Rasmi sasa: Container zote za import kubaki bandarini

Rasmi sasa: Container zote za import kubaki bandarini

Una hakika kua ukisema "majukumu ya kijinga'' ndiyo utakua umeonyesha kiwango chako cha ustaarabu?
Ni saa ngapi nilikuambia naonesha kiwango cha ustaarabu hapa? Nenda kashitaki basi kwamba nimesema "majukumu ya kijinga" manake sheria ya mitandao ipo wazi! Go... hurry up!
 
Pongezi kwa Serikali , Ni uamuzi wenye maslahi ya uuma , hawa jamaa walikuwa wana make super normal profits ambayo sasa itatudi Serikalini Ili ipatikane fedha za Dawa, maji, barabara n.k. Sasa tutarajie makusanyo ya TPA yaongezeke Sio yabaki Kabla ya uwepo wa ICDs ! Bado fupa la Ticks Kama wataweza irudisha kwa TPA itakuwa vizuri sana kwa manufaa ya uuma wa waTZ
Kwani huko ICDs hawakuwepo hao watu wa TRA?
 
Container hulipiwa ushuru pale mwenye mzigo anapokuja kuuchukua mzigo wake. Kwahiyo kama kontena litapelekwa ICD halitalipiwa ushuru likiwa bandarini... Kontela linaweza kupakuliwa melini leo, na kesho likahamishiwa kwenye ICD hata kabla mteja hajaanza kuprocess malipo ya kodi.

Hujui taratibu za ICD, achilia mbali mteja kutoa kasha bila kulipa kodi hata mmiliki wa ICD hawezi kutoa kasha lake bila kulipa kodi.

Tatizo sio ICD tatizo mfumo wa nchi hii sera ni kiongozi. Sera haijaainishwa kikatiba badala yake kila kiongozi anayekuja basi yeye ndiye sera.
 
Wakipoteza ajira sio kwamba hawatapata hadi KUFA KWAO. Wataendelea kuomba tena hata hukohuko bandarini pale nafasi zitakapotoka tena, ajira zinatengenezwa kwa wingi sana kipindi hiki na zitakapotangazwa watu watakuwa hawatoshi hata kuku na bata watatamaniwa wafanye kazi serikalini ila haitawezekana....Time will tell!, wanaotolewa huko kwenye ajira zinazoingizia hasara serikali wawe na moyo wa ujasiri kipindi hiki kigumu.....watapata kazi nzuri kuliko hizo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Taarifa kwa wasiojua, serikali ilishafanya uhakiki wa ICD kuhusiana na malipo ya kodi pamoja na ushuru wa bandari. kwa ujumla matatizo hayakuonekana kwenye ICDs wala Clearing companies bali matatizo makubwa yalionekana yanatokana na watendaji wa serikali wakishirikiana na mabenki kuiibia serikali mapato.

Kila walipozishutumu ICD na Clearing companies kwa tuhuma za ubadhirifu na wizi wa fehda za serikali ICD walipeka vielelezo vyao na clearing firms nazo zilipeleka vielelezo ndio uozo ukaoneka upo kwenye baadhi ya watendaji.
 
Wakipoteza ajira sio kwamba hawatapata hadi KUFA KWAO. Wataendelea kuomba tena hata hukohuko bandarini pale nafasi zitakapotoka tena, ajira zinatengenezwa kwa wingi sana kipindi hiki na zitakapotangazwa watu watakuwa hawatoshi hata kuku na bata watatamaniwa wafanye kazi serikalini ila haitawezekana....Time will tell!, wanaotolewa huko kwenye ajira zinazoingizia hasara serikali wawe na moyo wa ujasiri kipindi hiki kigumu.....watapata kazi nzuri kuliko hizo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Tatizo sio ajira tu, tatizo tunapoteza sana mapato sasa hivi wateja wamehamia bandari za nchi jirani, pia kuna baadhi ya wafanyabiashara wa hapa wameanza kujenda ICD mombasa sasa nchi inapata nini kwa hili?
 
Ni saa ngapi nilikuambia naonesha kiwango cha ustaarabu hapa? Nenda kashitaki basi kwamba nimesema "majukumu ya kijinga" manake sheria ya mitandao ipo wazi! Go... hurry up!
Huna mamlaka ya kuniamrisha wewe endelea na mabezo kwakua wewe ni mjanja sana lkn mda ukifika wakikuzukia na kukutia mbaroni usije ukaanza kutoa utetezi ohoo ulimi uliniteleza,mhemko si jambo zuri litakuingiza kwenye shida.
 
Maadam sina ushahidi kama nilivyouona kwa ICDs nashindwa kusema siamini au laa. Kama upo si kwa kiasi kikubwa kama kule ICDs. Yes Wafanyakazi WEZI... nadhani wale wezi wazuri zaidi walipelekwa kwa makusudi kwenye ICDs ili waibe vizuri.... Kontena ili litoke lazima lifanyiwe clearance na TRA... kwa kifupi wezi wakuu wako TRA... lakini cha kushangaza zaidi utumbuaji haukuwagusa sana hawa watoza ushuru. Na waliotumbuliwa ni makarani wa kawaida tu... Waliowaweka hao makarani hawakuguswa.

Kama ulivyosema, serikali imeshindwa kuwadhibiti wafanyakazi wake wenyewe. Period!
Afadhali tupo pamoja kwa jambo moja kwamba Wafanyakazi ni wezi na serikali imeshindwa kwadhibiti wafanyakazi wake wenyewe!!

Kuhitimisha ni kwamba, there's no way kwa hapa tulipo tunaweza kuzikwepa ICDs, no way! Na endapo utaona mwaka unapita bila kuonekana mahitaji ya ICDs basi unatakiwa kuingiwa hofu kwavile si dalili njema! Si dalili njema kwa sababu, jambo lililo wazi hadi sasa bandari ya Dar es salaam haina nafasi ya kutosha kuweza ku-handle containers. Sasa ukiona wanaweza tafsiri yake ni moja tu... mizigo itakuwa imepungua! Lakini endapo matumizi ya bandari yataongezeka kidogo tu; bandari watakosa pa kuweka mizigo. Hapo tena watalazimika kurudi kwenye ICDs!
 
Afadhali tupo pamoja kwa jambo moja kwamba Wafanyakazi ni wezi na serikali imeshindwa kwadhibiti wafanyakazi wake wenyewe!!

Kuhitimisha ni kwamba, there's no way kwa hapa tulipo tunaweza kuzikwepa ICDs, no way! Na endapo utaona mwaka unapita bila kuonekana mahitaji ya ICDs basi unatakiwa kuingiwa hofu kwavile si dalili njema! Si dalili njema kwa sababu, jambo lililo wazi hadi sasa bandari ya Dar es salaam haina nafasi ya kutosha kuweza ku-handle containers. Sasa ukiona wanaweza tafsiri yake ni moja tu... mizigo itakuwa imepungua! Lakini endapo matumizi ya bandari yataongezeka kidogo tu; bandari watakosa pa kuweka mizigo. Hapo tena watalazimika kurudi kwenye ICDs!
Mzigo ukiongezeka,hatua mwafaka zitachuliwa kwa wakati mwafaka.
 
Afadhali tupo pamoja kwa jambo moja kwamba Wafanyakazi ni wezi na serikali imeshindwa kwadhibiti wafanyakazi wake wenyewe!!

Kuhitimisha ni kwamba, there's no way kwa hapa tulipo tunaweza kuzikwepa ICDs, no way! Na endapo utaona mwaka unapita bila kuonekana mahitaji ya ICDs basi unatakiwa kuingiwa hofu kwavile si dalili njema! Si dalili njema kwa sababu, jambo lililo wazi hadi sasa bandari ya Dar es salaam haina nafasi ya kutosha kuweza ku-handle containers. Sasa ukiona wanaweza tafsiri yake ni moja tu... mizigo itakuwa imepungua! Lakini endapo matumizi ya bandari yataongezeka kidogo tu; bandari watakosa pa kuweka mizigo. Hapo tena watalazimika kurudi kwenye ICDs!
Hilo halina ubishi... ICDs hazikwepeki. Hivi sasa zinaonekana si mali kitu kwa kuwa bandari haina mizigo. Tukilemewa utashangaa haya masharti yanapunguzwa bila shuruti.

Ukweli ulio wazi ni kuwa mizigo imepungua bandarini.
 
Huna mamlaka ya kuniamrisha wewe endelea na mabezo kwakua wewe ni mjanja sana lkn mda ukifika wakikuzukia na kukutia mbaroni usije ukaanza kutoa utetezi ohoo ulimi uliniteleza,mhemko si jambo zuri litakuingiza kwenye shida.
Tafuta wa kuwatisha wewe; sio mimi! Eti wakija kukutia mbaroni... mbona tunaleteana viroja!!!
 
Ukiona watu wanalalamika na kuponda jua, wameguswa kwenye mirija yao. ila kwa wale walozoea vya halali hawalalamiki mbona??? Kisa ajira za watu 50,000 ndo serikali ikose mapato yatakayoweza kusaidia millions of Tanzanian, Mtuache tufanye kazi jamani, HII HABARI YA KUWAANGALIA WACHACHE NA WENGI WANAUMIA MAGUFULI NDO HAITAJI, MTAMZOEA TU, Tuko nyuma yako baba, Tunakuombea.
 
Kwa mara nyingine tunaelekea kuona zaidi ya watu 50,000 wanaenda kupoteza ajira baada ya serikali kupitia SUMATRA kutoa waraka wa kuzuia mizigo yote inayoingia bandarini kubaki hapo tofauti na awali ambapo mteja alikuwa anaweza kuamua container yake akaitolee Icd atakayochagua.

Waraka huo ambao umetolewa tarehe 10, 2016 unaelekeza amri hiyo imeanza kutekelezwa tangu tarehe 7/10/16.

Kwa uamuzi huo wa serikali maana yake sasa zile ICD zote zitabaki bila kazi na kupelekea wafanyakazi karibu wote kupoteza ajira.


Usiwe na haraka. ICD itabaki kuendelea kufanya Kazi kama storage ya muda. Lengo hili inania nzuri na niya kuondoa mianya ya rushwa na ukangaja. Ila tu Bandari utendeji uwe 24hrsx7days kwa mamlaka zote. (Full Transactions-TRA,Benk,TFDA etc). Wakifanya hivi wataongeza mapato na ufanisi.
 
Usiwe na haraka. ICD itabaki kuendelea kufanya Kazi kama storage ya muda. Lengo hili inania nzuri na niya kuondoa mianya ya rushwa na ukangaja. Ila tu Bandari utendeji uwe 24hrsx7days kwa mamlaka zote. (Full Transactions-TRA,Benk,TFDA etc). Wakifanya hivi wataongeza mapato na ufanisi.

Kiongozi umepitia waraka ulioambatanishwa?
 
Mzigo ukiongezeka,hatua mwafaka zitachuliwa kwa wakati mwafaka.
Hatua mwafaka za wapi zaidi ya kurejea tena kwenye hizo hizo ICDs mnazotaka kuaminisha watu kwamba serikali imetoa hiyo order kwavile wanatorosha makontena badala tu ya kuwa wazi kwamba mzigo umpungua na nafasi bandarini ipo!! Hata hivyo, hiyo nayo ni ku-abuse private sector. Solution sio kusimamisha matumizi ya ICDs bali kutoa good services kwa depots zilizopo bandarini ili kuwashawishi importers kutumia hizo depots badala ya kupeleka mzigo ICDs!!
 
Back
Top Bottom