Rasimu ya Katiba inayopendekezwa 2014

Rasimu ya Katiba inayopendekezwa 2014

Hivi, ukiiweka rasimu hii ya katiba, pembeni ya rasimu ya pili ya tume kuna tofauti zipi ambazo zimejitokeza ukiacha kuundwa kwa shirikisho la serikali 3. nadhani haya ndio ya kujadili zaidi kwa nini wananchi hasiikubali rasimu hii badala ya kutumika kisiasa. Tuyasome mapendekezo yao na tuyachambue wapi wananchi hawaridhiki badala ya kuendelea kulilia rasimu ya Warioba ambayo ingepitia mtihani huu vile vile.
 
Kinacholeta utata zaidi ni pale ambapo kwenye sifa za mtu anayeweza kugombea Urais wa Muungano inatamka kuwa Mtu yeyote aliyeshika madaraka ya Urais wa Zanzibar ataruhusiwa kugombea nafasi ya Urais wa Muungano na hivyo atasimamia mambo yote ya Tanzania Bara na alhali akisimamia ya Muungano pia. Je, kama ni hivyo kuwa mtu aliyewahi kuwa Rais wa Zanzibar anaweza kuwa pia Rais wa Muungano, ni kwa nini Rais wa Muungano anayetoka Tanganyika (aka Tanzania Bara) asiweze kugombea Zanzibar na kuwa Rias wa Zanzibar? Sidhani kama suala la Rais Mwinyi (anayethibitisha kuwa yeye ni Mtanganyika aliyezaliwa Kisarawe) kutawala Zanzibar na kisha Tanganyika na Jamhuri ya Muungano itajirudia tena. CCM kuna agenda gani ya siri kwenye rasimu hii ya Chenge inayoendana na mambo yenu ya Chama (Japo mlishafikia ku-exclude mgombea wa Muungano kutoka Zanzibar kwa kusitisha utaratibu wa ROTATION ya kugombea U-Rais)!!!

Mbona rasimu inaruhusu sehemu moja kutawala mambo ya ndani ya sehemu nyingine alhali hayaihusu sehemu hiyo? Rais wa Muungano ni Kiongozi mkuu wa Tanganyika na Jamhuri ya Muungano. Huu ni UDUKUZI wa Hali ya JUU wa mambo ya siri na ndani kabisa ya sehemu nyingine. Tunahatarisha usalama wa sehemu moja ya Muungano. Hii kitu haijakaa sawa. Kuna wenye macho na masikio na akili kutuzidi katika nyakati zijazo watakuja kufanya maamuzi sahihi. Hii issue ya Katiba na Muungano bado ni EPISODES katika Season moja tu zinaendela. SEASON nyingine yenye maamuzi mtambuka itakuja leo ama kesho. Ni suala la muda tu.
 
Ni shidaaa... kuwa mwanasiasa kosa moja unaishi nalo miaka... ubora wako na uwezo wako unakuwa hauthaminiki...
 
Hivi, ukiiweka rasimu hii ya katiba, pembeni ya rasimu ya pili ya tume kuna tofauti zipi ambazo zimejitokeza ukiacha kuundwa kwa shirikisho la serikali 3. nadhani haya ndio ya kujadili zaidi kwa nini wananchi hasiikubali rasimu hii badala ya kutumika kisiasa. Tuyasome mapendekezo yao na tuyachambue wapi wananchi hawaridhiki badala ya kuendelea kulilia rasimu ya Warioba ambayo ingepitia mtihani huu vile vile.
Kilichoandikwa na Chenge ni maoni ya rasimu yao ya mafichoni.
Kuyajdili ni kutoa uhalali usiohitajika.

Tume ya Warioba usioikubali, mapendekezo yake yamepigwa chini.

Haya unayoyaona ni ya tume ya Samwel Sitta na Shibuda waliojiteua na kuanza kuongea na wafugaji na wakulima tu.

Tena wanatumia takwimu za wakulima 17 na wafugaji 23.

Wewe Mkandara ulihoji takwimu za Warioba kama si sahihi, hebu tueleze takwimu za watu 40 zina usahihi gani.

Mkuu, katiba ni nyaraka nyeti si daftari la shule kama unavyodhani.

Hakuna maoni ya wananchi, hakuna kujadili

Mkandara exposure inakusaidiaje mkuu.
Hata wewe unaamini mtovu na muovu kama Cheng anaweza kuandika kitu cha maana ukajadili kweli.

Kwamba hukuona usanii wa kupiga kura kwa internet via yahoo na fax bila msimamizi.

Huoni vituko vyote hivyo unataka watu wajadili upuuzi.

Mkuu, kwani hukuona jinsi vifungi 1 na 6 vilivyoepukwa. Hivi unawezaje kujadili jengo bila msingi.

CCM wenyewe awanasema vifungi hivyo ni moyo wa katiba, wewe unavikwepa kwasababu tu unataka kulinda masilahi ya S2 kwa faida za wazanzibar.

Unasikitisha sana, najiuliza huko vijijini sijui ni aje kama mtu mwenye fursa kama wewe hawezi kuona umbali zaidi ya pua yako
 
Hivi, ukiiweka rasimu hii ya katiba, pembeni ya rasimu ya pili ya tume kuna tofauti zipi ambazo zimejitokeza ukiacha kuundwa kwa shirikisho la serikali 3.
kama hujaona tofauti ninawasi wasi mkubwa sana na uwezo wako wa kusoma na kuelewa. Hata wewe na exposure huwezi kuona hilo, tuna safari ndefu sana.

Nadhani diaspora wanashika vichwa maana kama wewe ndie muwakilishi wao, ni shiida!
 
"Mkuu wa Mkoa wowote katika Zanzibar
atatekeleza kazi na shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
atakazokabidhiwa na Rais wa Zanzibar, na kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya
1984 au sheria yoyote iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi..."
Hapa pakoje au ina maana mkuu wa mkoa Zanzibar ni mlolongo wa mamlaka ya raisi wa muunganao kwenda kwa rais wa zanziba na halafu mkuu wa mkoa au vipi? kwa nini Zanzibar ilazimike kufuata utaratibu huu wakati ni serikali inayojitegemea na pia ni sehemu/nchi ndogo tu ambayo si lazima iwe na mikoa, wilaya, tarafa ...
 


Huu ni uendawazimu...

Wakati wenzetu wenye maono na matumaini wanatumia fursa ya kutunga katiba mpya kutoa mchango wa kimapinduzi sisi tunaleta mawazo mgando. Hii mijitu gani hii, eti mibunge? Inakula tu hela za nchi, bila ya aibu. Njaa! Kweli hatari.

Hii ni najisi, upuuzi mtupu. Yaani Chenge Mbunge aliyeiba zile fedha za Rada, kushirikiana na Barclays na BAE ndio msimamizi wa uandishi wa katiba ya nchi. Kweli? kweli, kweli Tanzania Bomu.

Hivi Lowassa na Chenge ni marafiki?


Ukurasa wa 17 – Eti "ushiriki Mpana"

NA KWA KUZINGATIA, uzoefu wa zaidi ya Miaka Hamsini ya Uhuru wa Tanganyika, Miaka Hamsini ya Mapinduzi ya Zanzibar na Miaka Hamsini ya Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, na umuhimu wa ushiriki mpana na bayana wa wananchi katika utungaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

HIVYO BASI, KATIBA HII YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ILIYOPENDEKEZWA NA BUNGE MAALUM LA KATIBA imetungwa na SISI WANANCHI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA kupitia KURA YA MAONI kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na kuhakikisha kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia na utawala wa sheria, kujitegemea na isiyofungamana na dini.

Huu ni ujinga – Kwanini rais ateue mwanasheria mkuu na kwanini asisahiliwe na majaji wakuu, tena kwa uwazi (kwenye TV) kama ilivyo Kenya nan chi nyingine?

Ukurasa – 37-38

110.-(1) Kutakuwa na Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano watakaoteuliwa na Rais kwa kushauriana na Makamu wa Rais.

(c) Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Mwanasheria Mkuu wa Serikali
113.-(1) Kutakuwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano ambaye katika Katiba hii ataitwa kwa kifupi kama “Mwanasheria Mkuu” ambaye atateuliwa na Rais.
(2) Mtu ataweza kuteuliwa kuwa.....


115.-(1) Kutakuwa na Mkurugenzi wa Mashtaka ambaye atateuliwa na Rais,

116.-(1) Kutakuwa na Katibu Mkuu Kiongozi atakayeteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa Maafisa Waandamizi walio katika nafasi ya uteuzi katika Utumishi wa Umma.

(2) Wakuu wa Mikoa katika Tanzania Bara watateuliwa na Rais baada ya kushauriana na Waziri Mkuu.


(c) wabunge wasiozidi kumi watakaoteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa watu wenye sifa za kuwa wabunge;

WABUNGE -

140.-(1) Kila Mbunge kabla ya kumalizika siku thelathini tangu aapishwe kushika nafasi ya madaraka ya Mbunge sharti awasilishe kwa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma nakala mbili za tamko rasmi kuhusu mali na madeni kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
(2) Tamko rasmi lililotajwa katika ibara ndogo ya (1), litatolewa katika fomu maalum itakayoandaliwa kwa mujibu wa
sheria.

Huyo Chenge ametaja vijisenti vyake, na alivipataje?
JAJI

170.-(1) Jaji Mkuu atateuliwa na Rais kutoka orodha ya majina ya watu watatu yaliyopendekezwa na Tume ya Utumishi wa Mahakama.
(2) Jaji Mkuu ndiye atakuwa Mkuu wa Mhimili wa Mahakama katika Jamhuri ya Muungano.

.....na upuuzi mwingine.......
Hii siyo katiba mpya.

Vya muhimu zaidi ni vile ambavyo, wameviondoa. Hii siyo katiba ya kupitisha.

U
Mkuu shukran haya ndio mambo ya kuyatazama na kuyapinga waziwazi..
 
"Mkuu wa Mkoa wowote katika Zanzibar
atatekeleza kazi na shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
atakazokabidhiwa na Rais wa Zanzibar, na kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya
1984 au sheria yoyote iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi..."
Hapa pakoje au ina maana mkuu wa mkoa Zanzibar ni mlolongo wa mamlaka ya raisi wa muunganao kwenda kwa rais wa zanziba na halafu mkuu wa mkoa au vipi? kwa nini Zanzibar ilazimike kufuata utaratibu huu wakati ni serikali inayojitegemea na pia ni sehemu/nchi ndogo tu ambayo si lazima iwe na mikoa, wilaya, tarafa ...
Katiba hii ni sheria mama itafuatwa na serikali zote, hivyo japo mamlaka ya utekelezaji shughuli zake yapo kwao lakini mamlaka walonayo hayawezi kukiuka mwongozo huu (Principal). Kifupi katiba hii haiwezi upita tumeliwa mchana kweupeeee. Wajumbe wa baraza hilo wengine walijua hawatarudi bungeni hivyo wamejijengea mtaji tosha wa kuanza maisha mapya ya Utajirisho..
 
Asante sana Mkuu. Hata hivyo kabla sijaipakua, naomba kufahamishwa kama Kadhi yumo au hayumo.

hayumo labda kamuulize mkuu wa bakwata we kadhi wanini? kwanza hana maana sisi tunataka tanganyika kama unataka mahakama ya kiislam nenda wanakokata vichwa kule IRAN NA IRAKI
 
TUME HURU YA UCHAGUZI
(a) Tume Huru ya Uchaguzi
Kuundwa kwa
Tume Huru ya
Uchaguzi
211.-(1) Kutakuwa na Tume Huru ya U chaguzi ya Jamhuri ya
Muungano itakayoitwa “Tume Huru ya Uchaguzi”.
(2) Tume Huru ya Uchaguzi itakuwa na Mwenyekiti, Makamu
Mwenyekiti na wajumbe wengine saba watakaoteuliwa na Rais baada ya
kupendekezwa na Kamati ya Uteuzi.
(3) Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe wa Tume Huru ya
Uchaguzi watashika madaraka mara baada ya kuapishwa na Rais.
(4) Uteuzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya
Uchaguzi utafanywa kwa misingi kwamba, endapo Mwenyekiti atateuliwa kutoka
upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano, basi Makamu Mwenyekiti atateuliwa
kutoka upande wa pili wa Jamhuri ya Muungano.

Hii ni tume ya Rais ya uchaguzi
 
Mkandara watu wanataka rasimu maana znz kule sasa watanganyika hawaruhusiwi kumiliki ardhi, usawa katika kuchangia muungano kwa nchi mbili washirika hauonekani katika muundo huu,watanganyika hawaruhusiwi kuajiriwa smz lakini waznz ruksa maana ni serikali ya muungano na wanatengewa 21% ya ajira zote,tofauti za kodi wazanzibar wanaagiza magari wanakatwa kodi kidogo na tra kuliko watanganyika,utofauti wa ukumbwa wa majimbo kwa zanzibar na tanganyika idadi ya kura za mbunge wa ubungo ni sawa na za rais zanzibar sasa kama wabunge huku wako 70 maana yake utendaji wao jimboni unakuwa mzuri maana hawana eneo kubwa la kuzunguka angali mfuko wa jimbo wanapewa sawa kwa wabunge wote.ubaguzi kwa watanganyika wanaoenda zanzibar kutafuta ajira nao ni kero inayopelekea watu kudai serikali tatu.
 
Last edited by a moderator:
Sijui ina maana gani, labda kuna mwenye kuweza kunisadia, Mbunge nimemchagua kwa Kura yangu mwenyewe, Hajakidhi matakwa yetu, kahamia anapopajua katuacha, Kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye ina maana kwa CCM kosa? Kwa nini kulazimishiana utawala? Rais Bunge limepewa mamlaka ya kupiga kura ya kutokuwa na imani naye, Mbunge hapana, Sijui labda mwenye kuweza kuniambia maana yake...

Mod usiitoe plz
 
Back
Top Bottom