Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 2,208
- 4,705
Rais wa Ufaransa Emanuel Macron amuandikia Barua kumpongeza Rais Magufuli kwa kuiwezesha Tanzania kuingia Uchumi wa kati miaka mitano kabla ya muda uliopangwa
Serikali imesema katika kipindi cha pili cha awamu ya pili ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli itajikita zaidi katika kuboresha uwekezaji wa ndani na nje ya nchi na kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika kujenga uchumi wa nchi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ameyasema hayo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Ufaransa hapa Nchini na kuongeza kuwa baada ya kipindi cha kwanza cha miaka mitano ya uongozi wa Rais Dkt John Pombe Magufuli kujikita katika uwekezaji mkubwa wa maeneo ya miundombinu na nishati pamoja na huduma za kijamii sasa serikali inalenga kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika ujenzi wa uchumi.
Balozi wa Ufaransa hapa Nchini Mhe. Frederic Clavier amemkabidhi Prof Kabudi barua ya iliyoandikwa na Rais wa Ufaransa Mhe Emmanuel Macron kwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kumpongeza kwa kuiwezesha Tanzania kuingia katika uchumi wa kati ikiwa ni miaka mitano kabla ya muda uliopangwa.
Serikali imesema katika kipindi cha pili cha awamu ya pili ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli itajikita zaidi katika kuboresha uwekezaji wa ndani na nje ya nchi na kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika kujenga uchumi wa nchi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ameyasema hayo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Ufaransa hapa Nchini na kuongeza kuwa baada ya kipindi cha kwanza cha miaka mitano ya uongozi wa Rais Dkt John Pombe Magufuli kujikita katika uwekezaji mkubwa wa maeneo ya miundombinu na nishati pamoja na huduma za kijamii sasa serikali inalenga kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika ujenzi wa uchumi.
Balozi wa Ufaransa hapa Nchini Mhe. Frederic Clavier amemkabidhi Prof Kabudi barua ya iliyoandikwa na Rais wa Ufaransa Mhe Emmanuel Macron kwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kumpongeza kwa kuiwezesha Tanzania kuingia katika uchumi wa kati ikiwa ni miaka mitano kabla ya muda uliopangwa.