"Rais wa misiba"

"Rais wa misiba"

Kijana ni nani?unanijua?fanya kazi wewe ndugu,usipoteze muda kupiga porojo.Rais huyu ndo tuliwahi kimtaka ktk nchi hii.sasa hv mnapiga kelele za nini?ni kweli maisha ni magumu sote tunajua lakini ni lini maisha yaliwahi kua rahisi toka dunia imeumbwa?miaka yote kuko hivi hivi.nyamaza bwana na ufanye kazi
Usiwe mbinafsi kiasi hiki kijana kuwa na upendo na Jirani zako,ninachokiongea Mimi ni kile ninachokiona na kukisikia,sicho kinachonipata Mimi Bali kina wapata wengine,Mimi na feel maumivu yao kwasababu ni wanadam wenzangu! Mtu mzima aliyebakiza miaka miwili kustaafu amelitumikia taifa hili kwa miaka Yake yote Leo hii anaambiwa ameliibia taifa kwa sababu hana cheti,niambie uchungu anaoupata mzee huyu je atakuwa na upendo kutoka moyoni kwa kiongozi wake?

Wana Kagera walipatwa na majanga,kauli ya kwanza kutoka kwa kiongozi wao ni wafanye kazi wajenge miundo mbinu na nyumba zao kwasababu tetemeko halijaletwa na serikali,michango ya kuwasaidia mkaipeleka kwenye ujenzi wa miundombinu ya serikali wao kama wananchi wakaachwa walalie majani ya migomba.
Upendo wa mwanadam huyu kwa kiongozi wake utatoka wapi? Kijana jitahidi kulichukulia hili jambo liwe kama limekupata wewe.

Tumuogope Mungu,unafiki kitu kibaya sana palipo na ukweli ongea ukweli ila iwe ni kweli kutoka moyoni.

Manung'uniko yao ndio ishara ya kukata tamaa na kiongozi wao.
 
Kijana ni nani?unanijua?fanya kazi wewe ndugu,usipoteze muda kupiga porojo.Rais huyu ndo tuliwahi kimtaka ktk nchi hii.sasa hv mnapiga kelele za nini?ni kweli maisha ni magumu sote tunajua lakini ni lini maisha yaliwahi kua rahisi toka dunia imeumbwa?miaka yote kuko hivi hivi.nyamaza bwana na ufanye kazi
Hawezi kunyamaza labda wewe uende kijijini ndiyo utajua level ya huyo unayemt.t.a. wanavijiji hatujahawahi kuchoka mapema kiasi hiki halafu tunaowategemea wameachishwa kazi ghafla hata bila kufuata kanunu za kazi
 
Usiwe mbinafsi kiasi hiki kijana kuwa na upendo na Jirani zako,ninachokiongea Mimi ni kile ninachokiona na kukisikia,sicho kinachonipata Mimi Bali kina wapata wengine,Mimi na feel maumivu yao kwasababu ni wanadam wenzangu! Mtu mzima aliyebakiza miaka miwili kustaafu amelitumikia taifa hili kwa miaka Yake yote Leo hii anaambiwa ameliibia taifa kwa sababu hana cheti,niambie uchungu anaoupata mzee huyu je atakuwa na upendo kutoka moyoni kwa kiongozi wake?

Wana Kagera walipatwa na majanga,kauli ya kwanza kutoka kwa kiongozi wao ni wafanye kazi wajenge miundo mbinu na nyumba zao kwasababu tetemeko halijaletwa na serikali,michango ya kuwasaidia mkaipeleka kwenye ujenzi wa miundombinu ya serikali wao kama wananchi wakaachwa walalie majani ya migomba.
Upendo wa mwanadam huyu kwa kiongozi wake utatoka wapi? Kijana jitahidi kulichukulia hili jambo liwe kama limekupata wewe.

Tumuogope Mungu,unafiki kitu kibaya sana palipo na ukweli ongea ukweli ila iwe ni kweli kutoka moyoni.

Manung'uniko yao ndio ishara ya kukata tamaa na kiongozi wao.
siyo hilo tu ndugu yangu fikiri kumwachisha mtu kazi Ghafla aliyekuwa kazini kwa miaka 32 bado mmoja astaafu hii siyo haki, kwa sababu alikuwepo hapo kihalali na serikali iliyopita ilimtambua wewe uko tofauti gani na huyo aliye mwajiri na kufurahia matunda ya kazi yake? Jamani twende mbele na kurudi, wakuhukumiwa siyo huyu mlalahoi ni wale waliompokea ili asaidie kuliendesha gurudumu la nchi hii.(
 
Binadamu ni kiumbe changamani sana.

Huo ni ukweli ulio dhahiri ambao wala hauhitaji mtu uwe na 'kipaji maalumu' kuuona.

Hata iweje, binadamu kamwe huwa haridhiki.

Kwa kifupi, ni ndivyo tulivyo!

Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu ya yaliyotokea huko Arusha wiki ilopita na kuagwa kwa waliopoteza maisha yao kwenye hiyo ajali mapema leo hii.

Kama ilivyodhaniwa/ ilivyotarajiwa, rais Magufuli hakuwepo kwenye hiyo shughuli.

Hii si mara yake ya kwanza yeye kukosa shughuli kama hii ya leo tangia awe rais.

Watu wengi sana wanamlaumu kwa kukosekana kwake. Kwangu hizo ni lawama halali kabisa.

Naamini ingekuwa ni vyema yeye mwenyewe kuwepo kuliko kutuma mwakilishi.

Sababu za yeye kutokwenda mimi sizijui na wala sitajaribu kuanza kusadiki ni nini kilichomfanya asiende.

Ila pia bado sijasahau kipindi ambapo Jakaya Kikwete alikuwa rais na watu wengi tu [hususan humu JF] walikuwa wakimbeza kuwa eti anapenda sana kwenda misibani kuuza sura kuliko kufanya kazi.

Kuna watu walimbatiza hadi jina kuwa eti ni "rais wa misiba". Na simzushii mtu...bofya hapa usome mwenyewe!

Kikwete alibezwa, akachekwa, akaitwa kila aina ya majina kutokana na kupenda kwake kuhudhuria misiba hata ya watu wa kawaida tu wasio maarufu.

Kuna wengine walidai eti anaweka 'precedent' mbaya na kwamba eti watu watakuwa wanategemea kumwona 'rais' kwenye kila msiba utokeao.

Sasa huyu Ngosha yeye yuko tofauti. Anaonekana si mtu wa kupenda kujichanganya changanya sana na watu.

Misiba mingi tu itatokea katika utawala wake maana huo ndo uhalisia wa maisha. Watu hufa kila siku kwa sababu anuai.

Labda yeye hataki kujenga matarajio kwa watu kuwa kila msiba utokeao na yeye lazima atawepo maana vifo ni vingi mno na ukienda kwenye kifo cha huyu au vifo vya hawa basi kila afapo mtu au wafapo watu, basi na wewe lazima uwepo.

Vyovyote vile, urais ni kazi ngumu sana. Ni kazi ambayo kwa kiasi kikubwa haina shukurani.

Ufanye hili, utalaumiwa na kulaaniwa. Usifanye lile, utalaumiwa na kulaaniwa.

Chochote ufanyacho na chochote usichokifanya, ni lawama na shutuma tu.

Wakati mwingine huwa hata sielewi kwa nini watu huwa wanapenda kuwa marais......
we jamaa ni jobless? hauko busy? unatumia muda na rasilimali bundle kuandika upuuzi
 
siyo hilo tu ndugu yangu fikiri kumwachisha mtu kazi Ghafla aliyekuwa kazini kwa miaka 32 bado mmoja astaafu hii siyo haki, kwa sababu alikuwepo hapo kihalali na serikali iliyopita ilimtambua wewe uko tofauti gani na huyo aliye mwajiri na kufurahia matunda ya kazi yake? Jamani twende mbele na kurudi, wakuhukumiwa siyo huyu mlalahoi ni wale waliompokea ili asaidie kuliendesha gurudumu la nchi hii.(
Asante mkuu kwa kunielewa,Mungu akubariki sana.
 
Alichokifanya mh rais siwezi laumu hata siku moja,wewe mwenyewe nyani ngabu umekiri urais ni mzigo mimi nasema hata sio urais tu tizama tu hata kwa ngazi za kifamilia yaani unaweza fanya jambo ukaishia kupewa lawama tu.

Wewe mwenyewe umekua shahidi hapa wengine wanasema kakosea kutohudhuria, wengine bora hajenda angeleta tafurani, yaani mitanzania tu wanafiki nafikiri tunaongoza, mimi naona aende, asiende poa tu kuongoza watu wa hivi nikujipa stress tu maana hatuishiwi maneno jamani.
Nilikua na mpenda kikwete naninampenda Magufuli kuongoza binadamu si mchezo bwana.
 
413013-155fe61155a5fed6e2a5cfb2e408356e.jpg
 

Attachments

  • 18380766_896346160506681_8488051894655123456_n.jpg
    18380766_896346160506681_8488051894655123456_n.jpg
    54 KB · Views: 29
Alichokifanya mh rais siwezi laumu hata siku moja,wewe mwenyewe nyani ngabu umekiri urais ni mzigo mimi nasema hata sio urais tu tizama tu hata kwa ngazi za kifamilia yaani unaweza fanya jambo ukaishia kupewa lawama tu.

Wewe mwenyewe umekua shahidi hapa wengine wanasema kakosea kutohudhuria, wengine bora hajenda angeleta tafurani, yaani mitanzania tu wanafiki nafikiri tunaongoza, mimi naona aende, asiende poa tu kuongoza watu wa hivi nikujipa stress tu maana hatuishiwi maneno jamani.
Nilikua na mpenda kikwete naninampenda Magufuli kuongoza binadamu si mchezo bwana.
Walau wewe naona umekuwa mkweli.

Yaani hata angefanyaje bado angelaumiwa tu.

He is damned if he does and damned if he doesn't.

It's just the nature of the beast.
 
Uzuri wa Rais Magufuli ni mtu ambaye ana misimamo isiyoyumba.

Ni kweli misimamo yake mingine iko kinyume na matarajio ya kisiasa lakini kwa Tanzania ya leo hii misimamo inahitajika sana.

Rais Magufuli amejifunza kwa yaliyotokea kwa Mzee Kikwete wakati akiwa Rais.

Mpaka pale wakosoaji wake watakapofahamu kuwa Rais Magufuli is the opposite of Rais Kikwete ndipo watakapogundua kuwa wanachokifanya ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.
aibu sana halafu akaingia twita akasema anauchungu sana hahaha kwahiyo msiba aliangalilia kwenye tv????????


my foots there is something wrong pahali iko taabu wala msijitie kusema ni msimamo .......... aliona la maana kwenda kwa masaburi kutangaza wake na watoto lakini hawa malaika aaah!!!!!!!
msimamo................. doooooooooooo,
mnaomshabikia huyu mtu mna walakini naninyi, kikombe cha loliondo kirudi mkimeze tena labda mtapona
 
Wenzetu wanasemaje kuhusu kiongozi wao kuhudhuria "tragedies" ....

'Symbol of the country'


Ahead of Thursday's trip, White House press secretary Josh Earnest said the president sees these condolence trips as a solemn responsibility: "The president understands that he is a symbol of the country, and when he travels to a community and meets with a family that has endured a terrible tragedy, he's offering a message of condolence and comfort on behalf of the American people."

"When these kinds of events occur," Rottinghaus said in an interview, "the public really does look to the president as a true national healer, and somebody who can make sense of the situation, but who can also lend a shoulder to be able to understand what this means in the grand scheme of things."


Source: Obama Is ‘Healer-in-chief,' Comforting Families of Those Slain in Orlando
 
Wenzetu wanasemaje kuhusu kiongozi wao kuhudhuria "tragedies" ....

'Symbol of the country'


Ahead of Thursday's trip, White House press secretary Josh Earnest said the president sees these condolence trips as a solemn responsibility: "The president understands that he is a symbol of the country, and when he travels to a community and meets with a family that has endured a terrible tragedy, he's offering a message of condolence and comfort on behalf of the American people."

"When these kinds of events occur," Rottinghaus said in an interview, "the public really does look to the president as a true national healer, and somebody who can make sense of the situation, but who can also lend a shoulder to be able to understand what this means in the grand scheme of things."


Source: Obama Is ‘Healer-in-chief,' Comforting Families of Those Slain in Orlando

Hiyo ni kweli kabisa.

Magufuli was wrong for not going.
 
Sio lazima aende kwenye misiba wakati wapo makamu wake na anaweza kumuwakilisha... kwenye mambo kama hayo wacheni maneno mengi CHAPENI KAZI.
 
Yule dogo uliyefurahia alipompa peremende yuko wapi?

8D6U9682kikwetenapipi.jpg
Ahahahaaa daaaaah....

Umenikumbusha mbali sana aisee.

Hivi hii haikuwa 2008 au 2009 kweli?

Pia naukumbuka vyema kabisa ule mjadala wake.

I pretty much rolled solo in defending him saying there was nothing wrong with him giving candy to that youngster.

Dogo si ajabu atakuwa keshakuwa mtu mzima sasa.....

Umeifukulia wapi hiyo picha lakini?
 
Uzuri wa Rais Magufuli ni mtu ambaye ana misimamo isiyoyumba.

Ni kweli misimamo yake mingine iko kinyume na matarajio ya kisiasa lakini kwa Tanzania ya leo hii misimamo inahitajika sana.

Rais Magufuli amejifunza kwa yaliyotokea kwa Mzee Kikwete wakati akiwa Rais.

Mpaka pale wakosoaji wake watakapofahamu kuwa Rais Magufuli is the opposite of Rais Kikwete ndipo watakapogundua kuwa wanachokifanya ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.
Kwa hiyo unasema Mzee Kikwete alifanya madudu siyo?
 
Kwa hiyo unasema Mzee Kikwete alifanya madudu siyo?
Unaposema Rais Kikwete alifanya madudu una maana gani?

Kumbuka hakuna Rais au Waziri Mkuu duniani anayetoka madarakani bila kufanya madudu.

Hoja ya msingi ni madudu gani na yalikuwa na impact gani kitaifa na kimataifa?

Hukusikia wakati wa kampeni viongozi wa CCM walikuwa wanahubiri mabadiliko ya kweli? Hiyo inakuambia kuwa kuna masuala fulani yalifanywa na serikali ambayo yalitakiwa yafanyiwe mabadiliko ya kweli katika utawala wa serikali ijayo.
 
Back
Top Bottom