro na Mkuu huyo wa mkoa na kuapa kutoshirikiana naye kutokana na kuonyesha dharau kwao, chama na viongozi wao wa kitaifa.
Leo (jana) tumeitwa hapa kwa barua zinazoonyesha RC atazungumzia mikakati na mipango ya maendeleo Arusha. Lakini badala ya kujikita katika misingi hiyo anageuza kikao jukwaa la kuishambulia Chadema na viongozi wake. Kwa mtindo na kasi hii aliyoanza nayo, Arusha itamshinda. Tunamshauri ahame kabla mambo hayajamharibikia, alisema Mwenyekiti wa Mtaa wa Kambi ya Fisi, Hillary Monyi.
Wakati viongozi hao wa Chadema wakitoka nje ya ukumbi, Mulongo alilazimika kunyamaza kidogo na kuendelea: Hata siku Rais anazindua Bunge kule Dodoma hawa wenzetu walitoka nje, lakini waliporudi hawakutueleza. Naamini nao (waliokuwa wakitoka nje) watarudi.
Katika kikao chake na waandishi wa habari muda mfupi kabla ya kujisalimisha polisi Jumatano iliyopita, Mbowe alihoji kitendo cha Mulongo kutumia vyombo vya dola kuwatishia viongozi, wanachama na wafuasia wa Chadema.
Alilalamika akisema hana mkuu huyo wa mkoa mamlaka ya kuwatisha waliochaguliwa kwa kura nyingi za umma wakati yeye (RC) ameteuliwa na mtu mmoja (Rais).