Rais wa TLS: Tumezungumza mengi na Rais Samia

Rais wa TLS: Tumezungumza mengi na Rais Samia

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Boniface Mwabukusi, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma.
 
20250827_210242.jpg
 
sehemu ya mkakati wa pre-campain???
 
Leo Nimefika Ikulu CHAMWINO kuwasilisha Majumuisho ya wadau na tulipata nafasi ya kuzungumza na Kumueleza Mh.Rais wa Jamuhuri ya Muungano kuhusu Utawala Bora,Haki za kushiriki katika chaguzi za kidemokrasia, Masuala ya Utekwaji na enforeced Disappearance , Kuhusu Umuhimu wa kuwa na chaguzi zinazozingatia haki za wananchi kupata,Watu na wagombea kutokuondolewa kwa kukatwa kwa masuala ya kiufubdi na Maeneo yenye kuhitaji maboresho ili kuwa na uchaguzi mzuri ulio Huru na wa Haki ili kuoata viongozi wanao wataka kupitia sanduku la kura.

Mh.Rais Ametusikiliza na kuahidi kuangalia namna bora ya Kufanya kwamambo yatakayowezekana kwa muda uliopo na kuboresha ili kuwa na Uchaguzi huru na Haki na kuondoa kadhia ya kutoa wagombea kwasababu za kiufundi.

Aidha kwa kuwa kulikuwa na Mapendekezo ya Muda mfupi,Muda wa kati na Muda mrefu ameahidi kuyapitia yote na kuona namna bora ya kuyatekeleza.

BAK Mwabukusi.
 
Amekula vitafunwa vya ikulu akapata tabasamu la kuonesha katika TV.

Ile nyumba nyeupe ukiingia na kutoka unakuwa na tabasamu na kucheka hata kwa vitu visivyo chekesha.

Anaulizwa walichoongea, anajibu tumeongea mengi. Kila mtu anatafuta mrija kwa namna yake
 
Makelele yote kumbe Mwabukusi nae anabei.

CDM wanapenda kuwa promote watu kirahisi sana ambao hawana track record ya uzalendo.

Haya kiko wapi, hata huyo Lissu keshasahau kama anasota ‘death row’, hayo ya reforms kabla ya uchaguzi ndio kabisa hayapo kwenye kichwa cha Mwabukusi.

Yeye anahimiza watu wajitokeze kupiga kura siku ya uchaguzi.

Kaazi kweli kweli hawa wanaharakati uchwara. Halafu uso wake anavyoongea umejawa na bashasha lazima kalamba dau nono safari hii.
 
Leo Nimefika Ikulu CHAMWINO kuwasilisha Majumuisho ya wadau na tulipata nafasi ya kuzungumza na Kumueleza Mh.Rais wa Jamuhuri ya Muungano kuhusu Utawala Bora,Haki za kushiriki katika chaguzi za kidemokrasia, Masuala ya Utekwaji na enforeced Disappearance , Kuhusu Umuhimu wa kuwa na chaguzi zinazozingatia haki za wananchi kupata,Watu na wagombea kutokuondolewa kwa kukatwa kwa masuala ya kiufubdi na Maeneo yenye kuhitaji maboresho ili kuwa na uchaguzi mzuri ulio Huru na wa Haki ili kuoata viongozi wanao wataka kupitia sanduku la kura.

Mh.Rais Ametusikiliza na kuahidi kuangalia namna bora ya Kufanya kwamambo yatakayowezekana kwa muda uliopo na kuboresha ili kuwa na Uchaguzi huru na Haki na kuondoa kadhia ya kutoa wagombea kwasababu za kiufundi.

Aidha kwa kuwa kulikuwa na Mapendekezo ya Muda mfupi,Muda wa kati na Muda mrefu ameahidi kuyapitia yote na kuona namna bora ya kuyatekeleza.

BAK Mwabukusi.
Alafu mie eti niandamane. Alafu eti yule wa USA aniambie mie wa TZ niandamane. Alafu eti yule wa Arusha aliekimbiza familiar yake Canada anidanganye mie niandamane. Alafu eti yule mwenye mke na watoto wake wapo Ubelgiji waniambie mimi niandamane. Alafu eti yule Wanairobi ambaye hata mazishi ya baba yake aliyefariki bongo hakuhudhuria maziko aniambie mie niandamane. Arafu eti yule Mchungaji aliyetuambia sisi wa Kawe tutapelekwa Birmingham aniambie niandamane. Arafu eti yule balozi aliyeshiriki kuwanunua akina Katambi, Gekuru wa Babati, Nasari, Dr Mashinji, Dr Molel, Mtolea, Mtatiro leo aniambie niandamane. La hasha abadan sijaingia mtego huo.
 
Alafu mie eti niandamane. Alafu eti yule wa USA aniambie mie wa TZ niandamane. Alafu eti yule wa Arusha aliekimbiza familiar yake Canada anidanganye mie niandamane. Alafu eti yule mwenye mke na watoto wake wapo Ubelgiji waniambie mimi niandamane. Alafu eti yule Wanairobi ambaye hata mazishi ya baba yake aliyefariki bongo hakuhudhuria maziko aniambie mie niandamane. Arafu eti yule Mchungaji aliyetuambia sisi wa Kawe tutapelekwa Birmingham aniambie niandamane. Arafu eti yule balozi aliyeshiriki kuwanunua akina Katambi, Gekuru wa Babati, Nasari, Dr Mashinji, Dr Molel, Mtolea, Mtatiro leo aniambie niandamane. La hasha abadan sijaingia mtego huo.

View: https://www.instagram.com/p/DN3lqNpUGRE/?igsh=MTR2ajBvMzk4dTRrdA==
 
TLS KUMUUNGA MKONO RAIS SAMIA - ASEMA ADV. MWABUKUSI

Rais wa Chama Cha Wanasheria wa Tanganyika ( TLS) Wakili Boniface Mwabukusi leo amekutana na kuzungumza na Rais Samia Ikulu, Chamwino Dodoma.

Mara baada ya kikao hicho Wakili Mwabukusi akizungumza na waandishi wa habari katika viwanja vya Ikulu amesema, hoja zao zote walizomuwasilishia Rais Samia amezipokea vizuri na kwamba atazifanyia kazi.

Mwabukusi ambaye aliongea kwa bashasha ameongeza kuwa wao kama TLS wanamuunga mkono Rais Samia kwani ni kiongozi msikivu ambaye ametumia muda mrefu wa zaidi ya masaa 3 kuwasikiliza na kuwapa majawabu ya baadhi ya hoja zao huku nyinginezo zikiendelea kufanyiwa kazi.
 
Back
Top Bottom