Rasimu ya Katiba inayopendekezwa 2014

Rasimu ya Katiba inayopendekezwa 2014

hapa sijaelewa ina maana zanzibar haitakua na raisi wa jamhuri ya tanzania?maana naona makamu wa kwanza lazima awe kutoka zanzibar
jee makamu wa pili wa rais ni nani?
Mapendekezo hayo yote yanafuata katiba ya ccm jinsi ilivyo.
Tutatumia nguvu zote kupinga uchafu huu kwa wananchi

maanake zanzibar tumezikwa rasmi kwenye hii katiba mpya,makamu wa 2 ni wazir mkuu.na wazir mkuu anatoka wapi na nikwanini.
 
naheshimu mawazo yoote humu... Njia rahisi ya kukritique ni kuchukua nafasi ya wewe kuwa raisi au mbunge au nafasi yeyote iliyopewa majukumu kikatoba.. Ni rahisi kuongea si kutenda. Ukiwa kiongozi halafu kila unalofanya zuri linakosolewa ikiwamo kuyokuwa na uhuru wa kufanya maamuxi au uteuzi itakuwaje? Na ukiteua kwa uhuru ukajikuta umeingiza wasioafikiana na wewe kuna kazi itafanyika? Kuna swala la ulinzi na usalama ukiacjia kila kitu bila kuwa na mamlaka kamili kama kiongozi hii nchi kila miezi sita tutakuwa na uchaguzi hakuna kazi nyingine... Ni bema kutafakari...

ingekuwa hivyo tusingetengeneza katiba mpya bali tungeboresha katiba iliyopo.tulitaka katiba iakisi mazingira ya tz
 
Ndugu wana jf... Kilichosomwa bungeni tayari kwa kujadiliwa na bunge kabla ya kupigiwa kura hiki hapa....

Huu ni uendawazimu...

Wakati wenzetu wenye maono na matumaini wanatumia fursa ya kutunga katiba mpya kutoa mchango wa kimapinduzi sisi tunaleta mawazo mgando. Hii mijitu gani hii, eti mibunge? Inakula tu hela za nchi, bila ya aibu. Njaa! Kweli hatari.

Hii ni najisi, upuuzi mtupu. Yaani Chenge Mbunge aliyeiba zile fedha za Rada, kushirikiana na Barclays na BAE ndio msimamizi wa uandishi wa katiba ya nchi. Kweli? kweli, kweli Tanzania Bomu.

Hivi Lowassa na Chenge ni marafiki?


Ukurasa wa 17 – Eti "ushiriki Mpana"

NA KWA KUZINGATIA, uzoefu wa zaidi ya Miaka Hamsini ya Uhuru wa Tanganyika, Miaka Hamsini ya Mapinduzi ya Zanzibar na Miaka Hamsini ya Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, na umuhimu wa ushiriki mpana na bayana wa wananchi katika utungaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

HIVYO BASI, KATIBA HII YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ILIYOPENDEKEZWA NA BUNGE MAALUM LA KATIBA imetungwa na SISI WANANCHI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA kupitia KURA YA MAONI kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na kuhakikisha kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia na utawala wa sheria, kujitegemea na isiyofungamana na dini.

Huu ni ujinga – Kwanini rais ateue mwanasheria mkuu na kwanini asisahiliwe na majaji wakuu, tena kwa uwazi (kwenye TV) kama ilivyo Kenya nan chi nyingine?

Ukurasa – 37-38

110.-(1) Kutakuwa na Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano watakaoteuliwa na Rais kwa kushauriana na Makamu wa Rais.

(c) Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Mwanasheria Mkuu wa Serikali
113.-(1) Kutakuwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano ambaye katika Katiba hii ataitwa kwa kifupi kama “Mwanasheria Mkuu” ambaye atateuliwa na Rais.
(2) Mtu ataweza kuteuliwa kuwa.....


115.-(1) Kutakuwa na Mkurugenzi wa Mashtaka ambaye atateuliwa na Rais,

116.-(1) Kutakuwa na Katibu Mkuu Kiongozi atakayeteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa Maafisa Waandamizi walio katika nafasi ya uteuzi katika Utumishi wa Umma.

(2) Wakuu wa Mikoa katika Tanzania Bara watateuliwa na Rais baada ya kushauriana na Waziri Mkuu.


(c) wabunge wasiozidi kumi watakaoteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa watu wenye sifa za kuwa wabunge;

WABUNGE -

140.-(1) Kila Mbunge kabla ya kumalizika siku thelathini tangu aapishwe kushika nafasi ya madaraka ya Mbunge sharti awasilishe kwa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma nakala mbili za tamko rasmi kuhusu mali na madeni kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
(2) Tamko rasmi lililotajwa katika ibara ndogo ya (1), litatolewa katika fomu maalum itakayoandaliwa kwa mujibu wa
sheria.

Huyo Chenge ametaja vijisenti vyake, na alivipataje?
JAJI

170.-(1) Jaji Mkuu atateuliwa na Rais kutoka orodha ya majina ya watu watatu yaliyopendekezwa na Tume ya Utumishi wa Mahakama.
(2) Jaji Mkuu ndiye atakuwa Mkuu wa Mhimili wa Mahakama katika Jamhuri ya Muungano.

.....na upuuzi mwingine.......
Hii siyo katiba mpya.

Vya muhimu zaidi ni vile ambavyo, wameviondoa. Hii siyo katiba ya kupitisha.

U
 
Kabla ya wakoloni kuigawa afrika, kulikuwa na nchi tanganyika? Tanzania ni zao na mawazo na mwelekeo wa watu huru wenye akili timamu. Hiyo tanganyika ni ya wakoloni.

Nakupuuza , halafu nakudharau pia!
najua ni njaa tu inakusumbua!
kwanini hujuulizi ni vingapi vya mkoloni tunatumia na kwanini hatubadilishi? ni barabara ngapi tumabadili majini ya ASILI na kuweka ya KIKOLONI?

Unamjua shilingi wewe?


nasema Nakuupuuza tena!
 
Fungua bungemaalum.go.tz kupakua rasimu ya Sitta.

Wenye uwezo wa kupakua tupakulieni basi maana binafsi na hamu ya kuujua huu upuuzi uliomo ili nione pa kuanzia kuwalisha wananchi sumu waje waikatae kwa asilimia 90 na zaidi.
 
Hii sio katiba, ni uchafu kabisa.
Dr. Hellen kijo ameongea leo point sana chanel 10...watanzania sisi ni waoga sana. Tukitishwa na chagonja tu hatuwezi kudai haki yetu. Tunaogopa kupigwa na kufa, lakn hata kama hutakufa lwa kudai haki yako bado utakufa kwa kunyimwa haki yako. Beter ufe kwa kudai haki yako.
Watz kama tukiamu huu ufafu hautapita. Huu ni uchafu tena matapishi ya sitta na chenge. I hate these guys
 


Huu ni uendawazimu...

Wakati wenzetu wenye maono na matumaini wanatumia fursa ya kutunga katiba mpya kutoa mchango wa kimapinduzi sisi tunaleta mawazo mgando. Hii mijitu gani hii, eti mibunge? Inakula tu hela za nchi, bila ya aibu. Njaa! Kweli hatari.

Hii ni najisi, upuuzi mtupu. Yaani Chenge Mbunge aliyeiba zile fedha za Rada, kushirikiana na Barclays na BAE ndio msimamizi wa uandishi wa katiba ya nchi. Kweli? kweli, kweli Tanzania Bomu.

Hivi Lowassa na Chenge ni marafiki?


Ukurasa wa 17 – Eti "ushiriki Mpana"

NA KWA KUZINGATIA, uzoefu wa zaidi ya Miaka Hamsini ya Uhuru wa Tanganyika, Miaka Hamsini ya Mapinduzi ya Zanzibar na Miaka Hamsini ya Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, na umuhimu wa ushiriki mpana na bayana wa wananchi katika utungaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

HIVYO BASI, KATIBA HII YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ILIYOPENDEKEZWA NA BUNGE MAALUM LA KATIBA imetungwa na SISI WANANCHI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA kupitia KURA YA MAONI kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na kuhakikisha kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia na utawala wa sheria, kujitegemea na isiyofungamana na dini.

Huu ni ujinga – Kwanini rais ateue mwanasheria mkuu na kwanini asisahiliwe na majaji wakuu, tena kwa uwazi (kwenye TV) kama ilivyo Kenya nan chi nyingine?

Ukurasa – 37-38

110.-(1) Kutakuwa na Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano watakaoteuliwa na Rais kwa kushauriana na Makamu wa Rais.

(c) Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Mwanasheria Mkuu wa Serikali
113.-(1) Kutakuwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano ambaye katika Katiba hii ataitwa kwa kifupi kama “Mwanasheria Mkuu” ambaye atateuliwa na Rais.
(2) Mtu ataweza kuteuliwa kuwa.....


115.-(1) Kutakuwa na Mkurugenzi wa Mashtaka ambaye atateuliwa na Rais,

116.-(1) Kutakuwa na Katibu Mkuu Kiongozi atakayeteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa Maafisa Waandamizi walio katika nafasi ya uteuzi katika Utumishi wa Umma.

(2) Wakuu wa Mikoa katika Tanzania Bara watateuliwa na Rais baada ya kushauriana na Waziri Mkuu.


(c) wabunge wasiozidi kumi watakaoteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa watu wenye sifa za kuwa wabunge;

WABUNGE -

140.-(1) Kila Mbunge kabla ya kumalizika siku thelathini tangu aapishwe kushika nafasi ya madaraka ya Mbunge sharti awasilishe kwa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma nakala mbili za tamko rasmi kuhusu mali na madeni kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
(2) Tamko rasmi lililotajwa katika ibara ndogo ya (1), litatolewa katika fomu maalum itakayoandaliwa kwa mujibu wa
sheria.

Huyo Chenge ametaja vijisenti vyake, na alivipataje?
JAJI

170.-(1) Jaji Mkuu atateuliwa na Rais kutoka orodha ya majina ya watu watatu yaliyopendekezwa na Tume ya Utumishi wa Mahakama.
(2) Jaji Mkuu ndiye atakuwa Mkuu wa Mhimili wa Mahakama katika Jamhuri ya Muungano.

.....na upuuzi mwingine.......
Hii siyo katiba mpya.

Vya muhimu zaidi ni vile ambavyo, wameviondoa. Hii siyo katiba ya kupitisha.

U

chenge anausafi gani?

Si unaona mwenzake sitta ndo anamsifia mzalendo kaandika katiba, na atakubukwa kwenye historia. Hyu msukuma hata sijamuelewa alikuwa anamung'unya maneno tu. Mzee mwizi huyu nde apewe kandia katiba, ana usafigani
 
Nimeisoma Rasimu ya Katiba
Inayopendekezwa, nimeisoma yote, ni bahati
mbaya inapigiwa upatu kwamba imebeba
mambo ya wananchi, mambo ya wakulima,
wafugaji, wavuvi, vijana na kadharika. Jamani
hayo ni hadaa, msingi wa muundo
umebadilishwa, Tanganyika imevalishwa koti
jipya la Muungano, ambalo tusipokuwa
makini itaendelea kuishi nalo muda mrefu
zaidi.

Kigezo cha kukataa serikali 3 hakina
hoja zenye mashiko, wanasema Hati ya
Makubaliano ilisema serikali 2 hivyo hatuwezi
badili, huu ni uongo, mbona Hati ilisema
mambo ya Muungano ni 11, mbona wao
wameweka 14, uhalali wa kubadili mambo ya
Muungano kama Hati haibadiliki wanaupata
wapi.? Hii ni double standard. hati
haikujieleza kwamba kwa baadhi ya maeneo
mwiko kubadili na ruksa kwa mengine, Amka
ee Mtanzania.

Unasema katika Sura ya Pili unaanzisha Tume
ya Mipango ya Taifa ilhali ukijua Zanzibar
wana Tume ya Mipango pia, nashangaa sana.
Rasimu ya Katiba Inayopendekezwa inasema
Kutakuwa na Dira, Ohoo, kutakuwa tena,
nilidhani inapaswa itamkwe, na kwa asili ya
"Programmatic Constitutions" Dira inakuwa
ni ujumla wa Lengo Kuu la Katiba Pamoja na
Malengo Mahususi kama ilivyokuwa kwenye
Rasimu.

Wamefuta kumwajibisha Mbunge, wamefuta
ukomo, wamefuta mbunge asiwe waziri,
wamefanya ugombea binafsi kuwa mgumu
zaidi, wamevuruga Tume ya Uhusiano na
Uratibu, wao wamesema Tume hii ni kwa
Mambo ya Muungano, hili ni kosa kubwa la
kisanifu (design), Mambo ya Muungano
yanasimamiwa, yasiyo ya Muuungano
yanaratibiwa.

Wameweka Baraza la Vijana,
vijana wenzangu hii ni hadaa, walio wengi ni
wanawake mbona lao hawakuliweka,
ninazingatia haki hapa, wanataka
kuwahamasisha kwa mambo ambayo katika
utalaamu na uandishi wa Katiba hayapo,
yamewekwa ili msahau yale waliyofuta.
Wamerudisha wakuu wa Mikoa, wananchi
mlisema sana juu ya uwepo wa wakuu wa
mikoa na wilaya.. kwa namna walivyo rudi
sitashangaa wakiendelea kuwa makada wa
vyama vya siasa. Haya maoni ya kuwaweka
wakuu wa mikoa katika namna hii wameyatoa
wapi.? Maoni hayo mimi sikuyaona Tume ya
Katiba kipindi chote nilichokuwepo.

Vyanzo vya mapato ni vile vile kwa serikali ya
muungano (Katiba ya 1977) na wakadhani
mwarobaini ni kurejesha Tume ya Pamoja ya
Fedha ambayo haikuwahi kufanyiwa kazi
(kuna sababu kubwa zaidi kuliko kuwa na
Tume ya Pamoja ya Fedha), Bahati mbaya
Rasimu ya Katiba Inayopendekezwa imelikosa
hili.

Rasimu ya Katiba inayopendekezwa inasema
Makamu wa Rais Watatu, Makamu wa Kwanza
(Muungano), Makamu wa Pili (Rais wa
Zanzibar) na Makamu wa Tatu (Waziri Mkuu
wa Jamhuri ya Muungano)... Jamani
watanzania wenzangu, huu UTATU mbona
tunapewa kwa mgongo wa chupa, TATU
tunaziogopea nini.? Tume ya Pamoja ya Fedha
iliwaambia anzisheni akaunti ya pamoja ya
fedha, ikawa kigugumizi, leo kipi kitafanya
tuweze?
Mnasema Mahakama Kuu ya Zanzibar na
Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano
zitakuwa na Mamlaka sawa (concurrent
jurisdiction), hata kwa jina hapo si
tunadanganyana.? Hakuna kitu kama
Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano,
kwasababu ninyi mnajua haina Mamlaka
Zanzibar sasa kuiweka kwenye Muungano
kunani.?

NINAENDELEA NA UCHAMBUZI, KAMA
NILIVYOSEMA KAZI NDIO KWANZA IMEANZA.
 
TUME HURU YA UCHAGUZI
(a) Tume Huru ya Uchaguzi
Kuundwa kwa
Tume Huru ya
Uchaguzi
211.-(1) Kutakuwa na Tume Huru ya U chaguzi ya Jamhuri ya
Muungano itakayoitwa “Tume Huru ya Uchaguzi”.
(2) Tume Huru ya Uchaguzi itakuwa na Mwenyekiti, Makamu
Mwenyekiti na wajumbe wengine saba watakaoteuliwa na Rais baada ya
kupendekezwa na Kamati ya Uteuzi.
(3) Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe wa Tume Huru ya
Uchaguzi watashika madaraka mara baada ya kuapishwa na Rais.
(4) Uteuzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya
Uchaguzi utafanywa kwa misingi kwamba, endapo Mwenyekiti atateuliwa kutoka
upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano, basi Makamu Mwenyekiti atateuliwa
kutoka upande wa pili wa Jamhuri ya Muungano.

Hii ndio tume huru? Akili za Wanasiasa hasa wa CCM sijui zipo wapi aisee
 
Mtu mwenyewe kajizeekea anatembea kama ana nyata..hes 76 i guess..mwache ajifie..hatutaki kijeba kama Shimon Perez

Haaa haa haaaa....Aisee nimekuwa najiuliza several times anatembeaje huyu?? is he such old??
 
huyu polepole ni zaidi ya maintarahamwe wote mule bungeni, nadhani mungu amlinde huyu polepole maana huu mwaka huenda wakamtoa kucha; sisiemu wameamua kusigina maoni ya wananchi
 
Hii sita na wenzake walikuwa wanapoteza muda na kuchezea hela za wananchi tu, sijui Dodoma muda wote walikuwa wanafanya nini maana hata mkijifungia kwenye kaofisi kadogo tu huu UTUMBO wao mnaandika ndani ya siku 10 tu
 
Nimetokea kuwa mfuatiliaji mzuri sana wa makala za bwana Polepole na ongea yake ya Polepole ila uchambuzi wake wa mambo hasa haya ya katiba ni hazina kubwa sana kwa taifa hili.

Watanzania tunajua wao walioko huko wanaandika katiba ya ccm maana katiba ya watanzania tutaindika baada ya uchaguzi mkuu mwakani. Waacha waendelee kupoteza muda na rasilimali za taifa ila wakati unakuja wa kutulipa watanzania na hawatokaa waamini kuwa watanzania waliowaona ni wajinga imekuwaje wakapata akili za kuwakataa wao
 
Tuko nyuma yako Mr G.polepole, nilivyomuona mzee change nimepandwa na ghadhabu sana. Mwizi wa pesa za rader,vijisenti. Ipo siku mungu atamuchoma moto km si kuadhibiwa na wananchi.
 
Kinachonifurahisha kuhusu huu ubatili wooote ni kuwa, ipo siku ubatili utakaa kushoto na kweli itasimama kuume!

Hongera Sitta tumeipata katiba!!
 
Yaan mi kuna wakati huwa nafikiria niwatafute al shabaab ili niwape ajira wakalipue lile bunge la katiba na vyote vilivyomo.
 
Back
Top Bottom