Forbes1990
JF-Expert Member
- Apr 14, 2018
- 513
- 989
Aston villa msimu huu sijui wekuaje moja ya timu zilizosajili Ni Aston Villa ila wanachezea vichapo ...
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app
Daaaa kweli nimekumbukaDi canio alikuwa Westham na sio Aston Villa
hili litimu halitoboi EPL....level zake ni za championship kuleJanuary 20, 2020
Birmingham England
NEW SIGNING MBWANA SAMATTA
Exclusive haya ni mahojiano ya Mbwana Samatta akiongea na chaneli rasmi ya klabu ya Aston Vill FC baada ya kukamilisha mkataba kuchezea klabu hiyo.
Source: Aston Villa FC
Habari kamili :
Mchezaji wa kimataifa wa Tanzania amesaini rasmi mkataba wa miaka minne na nusu na Timu ya Aston Villa ya mjini Birmingham, England.
Mbwana Samatta na klabu yake mpya wameweza kukubaliana mkataba na sasa klabu inafuatilia kukamilisha kupata kibali cha kazi na international transfer clearance certificate vitavyo mruhusu kuchezea klabu hiyo.
Hii inamaana Aston Villa na Genk KRC wameafikiana masuala yote mchezaji huyo nyota wa Tanzania kuhama kwa kitita cha £ 10,000,000. Klabu ya Aston Villa ipo nafasi ya 18 ktk msimamo wa league ya Premier League ikiwa na pointi 24. Mbwana Samatta pamoja na midfielder Jack Grealish ndiyo karata turufu atakayo itegemea kocha Dean Smith wa Aston Villa ili timu hiyo isiteremke daraja.
Mmojawapo wa Shabiki mkubwa wa Aston Villa ni Prince William ambaye ni mjukuu wa Malkia wa Uingereza Elizabeth II. Hii ina maana kuwa kasri ya Malkia Elizabeth II itakuwa inazizima kwa kelele, furaha, gonga-tano-kiganja za mjukuu na kusikia jina la Mbwana Samatta na Tanzania kila atapofunga goli.
Aston Villa chini ya midfielder kapteni Jack Grealish mwenye miaka 24 aliyefunga mabao 7 na Mbwana Samatta kuchukua nafasi ya namba 9 kuwa tumaini kubwa kuwachachafya walinzi wa timu pinzani na kuleta matokeo makubwa ya pointi kibao kwa Aston Villa isiteremke daraja.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 wa zamani wa Genk KRC ya Ubelgiji alifumania nyavu mara 76 akiwa na timu hiyo ya Ubelgiji katika michuano ya ligi ya Ubelgiji, Europa na mwaka jana ktk Uefa Champion league.
Katika UEFA Champion league Mbwana Samatta aliweza kufunga magoli dhidi ya timu kubwa zenye kuta ngumu za ulinzi za Liverpool na Napoli ya Italy na kuanzia hapo nyota ya Mbwana Samatta ilingara na timu kubwa ulaya kuanza kutafuta saini yake.
Uwanja wa nyumbani wa Villa Park umekuwa wa kihistoria maana toka 1897 timu ya Aston Villa haijawahi kutumia uwanja zaidi ya huo. Timu zingine kama Arsenal, Manchester United n.k ama walihamisha viwanja au kuvifanyia ukarabati mkubwa viwanja vyao.
Historia nyingine ya kutukuka ya Aston Villa ni walicheza miaka 24 mfululizo ktk premier league ya Uingerza kuanzia 1992 hadi 2016 walipoteremka daraja. Lakini hawakukaa ktk daraja la chini muda mrefu na kurejea tena ktk premier league mwaka jana 2019.
Video toka maktaba:
Shabiki mkubwa wa Aston Villa, Prince William alipewa heshima ya kuingia ktk pitch ya uwanja wa Villa Park pamoja na mkewe Kate walipata fursa kuongea na wachezaji pia kuona miradi ya klabu hiyo kurudisha fadhila kwa wapenzi na mashabiki kwa kushirikisha watoto wa mji huo.
Source: The Royal Family Channel
Tawile Sangoma Tawile.
Mikataba ya mwaka mmoja au miezi sita iko Tanzania na nchi nyingie zakubahatisha. Samatta kusainishwa miaka minne maana yake akiperform fresh atauzwa kwa dau kubwa sana kuvunja mkataba.Samatta kusaini miaka minne katika club ya Astonvilla binafsi naona Kama Ni very risk kwakua endapo timu itashuka daraja na samatta hakuonesha kiwango kizuri Basi kununuliwa na club nyingine itakua ngumu sababu ya mkataba wa miaka minne.
Samatta anahitaji msimu mmoja pale uingereza ili kuweza kuonesha kiwango chake halisi ambacho hatuna shaka nacho Ila kwa Sasa hatoweza kutokana na Aina ya timu hasa ukizingatia kwa ratiba ilivyo wanakwenda kupambana na Big 4 wale wababe pale juu. Yote kwa yote tunakuombe katika fainali hii bro ufunge hata moja tu..
Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli kabisa na akivulunda inakula kwakeMikataba ya mwaka mmoja au miezi sita iko Tanzania na nchi nyingie zakubahatisha. Samatta kusainishwa miaka minne maana yake akiperform fresh atauzwa kwa dau kubwa sana kuvunja mkataba.