Rais wa wanyonge, wanyonge wapi?

Rais wa wanyonge, wanyonge wapi?

Halafu viongozi wetu hata awamu iliyopita wanapenda kutumia maneno ya kusema wananchi 'Masikini, wanyonge, dhaifu, au sisi ni taifa masikini sijui na nini lakini wanashindwa kujua hata kama kuna ukweli lakini wanatuumbia tu hizo hali na sisi tunajiona wanyonge na dhaifu

Kuna maneno mengi tu ya kupeana moyo, ushujaa, kutokukata tamaa na kuonyesha kama kesho yetu ipo nzuri zaidi kama Taifa kila mtu akitimiza wajibu wake

Namtambua mtoa mada hakulenga huku ila nimeona tu hii nayo changamoto ktk hotuba za viongozi wetu kutangaza umasikini na udhaifu wa wananchi hata kama upo sio sawa na badala yake waanze kutujenga ktk kuwa chanya na kesho yetu 'will be better than today'
 
Hizi kwangu mimi naziona kama ghiliba,kama kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa!

Kutuita watanzania wanyonge watanzania masikini ni kutukejeli! Watanzania sio wanyonge bali ni wavumilivu na watu tunaoheshimiana.

Tunakutaka usituite wanyonge,huku ukitubomolea makazi yetu tena kwa kukiuka agizo la mahakama.

Unatuita wanyonge huku ukikataa kutuletea katiba mpya itakayo wawajibisha wapindisha haki na mafisadi wote wa serikali yako!

Unatuita wanyonge huku ukituingiza kwenye hasara kubwa kwa kukiuka naagizo ya mahakama.

Unatuita wanyonge huku ukitupiga danadana kuwaongeza mshahara wafanyakazi

Unatuita wanyonge huku ukiruhusu makampuni yapoteze ajira kwa watu wako kwa kushindwa kujiendesha

Hili jina la Watanzania wanyonge tunaona linatumika kujinufaisha kwa baadhi ya viongozi kujiona miungu watu. Tunaomba likome

NDIO MIMI NI MBOVU WA MGUU LAKINI SIKO TAYARI KUITWA KILEMA
Asante mkuu kwa kuwakilisha,hata Mimi ningependa kujua sifa zinazotumiwa na rais kuwàjua hao watanzania wanyonge ili nàmi nijipime kama nipo kwenye hilo kundi la wanyonge ama laa
 
Okwo ,leo hutaki kuitwa mnyonge? Hujawai kunyongwa ww? Au neno mnyonge ngumu? Kwa kingereza mnyonge means what labda tuanzie apo kuelewa.
 
Watanzania wavumilivu/wajinga/waoga..Ona enya watu wanajua haki zao.Huwezi waita wanyonge wakuache salama
 
Kama wewe ni maskini unategemea uitweje ili usionewe? Uitwe tajiri? Hata Tanzania inaitwa maskini na nchi tajiri akiwemo huyo magufuri,
Sijui kama maskini ni tusi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ile billion 90 Alisha lipa. Au bombandier ndo ishapigwa mnada
 
Yaani kwwny hizi comments za watu ndonimeamini watanzania bado sana ndomana tunaonewa kila kukicha,,tukidai haki zetu tunakandamizwa,,,yan mtu anatoa mtazamo wake sisi sio wanyonge bali wavumilivu na wastaarab lakin cha ajab mijinga humu ndani inamshambuliaa kama akina kanyinya upuuzi mtupuu

Ni miMi CHalIIiiii Ya "R"
Fact

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza ni hatari sana mtu kuitwa mnyonge na maskini na we we unayeitwa hivyo ukawa unachekelea.(maana yake ni kuwa unaukubali unyonge na umaskini hivyo itakuwa ngumu sana kutoka hapo)
Pia sijawahi kumsikia rais akiwaongelea kwa wema matajiri,yeye kila tajiri kwake ni fisadi,na bahati mbaya sana hao anaowaita maskini na wanyonge wanaamini hivyo hivyo kama kiongozi wao anavyo amini jambo ambalo si kweli.
Tuukatae maskini na unyonge kwa nguvu zote sababu unyonge na umaskini si utakatifu
Anawapigania wanyonge ili iweje wakati waliofanikiwa anasema hawataki. Nadhani anawapenda wanyonge kama mapenzi yake sio anataka wafanikiwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo mnyonge ikizoeleka Kinachofuata ni mnyongeni
 
utaitwaje mnyonge wewe wakati mlibadilishia gia angani kwa nguvu ya 'rasilimali' ya kukwepe umasikini kibinafsi!!! wewe si mnyonge!!
 
Mheshimiwa Rais wa JMT mara nyingi umesema wewe ni Rais wa wanyonge sasa sijui wanyonge ni wapi?
1.Ni hawa Mamantilie wanaouza chakula walio fukuzwa Stand Kuu ya mabasi ya Mkoa wa Pwani Kibaha mjini wanaotangatanga hawana uhakika hata wa mlo mmoja ??????
2.Ni hawa Babantilie wanao uza chakula USIKU walio fukuzwa Stand Kuu ya mabasi ya Mkoa wa Pwani Kibaha mjini wanaotangatanga hawana uhakika hata wa kutunza mke kwa siku moja na wengi wao sasa wametengana na familia zao zimeludi vijijini hawana uhakika tena wakuwa na ukaribu na familia zao??????
3.Ni hawa wahanga wa Bomoabomoa wa Kimara wanao lala inje huku hawajui kesho yao ?
4.Ni hawa wakulima ulio watangazia Neema ya Viwanda na sasa Mazao hayana pa kwenda juzi nilikuwa Lindi Luangwa nimenunua mbaazi Kilo 100 kwa Shilling 8,000 kilo moja ni sawa na shiling 80????


WALALA HOI WA INCHI HII NI WAPI ???

HALI NI MBAYA SANA TUNAKOELEKEA KAMA TAIFA HUKO MBELE HALI SI SHWALI NATUMAI MUDA MCHACHE VIJANA KWA WAZEE WATAANZA KUZAMIA TUJITAFAKARI.
 
Back
Top Bottom