Rais wa wanyonge, wanyonge wapi?

Rais wa wanyonge, wanyonge wapi?

Hujielewi wewe
Usijiangalie wewe angalia vizazi vijavyo vitanufaika vipi? Kauli kama ya kwako mara nyingi hutolewa na watu wanaolazimisha kila mtu afanane naye. Mfano yawezekana huna uwezo biologically wa kupata watoto kwa hiyo unasupport ujinga kwa kuwa unajua hakuna mnufaika wako mbeleni. Tofauti na son biologically unaweza hata mnunua mtoto katika vituo then akaja nufaika na Katiba kama ya Kenya people wangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizi kwangu mimi naziona kama ghiliba,kama kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa!

Kutuita watanzania wanyonge watanzania masikini ni kutukejeli! Watanzania sio wanyonge bali ni wavumilivu na watu tunaoheshimiana.

Tunakutaka usituite wanyonge,huku ukitubomolea makazi yetu tena kwa kukiuka agizo la mahakama.

Unatuita wanyonge huku ukikataa kutuletea katiba mpya itakayo wawajibisha wapindisha haki na mafisadi wote wa serikali yako!

Unatuita wanyonge huku ukituingiza kwenye hasara kubwa kwa kukiuka naagizo ya mahakama.

Unatuita wanyonge huku ukitupiga danadana kuwaongeza mshahara wafanyakazi

Unatuita wanyonge huku ukiruhusu makampuni yapoteze ajira kwa watu wako kwa kushindwa kujiendesha

Hili jina la Watanzania wanyonge tunaona linatumika kujinufaisha kwa baadhi ya viongozi kujiona miungu watu. Tunaomba likome

NDIO MIMI NI MBOVU WA MGUU LAKINI SIKO TAYARI KUITWA KILEMA
Unavumilia nini Sasa....ndiyo maana mnyonge!

Rais yuko sawa watanzania ni wanyonge.

Kama wewe siyo unyonyesha kuwa wewe si mnyonge Sasa.

Wakenya wanakushinda hapo halafu unamzuia Rais asikuite mnyonge wewe ni mnyonge tu na utaendelea kuwa mnyonge tu maana hujitambui.
 
Hivi kwa mtu ambaye anayejua hali ya nchi ilivyo kiuchumi ni Kiongozi gani atakayekubali kupewa amri ya kwenda kuvunja nyumba za watu huku akijua maisha halisi ya huyo anayemvunjia.

Hizi dhambi hatutaziona leo kwani Hitla hakuwa na Familia kwani hiyo familia yake iko wapi isiyosikika na dunia kila kitu huwa kinakuja na majibu yake na hayo majibu yanaweza yakawa mazuri au mabaya.

Kwa hiyo tujitahidi kutenda kwa haki tusitende kwa ubaya kwa kuwa sasa hivi tupo ktk uongozi na huyu Kiongozi akumbuke uongozi ni kitu cha kupita kwa hiyo mtu ambaye anatenda kwa haki ni hazina ktk jamii.

Ndugu viburi jeuri havijawahigi kumnyanyua mtu kutoka sehemu fulani kwenda nzuri kimaisha zaidi Sana huishia ktk matatizo ambayo hayatampa muhusika majibu zaidi ya kujengewa chuki ktk jamii inayomzunguka na ni mtu yupo aliyewahi kuchukiwa na jamii inayomzunguka akabaki salama.

Tukumbuke Kiongozi hubarikiwa kutokana na matendo yake hasa ya kutatua matatizo waliyonayo raia wake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani dhambi kuwa Chadema?
Mku usimuhukumu mtu kwa itikadi kwani itikadi ni imani iliyo kamili kama zilivyo imani zingine.
Tenda kwa haki ili atakayekukosoa jamii imshangae anayekukosoa kwa kuwa unatenda kwa haki.
Kumbuka matendo ni mwonekano unaoonekana na wengi na ukiona waliowengi wanakupinga ujue kuna mahali umekosea na kukosea kwa mtu ni sehemu ya kujifunza lakini sio vizuri ukawa unaonekana kutokujifunza kutokana na mazingira hapo hutakosa upingwaji kutoka kwa jamii husika.
Mku itikadi ni kuvumiliana sio kuogopana na kuogopana ni sehemu ya kuigawa jamii kwani itikadi isitugawe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama we una mitonyo ucfikir wote, wengne bila kushika jembe hawajala tena kwa mvua za mcmu
Na hao si wanyonge.
Watu ambao wamepewa Mamlaka za KUPIGA KURA KUCHAGUA VIONGOZ SI WANYONGE.
Ila wenyewe wamekariri kuwa wao ni WANYONGE.Wao ndo mabosi

May Allah bless Me and You
 
Ajira kwa wadogo zetu waliohitimu vyuo zimekua kizungumkuti afu anawaita wanyonge.
 
Kwanza ni hatari sana mtu kuitwa mnyonge na maskini na we we unayeitwa hivyo ukawa unachekelea.(maana yake ni kuwa unaukubali unyonge na umaskini hivyo itakuwa ngumu sana kutoka hapo)
Pia sijawahi kumsikia rais akiwaongelea kwa wema matajiri,yeye kila tajiri kwake ni fisadi,na bahati mbaya sana hao anaowaita maskini na wanyonge wanaamini hivyo hivyo kama kiongozi wao anavyo amini jambo ambalo si kweli.
Tuukatae maskini na unyonge kwa nguvu zote sababu unyonge na umaskini si utakatifu
 
Back
Top Bottom