Rare Pictures From My Personal Album!

Rare Pictures From My Personal Album!

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
3,635
Reaction score
6,535
Ok, I've been going through my 'makabrasha' and I found some few things I'd like to share with the world. Give me few hours as I'm still scanning them, trust me you won't be dissapointed.

Happy New Year.
 
nothing to display yet (its been hours)
 
Just have a little patience, it's been what, 5 minutes? Not hours, come on man.
 
Kuna watu hawakuna na subira naona....anyway, kwa sasa naona ni hizi ninazoweza kuziweka hapa.
 
Hii ni siku mwili mwa Mwalimu Nyerere ulipofika Dar kutoka London, wananchi wakiwa wamejipanga barabarani, tarehe ni October 18, 1999.


93618646.jpg




15405408.jpg
 
Hili ni zao la 'experiment' ya Katibu Mkuu wa Yanga wakati ule George Mpondela, baadhi ya wachezaji hawa walitokea timu ya vijana wadogo ya Yanga, wengine kama Salvatory Edward alitokea moja mwa moja shule ya sekondari ya Kibasila.

Waliosimama kutoka kushoto ni:
Anwar Awath, Mzee Abdallah, Sylvantus Ibrahim, Mahmoud Nyalusi, Salvatory Edward na Peter Louis.

Waliochuchumaa kutoka kushoto ni:
James Tungaraza, Mohammed Hussein, Reuben Mgaza, Vincent Peter na Ally Yusuph 'Tigana'.


76183001.jpg
 
Hii tena ni Yanga, mechi ilikuwa kati ya Yanga na Cadet Club ya Mauritius katika kombe lililokuwa linaitwa 'Africa Cup of Winner Cup', mwaka sikumbuki. Yanga tulishinda 3-1, magoli yaliyofungwa na Mohammed Hussein (goli 1,3) na James Tungaraza (goli la 2). Unaweza kuamini nimekumbana na tiketi ya mechi hii katika takataka zangu?

Waliosimama kutoka kushoto ni:
Team Manager Nurdin Ally, Mahmoud Nyalusi, Keneth Mkapa, Reuben Mgaza, Sylvatus Ibrahim, Ismail Issa, Mathias Mulumba, Vincent Peter, Sadiq Kalokola, Kocha Mkuu Mkongo Tambwe Leya (kwa wasiomfahamu inabidi mtafute historia yake na soka la Tanzania), na kocha msaidizi Mrundi Nzoyisaba Tauzany.

Waliochuchumaa kutoka kushoto ni:
Maalim Saleh, James Tungaraza, Ally Yusuph Tigana', Anwar Awath, Mzee Abdallah, Mohammed Hussein na Bakari Malima.



34598908.jpg
 
Yanga vs. Vaal Professional ya South Africa Uwanja wa Taifa, mwaka sikumbuki. Yanga walishinda 2-1, magoli yaliyofungwa na Benny Luoga na Mohammed Hussein. Wanaomkumbuka Mcongo, Nonda Shaaban, aliyekuja kwenda kucheza kwa mafanikio makubwa huko France ni huyo wa pili kushoto anayefunga viatu (ameishia wapi siku hizi?). Hii timu tena ilikuwa inaundwa na vijana wadogo ukiacha wachezaji wachache sana waliokuwa na uzoefu, mfano Mohammed Hussein.

Kwenye picha kutoka kushoto ni: Anwar Awadh, Nonda Shaaban, Benny Luoga (anayeruka), Sylvatus Ibrahim, Mohammed Hussein (sura imeziba), Maalim Saleh, Kaunda Mwakitope (mkono usoni), kipa Mahmoud Nyalusi, Mzee Abdallah (anafunga kamba za bukta), Peter Louis na Ismail Issa (anayeelekea kuinama).


82339481.jpg
 
Yanga ya msimu wa 1994.


Kutoka kushoto ni:
Joshua Kilale, Ally Yusuph 'Tigana', Willy Mtendawema, Fomu Felician, Keneth Mkapa, James Tungaraza, Suleiman Mkati, Said Mwamba 'Kizota' na Steven Nemes.

Waliochuchumaa kutoka kushoto ni:
Willy Martin, Mohammed Hussein, Nico Bambaga, Jose Ayoub, Sanifu Lazaro, Edibily Lunyamila na Sekilojo Chambua.


93861977.jpg
 
Yanga tena, hii ni uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza wakati wa mashindano ya club za afrika mashariki na kati, mwaka 1995.

Waliosimama kutoka kushoto ni:
Mahmoud Nyalusi, Reuben Mgaza, Nonda Shaaban, Sylvatus Ibrahim, Ally Yusuph 'Tigana', Mcongo Sammy Bitumba Iyela, James Tungaraza na Sadiq Kalokola.

Waliochuchumaa kutoka kushoto ni:
Mzee Abdallah, Bakari Malima, Steven Nyenge, David Mjanja, Mohammed Hussein, Salvatory Edward na Benny Luoga.


96932719.jpg
 
Najua nitawakuna wengi sana kwa hii picha. Hii ndiyo Yanga iliyobatizwa jina la 'Umoja wa Mataifa'. Wazee hawa wangekuwa na marupurupu wanayopata wachezaji wa siku hizi wangefanya maajabu.

Kuanzia kulia kwenda kushoto ni:
Aboubakar Salum 'Sure Boy', John Alex, Thomas Kipese, Justine Mtekere, Said Sued 'Scud', nadhani ni mtoto wa Marehemu Abbas Gulamali, Said Zimbwe, Sanifu Lazaro, Salum Kabunda, Joseph Machela, Godwin Aswile, Athuman China, Issa Athumani, kipa msaidizi Sahau Kambi, kipa Steven Nemes na captain Keneth Mkapa.


33007955.jpg
 
Mtu kapigwa bao hapo. Yanga vs Simba mwaka 1993, uwanja wa taifa. Yanga walishinda 2-1. Magoli ya Yanga yalifungwa na Said Mwamba 'Kizota' na la Simba lilifungwa na Edward Chumila.

Katika picha ni:
Issa Athumani (10), Mtwa Kihwelu (15), Suleiman Mkati, Said Mwamba (14), Edibily Lunyamila (7), Method Mogella (anayeonekana sura tu), Keneth Mkapa (3) na kulia kabisa ndiyo Zamoyoni Mogella (nadhani Zamoyoni ndiyo alikuwa ametokea Simba, enzi hizo ni big deal ku-cross over katika timu mbili hizo).


67924183.jpg
 
Nadhani hizi zitatosha kuwavusha mwaka, tutaonana 2010, inshallah Mungu akipenda.
 
Nadhani hizi zitatosha kuwavusha mwaka, tutaonana 2010, inshallah Mungu akipenda.

Kwanza nianze kwa kukushukuru kutuwekea ukumbusho wa picha mbalimbali.

Pili, nashauri kama unaweza uziweke picha zote original katika file moja la zip na kupost hapa. Itafaa kama utaweka maelezo kama ulivyojitahidi hapo juu kwenye file la text na kuzip pamoja na picha. Kingine ni kwamba, size ya picha ni kubwa sana (jambo ambalo ni zuri), ila namna ya kuziangalia hapa jukwaani ni shida.. kama inawezekana ungeziweka zote katika size moja na kutubandikia... (najua quality inaweza kufifia lakini sidhani kama itakuwa kubwa kiasi cha kutoweza kuvumilika, na kama original zinakuwepo kwenye zip, basi hilo wala halitajalisha kabisa).

SteveD.
 
Kwanza nianze kwa kukushukuru kutuwekea ukumbusho wa picha mbalimbali.

Pili, nashauri kama unaweza uziweke picha zote original katika file moja la zip na kupost hapa. Itafaa kama utaweka maelezo kama ulivyojitahidi hapo juu kwenye file la text na kuzip pamoja na picha. Kingine ni kwamba, size ya picha ni kubwa sana (jambo ambalo ni zuri), ila namna ya kuziangalia hapa jukwaani ni shida.. kama inawezekana ungeziweka zote katika size moja na kutubandikia... (najua quality inaweza kufifia lakini sidhani kama itakuwa kubwa kiasi cha kutoweza kuvumilika, na kama original zinakuwepo kwenye zip, basi hilo wala halitajalisha kabisa).

SteveD.


Ok hamna tatizo, nitaifanya hiyo kazi kesho nikipata nafasi, nilijua picha zimekuwa kubwa lakini nilikuwa nataka kumalizana tu na ile shughuli niendelee na mambo mengine.
 
Ukumbusho mzuri kweli asante sana japo asilimia kubwa wengine bado tulikuwa hatuja ingia duniani!!
 
Ukumbusho mzuri kweli asante sana japo asilimia kubwa wengine bado tulikuwa hatuja ingia duniani!!

You are right my dear,picha nyingi hapa ni enzi hizoooo. Hizo picha za msiba wa Nyerere ndio nazikumbuka maana hapo nilikuwa atleast mkubwa, nilikuwa form 1.
 
at last kaka, asante...nimezipenda vipi naweza kukopi na kuanzishia thread??
 
Back
Top Bottom