Vijana wa Bongo na Ndoto ya Content Creation

Vijana wa Bongo na Ndoto ya Content Creation

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
24,792
Reaction score
60,618
Siku hizi ukikutana na kijana ana laptop, ring light na simu nzuri usidhani ni IT specialist… mwingine anakesha usiku kucha akihariri video ya sekunde 45 huku background kuna motivational music na caption “never give up”.

Lakini ukiangalia reality ya game yenyewe unaweza ukaanza kujiuliza… hivi hawa vijana wanatafuta mafanikio au wanatafuta stress za bure?

Kuna vijana wanatumia muda mwingi kupanga maudhui:
leo prank, kesho podcast, kesho kutwa street interview, mara “day in my life”, mara “nilitumia siku nzima bila kula”.
Views zinaingia, followers wanaongezeka, comments moto… lakini mwisho wa mwezi account inasoma elfu 78.

Meta monetization kwa sasa imekuwa kama bahati nasibu.
Unaweza kuwa na followers laki tano lakini hela inaingia kama nauli ya kwenda Mbezi.
Unakuta content creator ana jina kubwa, anajulikana kila kona, lakini deal anayopata ni kutangaza duka la viatu Sinza, mgahawa Mwenge au perfume za Kariakoo huku akipewa laki mbili na soda mbili za bure.

Wakati huo huo kuna kijana mwingine hata hana Instagram yenye picha tano.
Yupo Manyara huko anachimba, analima vitunguu, viazi, maharage, hoho… msimu ukifika anapiga million 10 kimya kimya bila kujua hata algorithm ni nini.

Mmoja anahangaika:
“Jamani tusaidiane kufikisha views laki moja.”

Mwenzake yupo shambani:
“Mvua ikinyesha wiki hii naongeza ekari mbili.”

Hii haimaanishi content creation haina future. Hapana.
Ila vijana wengi wameingia wakiamini kila mwenye followers ni tajiri. Kumbe wengine wanaishi kwa pressure ya kuonekana wana maisha mazuri kuliko walivyo nayo kweli.


Mwingine anakodisha gari kwa saa mbili apige content ya “hard work pays”.
Lakini mkulima wa nyanya ndio analipa cash gari lote.

Tatizo kubwa ni kwamba vijana wengi wanafuata trend kuliko uhalisia wa maisha.
Kila mtu anataka kuwa influencer, lakini hakuna anayetaka kuwa producer wa chakula ambacho hao influencers wanakula.
Mwisho wa siku unaweza kucheka ukagundua:
Yule anayehangaika kutafuta likes mjini, anaweza kuwa maskini kuliko yule anayehangaika na mbolea kijijini.
 
Ukiwa na Account yenye Followers n.k

Usiangalie tu Malipo ya META ila angalia namna ya kubadilisha followers kuwa clients.

Mfano Niffer umaarufu wake na mafanikio vimechangiwa na mtandao na hao followers.


Sifikirii kama META wanaweza kumlipa MTU pesa inayoweza kumbadilishia maisha .

Ila kampuni pamoja na biashara zinaweza kumlipa

Kuwekeza mtandaoni ni njia sahihi kwa Sasa .

Issue ya kulima vitunguu na kuwa na pesa ni sahihi ila huapaswi kulinganisha watu na kufanya generalization


Kwakuwa kama wanavyofeli content creators as well na wapo wakulima ambao wanafeli.

Ikiwa haupo katika field ya kilimo na haupo katika Field ya content creators hauwezi ukajua uhalisia

Zaidi zaidi utaongea kama motivation speakers.
 
tunajadili reality tu.
Kujaribu ni sawa, ila tatizo ni vijana wengi wanaaminishwa kwamba followers = utajiri automatic. Kumbe wengine wana followers laki 7 lakini hela ya kodi wanaitafuta mwisho wa mwezi.
Kukatishana tamaa, kuwadhihaki na kuwaweka chini wanaojaribu sio poa, na sio kila kitu tunachojaribu lazima tufanikiwe, acha wajaribu wakifeli watakuwa wamejifunza kitu pia ambacho kitafungua opportunity nyingine
 
Sasa vijana wafanye nini. Mbona kila kitu wanasimangwa. Huko kwenye kilimo tuna ndugu, jamaa na marafiki. Maisha wanayoishi tunayaona. Kama kilimo kingekua ukigusa tu kinakulipa tungeona wanavyoinuka. Badala yake wao ndio wanatuomba sisi ambao sio wakulima tuwaboost
 
Siku hizi ukikutana na kijana ana laptop, ring light na simu nzuri usidhani ni IT specialist… mwingine anakesha usiku kucha akihariri video ya sekunde 45 huku background kuna motivational music na caption “never give up”.

Lakini ukiangalia reality ya game yenyewe unaweza ukaanza kujiuliza… hivi hawa vijana wanatafuta mafanikio au wanatafuta stress za bure?

Kuna vijana wanatumia muda mwingi kupanga maudhui:
leo prank, kesho podcast, kesho kutwa street interview, mara “day in my life”, mara “nilitumia siku nzima bila kula”.
Views zinaingia, followers wanaongezeka, comments moto… lakini mwisho wa mwezi account inasoma elfu 78.

Meta monetization kwa sasa imekuwa kama bahati nasibu.
Unaweza kuwa na followers laki tano lakini hela inaingia kama nauli ya kwenda Mbezi.
Unakuta content creator ana jina kubwa, anajulikana kila kona, lakini deal anayopata ni kutangaza duka la viatu Sinza, mgahawa Mwenge au perfume za Kariakoo huku akipewa laki mbili na soda mbili za bure.

Wakati huo huo kuna kijana mwingine hata hana Instagram yenye picha tano.
Yupo Manyara huko anachimba, analima vitunguu, viazi, maharage, hoho… msimu ukifika anapiga million 10 kimya kimya bila kujua hata algorithm ni nini.

Mmoja anahangaika:
“Jamani tusaidiane kufikisha views laki moja.”

Mwenzake yupo shambani:
“Mvua ikinyesha wiki hii naongeza ekari mbili.”

Hii haimaanishi content creation haina future. Hapana.
Ila vijana wengi wameingia wakiamini kila mwenye followers ni tajiri. Kumbe wengine wanaishi kwa pressure ya kuonekana wana maisha mazuri kuliko walivyo nayo kweli.


Mwingine anakodisha gari kwa saa mbili apige content ya “hard work pays”.
Lakini mkulima wa nyanya ndio analipa cash gari lote.

Tatizo kubwa ni kwamba vijana wengi wanafuata trend kuliko uhalisia wa maisha.
Kila mtu anataka kuwa influencer, lakini hakuna anayetaka kuwa producer wa chakula ambacho hao influencers wanakula.
Mwisho wa siku unaweza kucheka ukagundua:
Yule anayehangaika kutafuta likes mjini, anaweza kuwa maskini kuliko yule anayehangaika na mbolea kijijini.
Kwa hiyo unataka kila kijana awe mkulima, sio?
Mbona huelezei shida wanazopata wakulima, mvua chache, mvua kubwa kuharibu mazao, kuwekeza hela nyingi kuliko faida wanayopata au kuambulia hasara
Hakuna sehemu isiyo na changamoto acha kusimanga vijana. Vijana wanajitajidi sana, wanafanya kila kazi unayoijua hapa Tz. Kama mtu anaona atafanikiwa kwa content creation anahitaji support, sio masimango
 
Haujui tu. Ukiwa serious hasa Youtube inalipa sana.
 

Attachments

  • Screenshot_20260518-094041.png
    Screenshot_20260518-094041.png
    86.9 KB · Views: 15
Haujui tu. Na acha kuwakatisha tamaa kwa sababu haujui kitu.


Content inalipa sana hasa Youtube
 

Attachments

  • Screenshot_20260518-094041.png
    Screenshot_20260518-094041.png
    86.9 KB · Views: 16
Ni africa tu ndio wanapatikana.Ulaya mtu anakuonesha anachokifanya.

Niambie mtanzania gani anaweza kutembea dunia nzima akijua maisha ya watu.Wakati hapo kufika tegeta kuna mshinda au mkoani.
Tafuta kijana Youtube anaitwa Explore with Bertin. Hata hajionyeshi sura ila ametembea zaidi ya 25 Afríca
Tena Youtube inamlipa vzr na analipa kodi nzr kuliko wakulima wote wa kijiji chenu. Maana TRA wanachukua 5% ya malipo yao Kila mwezi
 
Ili utoboe uwe na maudhui makhususi sana ... pia uwe famous.. ( uwe na followers wengi ) ili kaz zako ziende mbali upate engagement za kutosha !
Unakuta mtu kAweka video u tube ina miezi minne ana views 56
 
Back
Top Bottom