Rasimu ya Katiba inayopendekezwa 2014

Rasimu ya Katiba inayopendekezwa 2014

Leo taifa letu limeaibishwa mbele ya mataifa ya watu wanaojielewa na kujitambua. Tanzania hatutanusa maendeleo iwapo mafisadi wameachwa kuwa na upper hand hata kwenye mambo sensitive kama katiba.

Ukisoma kwa makini kilichowasilishwa leo ni mabadiliko yasiyokuwa ya msingi kufurahisha wakulima, wasanii, wanawake, wavuvi na wafugaji kwa maneno mazuri yasiyo na jinsi ya kuyatekeleza (nadhani lengo likiwa kurubuni ili kupata kura zao) huku mifumo inayo athiri maisha ya watu hao hao yakipewa mwanya kwa mafisadi kuendeleza desturi ya kutoa haki kama hisani; mfano: uteuzi wa watu muhimu, uajibishaji kwa wawakilishi, muundo wa serikali unaotengeneza kichaka cha kuficha ficha baadhi ya mambo, kwa uchache!

Ee Mungu tukumbuke sisi wana wa taifa hili ambalo future yake bila wewe ni kiza nene!
 
Tangu hilo BMK liundwe, liliundwa kwa ajili ya kujilinda wenyewe waliopo na waliowahi kushika madaraka. Hii ndiyo nafasi ya kipekee ambayo waliipata kujiwekea usalama wao baada ya kuona hofu ya upinzani na vuguvugu la mabadiliko.
Toka lini kinyozi ajinyoe?? Uende kumwambia mbunge ati ajitengenezee katiba ya kujiondoa mwenyewe madarakani, kujiwekea vipingamizi kuwa; Elimu yake iwe ya kiwango, muda wake uwe na mwisho, awajibishwe na walio mchagua kabla ya miaka 5. Hiyo fedha aliyoitumia kuwahonga nyiye wapiga kura mtairudishaje???
Jamani, tangu Mh. Baba wa kaya alipo inua mkono na kusema atateua hilo bunge, nilijua hakuna kitu hapo. Tulichagua wawakilishi wetu kuingia Legico ili kubadili katiba ya Malkia na kuingiza ile ya Tanganyika huru. Tuliwapigia kura na kuwachagua. Sasa hii ya kumpa kazi mtu mmoja tu ati ni rais, matokeo ndo hayo, mjomba, shangazi, mwanaye na hata wanamazingaumbwe wake. Tulitegemea nini zaidi?
Acheni Chenge Vijisenti atoe somo kwa watu hawa wasio na ufaham.
 
Wadau nimepitia Rasimu iliyowasilishwa kwa Mwenyekiti wa BMK kwa kweli ni kituko. Yaani ni kama ilani ya CCM wamejiandalia na si Katiba. Rais amebaki na Mamlaka yale yale ya kuteua hadi wakuu wa wilaya bila kudhibitishwa na chombo kingine. Kwa kifupi nakala ya rasimu hiyo ipo wadau msome then mje mtuambie kama kweli hii ndo rasimu ya katiba au ilani ya CCM.

Kwani hii rasimu maoni yake yametoka wapi, yamekusanywa lini, na nani na kwa mamlaka gani????
 
g)
(2) Wakuu wa Mikoa katika Tanzania Bara watateuliwa na Rais baada ya
kushauriana na Waziri Mkuu.
(3) Wakuu wa Mikoa katika Zanzibar watateuliwa na Rais wa Zanzibar.

(5) Pamoja na wajibu na madaraka yake yaliyotajwa kwenye masharti
yaliyotangulia ya Ibara hii, Mkuu wa Mkoa wa mkoa wowote katika Zanzibar
atatekeleza kazi na shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
atakazokabidhiwa na Rais wa Zanzibar, na kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya
1984 au sheria yoyote iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
Kwa nini neno Tanganyika linakera sana kutamkwa kwenye rasimu CCM na neno Zanzibar halileti kero?

Katiba inayotamkwa hapo kwenye ibara ndogo ya 5 inaashiria kuwa mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar ya hivi karibuni hayakuzingatiwa kwenye rasimu na hivyo rasimu inaharamisha katiba hiyo? Je, wajumbe wa baraza la wawakilishi lenye wajumbe kwenye BMK wanamaanisha walitumia fedha za wananchi kwa kutunga katiba ambayo wameshindwa kuona umuhimu wake kwenye Rasimu hii ya Chenge?

Filamu imeanza..staring ndo kwanza yuko ughaibuni, tusubiri SEASON mpya
 
Kapotoka huyu fisadi tena hajitambui!!! hawa mapanya na mafisi wanaokwapua mapesa chungu nzima ya walipa kodi kila mwaka nao kwa sababu wanaongea lugha ya Taifa basi nao ni Wazalendo!!!

Chenge: uzalendo sio tunu ya taifa kwasababu mtu hazaliwi akiwa mzalendo, uzalendo unatengenezwa tena kwa muda mrefu. Chenge tena: moja ya uzalendo ni lugha ya taifa. My take. hivi mtu anazaliwa akiwa anajua lugha ya taifa, nisaidieni jamani nyie ambao angalau mlimaliza darasa la saba, mi hali yangu mbaya kielimu
 
Nimeipitia hiyo rasimu, kusema kweli haina lolote jipya, raisi bado ana madaraka makubwa, hakuna tume huru ya uchaguzi kwa vile bado inateuliwa na raisi na mengineyo mengi. Kusema kweli mawazo ya wananchi yametupiliwa mbali na ccm wamejihidi sana kulinda maslahi ya watawala.
 
Nimeipitia hiyo rasimu, kusema kweli haina lolote jipya, raisi bado ana madaraka makubwa, hakuna tume huru ya uchaguzi kwa vile bado inateuliwa na raisi na mengineyo mengi. Kusema kweli mawazo ya wananchi yametupiliwa mbali na ccm wamejihidi sana kulinda maslahi ya watawala.

Lengo lao halikuwa katiba mpya,ilikuwa ni kuweka viraka kwenye katiba ya zamani
 
Naheshimu mawazo yoote humu... njia rahisi ya kukritique ni kuchukua nafasi ya wewe kuwa raisi au mbunge au nafasi yeyote iliyopewa majukumu kikatoba.. ni rahisi kuongea si kutenda. Ukiwa kiongozi halafu kila unalofanya zuri linakosolewa ikiwamo kuyokuwa na uhuru wa kufanya maamuxi au uteuzi itakuwaje? Na ukiteua kwa uhuru ukajikuta umeingiza wasioafikiana na wewe kuna kazi itafanyika? Kuna swala la ulinzi na usalama ukiacjia kila kitu bila kuwa na mamlaka kamili kama kiongozi hii nchi kila miezi sita tutakuwa na uchaguzi hakuna kazi nyingine... ni bema kutafakari...
 
Nimeipitia hiyo rasimu, kusema kweli haina lolote jipya, raisi bado ana madaraka makubwa, hakuna tume huru ya uchaguzi kwa vile bado inateuliwa na raisi na mengineyo mengi. Kusema kweli mawazo ya wananchi yametupiliwa mbali na ccm wamejihidi sana kulinda maslahi ya watawala. [/QUOTE mambo mapya yameongezeka tens Mazari ila kwa Kuwa haijaonesha baadhi ya mambo ya. msinigi ambayo watanzania wengi waliyatoa kama maoni ; basi hualali ni mdogo. kuhusu MA
daraka ya raising sioni tatizo kwenye rasim ipendekezwayo.
 
HII naona kama sawa na ile ya mwaka 1977 au nimekosea...sioni jipya

b) Baraza la Mawaziri
Baraza la 109.-(1) Kutakuwa na Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano
Mawaziri ambalo litakuwa na wajumbe wafuatao:
(a) Rais;
(b) Makamu wa Kwanza wa Rais;
(c) Rais wa Zanzibar ambaye ni Makamu wa Kwanza wa Rais;
(d) Waziri Mkuu ambaye ni Makamu wa Tatu wa Rais; na
(e) Mawaziri wote wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(2) Rais ataongoza mikutano ya Baraza la Mawaziri, na endapo Rais
hayupo, mikutano itaongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais na kama wote
wawili hawapo, Waziri Mkuu ataongoza Mikutano hiyo.
Hapa sijaelewa ina maana Zanzibar haitakua na raisi wa Jamhuri ya Tanzania?maana naona Makamu wa kwanza lazima awe kutoka Zanzibar
Jee Makamu wa pili wa Rais ni nani?
Mapendekezo hayo yote yanafuata katiba ya ccm jinsi ilivyo.
Tutatumia nguvu zote kupinga uchafu huu kwa wananchi
 
Jamani naomba msaada maana naona kama changa la macho;tulikubaliana kuwa serikali 3 ni gharama sasa huyu raisi wa nzanzibar kuwa makamu wa 1 wa jamhur ya muungano wa tz nikuwa akija kufanya shughuli za muungano kama makam wa rais halipwi? Na kama analipwa nini tofauti na serikali tatu
 
Back
Top Bottom