Rasimu ya Katiba inayopendekezwa 2014

Rasimu ya Katiba inayopendekezwa 2014

daaah yaani wakuu wa mikoa na wilaya ndani? hakuna kikomo cha ubunge? hii katiba imeangalia maslah yao wanasiasa! ona hawataki hata kuwajibishwa!
 
Rasimu iliyotolewa leo ni uharo mtupu, wanajisisifia na kutamba kwa mbwembwe na vitu ambavyo wanajuwa kabisa katika rasimu ya Mzee Sinde hayakuwekwa kwa sababu si ya muungano. Sasa sijui wanaona waTz wote ni wapumbavu kama wao, wacha tumalize uchaguzi ili tuandike katiba ya wananchi tuwaache na katiba yao ya ccm wakaitumie kuzimu!!!!!!!
 
Ndugu Polepole, Mwenyezi Mungu Muumba wa mbingu na ardhi, Aliyeumba watu, viumbe hai na visivyo hai, Akubariki na Akulinde. Unapiganie watu wa Mungu, na Mungu kwa Huruma na Upendo wake usio kikomo, ATAKULINDA dhidi ya maharamia hao. Naamini watashindwa tu. Haiwezekani Mwenyezi Mungu Aache kusikia kilio chetu Watanzania tulio wengi. Mungu Ibariki Tanganyika yetu. AMINA.
 
Wenye uwezo wa kupakua tupakulieni basi maana binafsi na hamu ya kuujua huu upuuzi uliomo ili nione pa kuanzia kuwalisha wananchi sumu waje waikatae kwa asilimia 90 na zaidi.

mbona iko kwenye thread nyingi tu hapa tangu mchana? nenda jukwaa la katiba kuna thread ipo imewekwa na mtaalam mmoja anajiita Profesa
 
Unafiki kitu kibaya sana, yaani ni dhambi mbaya sana. Ukimuona sitta anavyo toa ushirikiano kwa andrea utabaki kuduwaa. Andrea huyu wa vijisenti vya rada kageuka kinara wa kuandika katiba ya nji hii. Tena wenyewe wanasema ya miaka mpaka 100 ijayo.

Hawa wengine wanaandamana nchi nzima kuzuia bunge la bmk. Bunge linaendelea dodoma nyie mnaandama nchi nzima. Kwa nini msiandamane huko bunge liliko? Kama huku sikufikiri na kupanga kwa kutumia makalio tuite nini tena huku?

Kuhusu kufanya biashara na uongozi wa umma katiba imekaa kimya kwa lugha ya mtaani imepotezea hilo. Kazi tunayo kama taifa.
 
Rais kutoka znzn haiwezekani.? Milele. Mgombea mwenza ni ridhaa ya chama. Say rais mzanzibar Makamu muungano mtanganyika, makamu wa pili rais wa znz, makamu wa tatu waziri mkuu wa tz ambaye anateuliwa na rais mzbari anavyoona yampendeza na hakuna wa kuingilia uteuzi huo. Hivyo anaamua kumchagua mzanzibari. So tanganyika inatawaliwa na waznz. Hili ni ngumu kumeza
 
http:// api.ning.com/ files/ TQDVHBx0tuUoxwjg iL9qFDQQUzDLYpK W9GYBd7pqfkVhVv L1e4CK- tjubgrVL R2VENQzGLONSxok cRvLNPoV2cXYdQG 16vHZ/ RASIMU_YA_KATIBA _INAYOPENDEKEZW A_sw.pdf
 
Raisi wa Muungano kulipwa na Tanganyika, halafu Makamu wake pia, Then Makamu wa Kwanza naye kulipwa na Tanganyika then Waziri Mkuu kulipwa na Tanganyika, then wajumbe au wabunge wa bunge la muungano nao kulipwa na Tanganyika ambapo wa znz 10,000.00 wana mbunge waoo, wadanganyika zaidi ya 100,000 ndio wapate mbunge wao. hapo financial deiscipline hakuna kabisa na matusi toka zanjibari tutaendelea kuyapata kwamba tunawabania.
 
Baba wa Taifa alifanya mengi mazuri. Lakini sijapata jibu ni kwanini alitokea kuchukia kiasi hicho neno Tanganyika! Kwamba ukitamka neno Tanganyika unaonekana kama Shetani! Eti Uhuru wa Tanzania Bara; kwa hili Mwalimu alikosea sana.

akili ndogo haiwez kutawala akili kubwa mkuu yawezekana we si great thinker ktk forum za kisiasa fuatilia historia ya muungano na makubaliano ya marais wakat huo na si kulaumu mazingira yalifanya hivyo na mwl nyerere the man is saint 2be no comments
 

Mkuu Nguruvi3 again you are doing a great service to JF and Tanzania. Ni mjinga tu anayeweza kufananisha NO ya Scotland na NO ya CCM.

Nimefuatilia sana mjadala mzima wa Glasgow na nia ya kutaka kujitenga. It is exactly the same as what many in Tanzania are talking now. But even equally "Better together campaign", which to me sounded very much similar to the view of "wenye akili" wa visiwani Zanzibar, lengo lilikuwa sio kujitenga au la, leo lilikuwa fairness.

Mchawi wa Soctland ni Westimister, na huyo huyo ndio mchawi wa Engand.

Baada ya vote Cameron alisema wazi kuwa kutakuwa na suala la English laws for england, English men for english affairs, same to Wales, North Ireland and Scotland.

Tukumbuke mkenge wa UK ndio tulio nao sisi. Toafuti ni kuwa wenzetu chumi zao ni kubwa, kwa hiyo impact ya unyonyaji ni invisible kuliko ile ya kukwamisha mambo ya "ndani" ya members.

Sisi hapa kwetu Zanzibar ni parasite waziwazi kabisa, na kuna impact kubwa sana kwenye uchumi wetu.
 
akili ndogo haiwez kutawala akili kubwa mkuu yawezekana we si great thinker ktk forum za kisiasa fuatilia historia ya muungano na makubaliano ya marais wakat huo na si kulaumu mazingira yalifanya hivyo na mwl nyerere the man is saint 2be no comments

Nyerere ndie muhusika wa hili janga la muungano,ukifatilia historia utagundua yeye ndie alietumia nguvu nyingi kuificha tanganyika kwenye koti la muungano,amefariki lakini vibaraka wake nahisi wameanza kukosa nguvu za kuificha tanganyika kwenye koti la muungano.
 
Mimi pamoja na kuiona rasimu imejaa usanii mwingi lakini mantiki ya watu wanaoonesha kuwa wana uchungu sana na Tanganyika huwa siioni. Hii Tanganyika ambayo mnadai kwamba mnaipenda sana ilianzia wapi?? Tanganyika si ilizaliwa kule Berlin na wazungu? Sasa wewe leo umezaliwa kule Kishumundu mwaka 1967 halafu unajidai una uchungu sana na Tanganyika, huu uchungu unatoka wapi?

Hebu tuwe na uchungu na bara zima la Afrika basi kwa sababu hili bara lilitakiwa kuwa nchi moja tu. Hizi habari za Tangayika, Kenya, Uganda ... na msururu wa nchi zilizobakia ni wazungu ndio wametengeneza. Sioni sababu ya msingi sana ya mishipa kutusimama kwa kitu ambacho hata sio sisi tuliokianzisha!!
 
Rasimu iliyotolewa leo ni uharo mtupu, wanajisisifia na kutamba kwa mbwembwe na vitu ambavyo wanajuwa kabisa katika rasimu ya Mzee Sinde hayakuwekwa kwa sababu si ya muungano. Sasa sijui wanaona waTz wote ni wapumbavu kama wao, wacha tumalize uchaguzi ili tuandike katiba ya wananchi tuwaache na katiba yao ya ccm wakaitumie kuzimu!!!!!!!

Mkuu hatuna haja ya kupata hasira kwa kitu ambacho hakitaenda kwa wananchi. Baada ya UKAWA kuchukua nchi na hili liko wazi, hii takataka itatupiliwa mbali jalalani , kaeni na amani wakuu.
 
Back
Top Bottom