Ras simba tuhurumie

Ras simba tuhurumie

Najua kwa vyovyote una wadau humu kwahiyo watakupa taarifa ama la Pengine hata wewe mwenyewe ni member hapa
Ni wazi kwamba biashara ni matangazo na kwa sehemu kubwa ya matangazo yetu yamejaa uongo usio na uhalisia TUNAVUMILIA...!!!!! lakini uongo wako pls umepita viwango vya kawaida vya kudanganya
Una matangazo kwenye radio za kidini kila asubuhi kwamba kozi yako ya kufundisha kiingereza kwa mfumo wa kipekee inayochukua miezi mitatu ni shilingi laki tano za kitanzania na kama mwanafunzi atakayeshindwa kuongea kiingereza kwa kipindi hicho utamrudishia ada yake yote...!!! Ni ubunifu na ni tangazo zuri lililoteka wengi japo halina uhalisia hata chembe...!!!! Kufaulu ama kufeli kwa mwanafunzi kuna mengi ndani yake

Kero yangu hii hapa
Kama ada ni laki tano lakini katika tangazo lako unasema atakayelipa leo atalipa laki mbili mbili tu!!!! Uhalisia uko wapi hapo? Hiyo ni discount gani isiyoleta mfanano? Tangazo kila siku ni hilo hilo mpaka sasa watu wanajua fika kwamba kusoma lugha ya kiingereza kwako si laki 5 bali ni laki 2...
Sitaki kujadili wafaulu wako kwakuwa ni janga la kipekee lakini pls punguza skonyo kwenye matangazo yako

Sijawahi kukutana na Ras mwenye akili sawasawa katika tembea na maisha yangu yote popote pale nilipokuwa, hivyo sishangai hayo Mazingaombwe ya Kisanii ya huyo Ras Simba wenu.
 
Haa Ras Simba Ni Mjanjamjanja Kama Janjajanja Primary School

Hivi Mh Mnyaa Siku Alipoomba Kura Kwenye Bunge La East Africa Pale Mwisho Alikikoroga Kuliko Hata Ras Simba.

Na Yule Aliyesema Frent Foji
Huyu Habari Zake Zimeizuiliwa Ila Kwanini Mnaziweka Frent Foji
 
Ras simba ndiyo yaani?
image-1.jpeg
 
Mimi nadhani hawa watu wanamaanisha kujua kusalimiana,kutaja ulikotoka au unakokwenda na kununua bidhaa kwa kiingereza ndani ya siku 56!
Labda kama hivyo English huwezi ijua mpaka usome Grammar ili uwe na uwezo wa kuwa competence na sio performance ukawa unaropoka tu bila kuchunga Sheria za Lugha ya watu sasa uyo Ras kwa siku 56 atakufundisha nini kweli mpaka uijue Grammar?
 
Sijawahi kukutana na Ras mwenye akili sawasawa katika tembea na maisha yangu yote popote pale nilipokuwa, hivyo sishangai hayo Mazingaombwe ya Kisanii ya huyo Ras Simba wenu.
Mara nyingi watu kama wewe ndio mnao amini et Rasta ni uhuni. Yakupasa ufungue fikra zako kutoka katika utumwa wa fikra...
 
Haa Ras Simba Ni Mjanjamjanja Kama Janjajanja Primary School

Hivi Mh Mnyaa Siku Alipoomba Kura Kwenye Bunge La East Africa Pale Mwisho Alikikoroga Kuliko Hata Ras Simba.

Na Yule Aliyesema Frent Foji
Huyu Habari Zake Zimeizuiliwa Ila Kwanini Mnaziweka Frent Foji

Hivi aliyesema frent foji ni nani?
 
Back
Top Bottom