Rasmi sasa: Container zote za import kubaki bandarini

Rasmi sasa: Container zote za import kubaki bandarini

Mkuu kuwa mkweli,

kwenye mkataba wa TPA na ICD kuna kipengele ki nasema kuwa, mizigo itapelekwa IDC ikiwa tu eneo la kuhifadhia mizigo hiyo au Containers ndani ya Bandari litakuwa limejaa.

Sasa ICD nyingi zikawa zina mtandao wao hapo bandarini ambapo mizigo ikifika tu hata kama ndani ya Bandari bado kuna nafasi ya kuhifadhi mizigo ilikuwa inapelekwa ICD hivyo kuikosesha TPA mapato yake na wakati mwingine ICD zilikuwa zinawacheleweshea wateja wao mizigo yao kwa makusudi ili waweze kupata mapato.

kwa hatua hii, naishukuru sana serikali kwa hatua hii.
Mkuu tunashukuru kwa ufafanuzi ambao wapiga dili hawapendi watu wengine tujue. Wenyewe juzi walituambia meli zimekimbia bandari ya Dar kwa kodi wanazotozwa mawakala a.k.a. madalali wa kitanzania. Kwa maana nyingine walizifukuza meli wenyewe kwa kupiga debe bovu huko anga za Kimataifa wakifikiri wanaikomoa Serikali bila kujua kwamba wao ndio watakuwa waathirika wa kwanza. Na wakati huo huo bado wanataka mafuriko ya makontena kwenye ICD wanazopigia dili. Jamani you can't eat the cake and have it.
 
Sad! Yaani hiyo ni njia rahisi ya kukabili wizi wa makontena? Zile meli zilizotoroka bila kulipa kodi za TPA nazo zilitia nanga kwenye ICD?

Nadhani uamuzi huo una madhara makubwa kiuchumi, kijamii,na kisiasa. Serikali kama iliweza kugundua meli ambazo hazikulipa kodi ya kuegesha bandarini kwa nini inashindwa kukabili magendo ya ICD? Ni vema serikali ibadikishe sheria ili TPA na ICD wabanwe zaidi na kuwajibika iwapo itagundulika kuwa ICD imeruhusu makontena kupotea.

Vv
 
Hatua mwafaka za wapi zaidi ya kurejea tena kwenye hizo hizo ICDs mnazotaka kuaminisha watu kwamba serikali imetoa hiyo order kwavile wanatorosha makontena badala tu ya kuwa wazi kwamba mzigo umpungua na nafasi bandarini ipo!! Hata hivyo, hiyo nayo ni ku-abuse private sector. Solution sio kusimamisha matumizi ya ICDs bali kutoa good services kwa depots zilizopo bandarini ili kuwashawishi importers kutumia hizo depots badala ya kupeleka mzigo ICDs!!

Hatimaye baada ya wadau kutishia kusitisha kuleta meli Tanzania, Serikali kupitia TPA imeruhusu ICD,s kuendelea kutumika hadi hapo itakapoamua vinginevyo, wale waliosema ICD kuna wizi/rushwa waje sasa kutuambia serikali imepeleka ulinzi lini ?
 
Hatimaye baada ya wadau kutishia kusitisha kuleta meli Tanzania, Serikali kupitia TPA imeruhusu ICD,s kuendelea kutumika hadi hapo itakapoamua vinginevyo, wale waliosema ICD kuna wizi/rushwa waje sasa kutuambia serikali imepeleka ulinzi lini ?
Are you SERIOUS?!
 
Kwenye kila uamuzi kuna faida na hasara zake. Wingi wa ICD sio kila mara ni neema kwa kila mhusika kwenye import na export trade. Serikali imechezewa sana kupitia hizo hizo ICDs. Kifo cha NASACO kilikuja na neema kwa wachache waliokuwa na vyeo vya juu lakini national interests ziliumizwa sana.
 
Mzigo ukiongezeka,hatua mwafaka zitachuliwa kwa wakati mwafaka.

Naona mzigo umeongezeka OVERNIGHT!

TPA.png
 
Usiwe na haraka. ICD itabaki kuendelea kufanya Kazi kama storage ya muda. Lengo hili inania nzuri na niya kuondoa mianya ya rushwa na ukangaja. Ila tu Bandari utendeji uwe 24hrsx7days kwa mamlaka zote. (Full Transactions-TRA,Benk,TFDA etc). Wakifanya hivi wataongeza mapato na ufanisi.
Asikudanganye mtu kwamba itakuwa storage ya muda unless kuwe na serious cargo problem!! Itakuwa storage ya muda wakati huo wanatarajia permanent storage terminal kuwa wapi?! Labda kama serikali inataka ijenge ICDs zake wenyewe vinginevyo, ICDs haziepukiki labda alternatively effficiency ya containers handling iwe improved kwa zaidi ya 500%!!
 
Ukiona watu wanalalamika na kuponda jua, wameguswa kwenye mirija yao. ila kwa wale walozoea vya halali hawalalamiki mbona??? Kisa ajira za watu 50,000 ndo serikali ikose mapato yatakayoweza kusaidia millions of Tanzanian, Mtuache tufanye kazi jamani, HII HABARI YA KUWAANGALIA WACHACHE NA WENGI WANAUMIA MAGUFULI NDO HAITAJI, MTAMZOEA TU, Tuko nyuma yako baba, Tunakuombea.
Kwahiyo naona serikali ikiwa na akili timamu imeamua iendelee kukosa mapato!! Sijui nani kawadanganya kwamba tatizo ni ICDs wakati kila mmoja anajua tatizo ni watendaji wenyewe! Sasa kama unadhani watu tulikuwa tuna-criticise bila grounds; wenyewe tayari wameshagundua walichemka:
TPA.png
 
Tuna wa amini hawa kama walivyo ona icd ulikuwa utaratibu mbovu watakuja na utaratibu mwingine wa manufaa kwa taifa.

Huwezi kuta watu wanalima na wana viwanda vya mihadarati, eti Kiongozi makini uache kuchukua hatua kwa kuwa wajiriwa wa hiyo sekta ya mihadarati ni wengi watakosa ajira. Ndio mnalolitetea hapa. Mtu makini ataisambaratisha hiyo biashara ya mihadarati. Mh Rais yuko makini na kasambaratisha icds za kihunihuni.

Na wahawasha!
Nasikitika serikali yetu tukufu inabariki kuendelea kutumika kwa utaratibu mbovu:
TPA.png
 
MSUKUMA AJUII KUPINDAA KASOMA NYAKATI DILI ZOTE ZIKO BANDARINI NAWAMBIA YALE MAHAMMER MTAPAKI TU TUKUTANE MWENDOKASI

Basi naona amemgelezea Mbowe ku-change gia angani!!

TPA.png
 
Kwa haya yanayoendelea sasa nadhani wakati wa Sumatra kuvunjwa umefika, hao wapo kisiasa zaidi kuliko kuendeleza misingi ya kazi zao
Yaani kuna mambo mengine ukiyaangalia kwa makini tu unajua hayapo sawa hata kama si mdau!
 
Duh, kama ni kweli basi shughuli pevu, inatakiwa pia haya maamuzi yanapofanywa yawe yanaangalia ajira kwanza kwa watu ndo iwe kipau mbele.
 
Kubali tu kwamba walichemka... hili halihitaji shahada ya port logistics kufahamu kwamba walikurupuka!!!!
Hawakuchemka walikua na nia njema tu ndiyo maana wame respond timely baada ya ku sense challenges.
 
Nasikitika serikali yetu tukufu inabariki kuendelea kutumika kwa utaratibu mbovu:
View attachment 417989

Makasha ya kwenda kwenye icds hayatapatikana kama hakutakuwa na ucheleweshaji wa makusudi ili icd zipate makonteana. Icd zimetokana na artificial demand ya storage facility kwa ucheleweshwaji wa mizigo wa makusudi na kimkakati. Na hapo ndipo mh Rais na serikali yake wanapotakiwa wawe makini, otherwise it will be the same old story.

Na washawasha!
 
Back
Top Bottom