Unyonge wa watanzania anausababisha yeye
Utawala wa sheria ndio dawa ya unyonge,kwa maana kila mtu anakuwa sawa mbele ya sheria,mkiwa sawa mbele ya sheria,masikini na tajiri wote wanasikilizwa bila kujali hali zao,serikali na mwananchi wote wanasikilizwa kwa usawa bila kujali hali zao(serikali ina mapesa,mabomu,bunduki)mfanyakazi na mwajiri wakiwa mbele ya sheria wote ni sawa muajiri huwezi,kwa ubabe tu,kukataa ongezeko la mishahara
Serikali na wamiliki wa majengo,wanapokuwa mbele ya sheria,wanakuwa sawa, hakuna mmoja mnyonge na mwingine mbabe,serikali ikipokea amri za mahakama inatakiwa izitekeleze,ikizuiwa kufanya jambo na mahakama,basi,iache,na tena iwe mfano kwa wananchi kwa jinsi inavyotekeleza maagizo ya mahakama,badala yake,serikali ndiyo inkataa kutekeleza amri za mahakama kuzuia bomoa bomoa na inatumia nguvu za jeshi,katika hali hii mwananchi ataacha kuwa mnyonge mbele ya mbabe serikali?
Nani asiyejua kwamba mahakama haina jinsi ya kutekeleza amri zake na badala yake wanaitegemea serikali? Hakimu/Jaji huandika karatasi kuitaka serikali isifanye,basi,inaishia hapo, je serikali ikienda kufanya jambo,mfano bomoa bomoa ikiwa na FFU mamia kwenye magari,je JAJI/HAKIMU au mahakama,wao watolee wapi jeshi la kwenda kupambana na hao Tanroad(serikali) pamoja na FFU?
Unyonge utaishaje wakati anayeuhubiri ndiye chanzo cha tatizo?
Unyonge utaishaje wakati unazuia Uhuru wa majadiliano na watu wanaishi kwa hofu,badala yake umeruhusu ubabe wa ccm na Polisi ,sasa ccm wako juu ya sheria pamoja na polisi,wanakamata watu hovyo,utarajie watu hawa wasiwe wanyonge?
Uendeshaji wa bunge unatarajia usiwafanye wapinzani wasiwe wanyonge?
Uonevu wa mahakama,na Taasisi za Tanganyika dhidi ya CUF unatarajia utawafanya wazanzibari wasiwe wanyonge?
Unyanyasaji wa wafanyabiashara unatarajia uwafanye wasiwe wanyonge?