Rais, Tanzania si chochote katika utalii

Rais, Tanzania si chochote katika utalii

Mkuu hongera kwa analysis yako na facts kuhusu utalii na siasa za bongo...respect mkuu. Nilipopata hotuba ya Rais akiongelea watalii na mapata....nilichoona ni kuwa Rais ******, Worst president ever kwenye historia ya Tanzania. Lazima hatua za madhubuti zichukuliwe ili kuboresha sector ya utalii nchini ikiwa ni pamoja na kujenga ushawishi ili watalii waweze kuja. I guess tutakuja kuwa na hali mbaya ya kiuchumi huko mbeleni....
Hata miye nilisikiliza hotuba ya rais. Nilishatuka sana aliposema hao watalii kama hawataki kulipa VAT na wasije. Akaenda mbali zaidi na kusema hata meli bandarini nazo zisije. Kama tunawahimiza watu wetu waongeze uzalishaji ili tuweze kuuza nje zaidi, je hizo bidhaa tutabeba kichwani kama hizo meli haziji? Namshauri sana sana rais wetu awe anaandika hotuba zake kuepuka kutoa matamshi ambayo hayatoi mwelekeo wa tunakotaka kwenda. Baba wa taifa aliwahi kuonya juu ya wananchi kutokujua rais wao akiamka asubuhi atasema nini. Uchumi wetu unatawaliwa na sekta binafsi na hakuna mwekezaji makini atakayewekeza kama hana hakika na mkuu wa nchi atatoa amri gani akiamka asubuhi.
 
pamoja na kuamua kuweka vat serikali iweke nguvu sana katika kutangaza vivutio vyetu. mfano leo nimesikia redioni Kenya wameweka bajeti ya US dollar milioni 30 kutangaza vivutio vyao lakiniTanzania imetenga US dollar milioni 2, kwahiyo hata mambo ya wageni kusikia mlima Kilimanjaro uko Kenya yanaweza kuendelea kuwepo
 
Sawa! Lakini ata tukiwa wa mwisho wapo watu watakuja kitushangaa kwanini tu wajinga wa mwisho, hao sasa ndio tunataka waje walipe VAT, ata kama wawili. Waliobaki waende kunakovutia wakakwepe kodi!!.

....sio zalima waje kwetu........ Customer care na business strategies hapo zikoje?
 
Ukifuatilia kwa umakini, utaona nimetoa mapendekezo. Pendekezo kubwa ni kwa wahusika wa sekta kutambua kuwa utalii ni biashara, hivyo zinahitajika mbinu za kuboresha mazingira ya biashara hii ili yavutie watalii. Mazingira yetu yaonekane ni tofauti na ya sehemu nyingine kwa ubora kwa kutumia kile ambacho wengine hawana. Na hapo ndipo akili na werevu unapohitajika ili kujua ni nini na kwa namna gani tunaweza kufanya. Tusiamini kwa vile tu tuna pundamilia au twiga, eti kwa sababu tu hawapo sehemu nyingine, basi kila mtu atakuja kwetu au anataka kuja Tanzania. Utalii ni starehe, ni lazima uandamane na starehe. Ni namna gani utalii wetu unaweza kuwa unique na kuandamana na starehe? Haya ni mambo ambayo watendaji wa sekta hii wanatakiwa kuyafanyia kazi. Sisi kama wadau tuliopo nje, ushauri tunaotoa ni wa jumla, na wao wanatakiwa kuingia ndani zaidi kuyafanyia kazi mawazo yetu ili yaweze kuonekana katika uhalisia.
Si tunawalipa kwa kutengeneza sera, Watengeneze wawezavyo. Hata kama ni mbovu, sie huku mtaani iko powa tu. Tunajilia masebele, ulanzi na mikusu yrtu. Life GOes on. Kazi kwao wao wanategemea mishahara.
 
Na kumbuka amemuaddress mtanzania namba 1, ambaye ana machinery zote zinazoweza ku analyse hii taarifa na kutengeneza strategies!
Sio lzm ukiwa detective uwe pia hodari ktk kukamata!
Umenena vema sana mkuu,umeongeza kachumbali na chachandu kwenye hii hoja ya Msambichaka kaandika akiwa ametulia na werevu mkubwa hawa watu wa Lumumba siku zote ni mahaba niuwe.
 
Ndugu umeandika kinyodo saana,kusema tz tuna bahati mbaya na wajinga ni upuuzi mtupu. Maendeleo ni process na makosa nisehemu ya izo process...tunavyo vyetu vya kujivunia na vya kipekee ambavyo huvikuti kwingine. Yawezekana hujatembelea vivutio tofautitofauti ndomana unaishambulia nchi yetu Tz kwamaneno ya mkata tamaa,shame on You!!
Ziko tafiti za kuaminika kuwa tunavivutio vingi vya kipekee tukiwafuatia Brazili,ni swala la kubuni na kutekeleza sera nzuri ili tufaidi utalii. Tuanzie hapo nasio tujidharau na kusifia wengine.
Next time unapoandika epuka kuidharau nchiyako,jifunze uzalendo na kujikubali pia kujiamini. Leta mawazo constractive badala ya destructive nahapo utakuwa umeonesha kukuwa kiakili. Pole

Huna ujualo zaidi ya kupiga siasa. Mwenzio kaonyesha kabisa kwa data kuhusu utalii, ww unajifanya mzalendo huna data hata moja zaidi ya kusema tuna vivutio vingi tofauti nyuma ya Brazil wala huna data kutoka chanzo chochote. Au wewe ndio mmojawapo ya watu mnaompotosha rais kwamba tuna vivutio vingi mpaka watalii wanagombea kuja Tanzania? Ww ndio wale mliomezeshwa data kwenye vyuo vya siasa na hamna mjualo zaidi ya uzalendo wa kulinda tumbo.
 
Una mawazo mazuri lakini sijaona pale unapoleta suluhisho nini kifanyike bali umelalamika tu kama ilivyokawaida ya watanzania wengi ni hodari kwa kulalamika lkn wavivu kutoa suluhisho
Nami nichangie.....lazima tupitie upya hivyo viwango vya ushuru vinavyoonyesha kila dalili ya kuwapa Watalii chaguo mbadala la wapi kwa kwenda anapopanga kuja Africa au East Africa....tuongeze nguvu kwenye kutangaza (promotion)....tuwekeze pesa za kutosha la sivyo nchi jirani wataendelea kupanda juu ya migongo yetu.

Na lingine kubwa ni lazima tuache kuishi kwa ndoto za kudhania...hayo mafuta na Tanzanite Wazungu wakisema hawanunui ndio basi tumekwisha.
 
Cha kufanya tutumie vizuri hicho kidogo tulicho nacho na tusijione kwamba sisi ni special sana kwamba tutabembelezwa na mataifa mengine.
Nakubaliana na wewe. Kuna maeneo ya ushindani mkubwa kibiashara moja wapo hili la utalii anbalo umelitolea data nzuri sana. Miaka 10 iliyopita idadi ya watalii tanzania ilikua kwenye laki sita na serikali kupitia wakina waziri meghji na wadau walipania ifikapo 2010 watalii wafikie 1m. Bahati hiyo mark imefikiwa na kilichotakiwa kufanywa sasa ni kulinda idadi hiyo ya wageni na kuweka malengo mengine tufikie 2m 2020 na mikakati ya kuyafikia na si mikakati ya kupokonya kilichomkononi. Ukiangalia data zilizotolewa hapa utaona watalii hawapapatikii sana Tanzania. Hilo tu linatisho serikali ijue kwanini pamoja na vyote tuluvyonavyo iwe hivyo. Kwa hali hiyo tunatikisa kiberiti kwa watu ambao hawahitaji kuja Tanzania kama tunavyofikiri. Ona tu hata Uganda wako juu yetu na hapa hakuna data za Rwanda lakini nadhani wanakaribia au wako sawa na idadi tunayopokea. Labda serikali iache kumumunya maneno na iseme tu they want to do away with tourism. Hata hivyo wadau walishaweka wazi si kwamba wanaipinga vat ila walichoomba isogezwe ikiwezekana mwakani kuwapa nafasi ya kuwataarifu mawajala wa nje jambo ambalo limekua ndio utamaduni wa miaka yote kwenya hii sekta ya utalii.
 
Mkuu umenena ukweli mtupu.vivutio vingi vya utalii bila maarifa ni bure.hao viongozi hasa hiki kitengo cha utalii hawajui wanachofanya.hivi wanafikiri hao watalii matajiri watamiminika kuja tz katika mazingira haya ya sasa?waanze kufikiria kuwapata kwanza hawa watalii wa kawaida ambao ni wanunuz wa vinyago.nguo zetu za kitamaduni na ambao watahitaji vyumba vingi vya mahotelini na mwishowe watanufaisha wananchi wengi.fikiria idadi ya watu wataohitajika kutoa hizo huduma na bidhaa kwa hao watalii wa kawaida. Eti waziri anawaita maskini!
Hao watalii matajiri serikali inatafuta ni wale wanaokuja kwenye hotel za nyota tano zilizo mbugani. Wengi wao hawataki bughda ya kufanya shoping ya vinyago na hakuna biashara ndogondogo zitakazofaidi na watalii wa aina hiyo. Serikali haijuii tu jasho wakala analotoka kuleta mtalii moja tz. Wakati mwingine unajaza box file za email za mawasiliano na bado usimpate.
 
Mkuu wetu anasema kama hulipi VAT hatukutaki, kwani zamani walikua hawalipi? speech kama hiyo inatuma red alert kwa tourists wote kua hatuwajali kabisa, its disrespectful, binadamu tunapenda kuinterpret mambo tunavyojisikia, na in most cases siku hizi wako critical zaidi ukizingatia dunia ina idadi ya wasiojielewa kubwa kuliko wanaojielewa, ndio maana hua tunasema waandaliwe speech sio kuropoka.

Tunajidai tuna kila kitu huku hatuna chochote, ngoja tuendelee kufukuza tukidhani watakuja kutupigia magoti, mtu ambaye hajatembea hawezi jua kua ni cheaper kwenda kutembelea nchi kama US kuliko Tanzania (hii ni fact) tourism locations za Tz ni very expensive na tunajitahidi kuzifanya even more expensive. Kukusanya hela kwenye utalii tusingeconcentrate kwenye kuongeza VAT, concentration yetu ingekua kwenye kuleta more people, kubuild experiences ambazo zitavutia watu kuja Tz kua na wanyama peke yake is nothing kama we are not innovative, we have to transform hizi tourist destinations into paradise sio kuzifunga au kupunguza employees kucover costs. "Father is always right"

Zanzibar, Serengeti, Ngorongoro na Mlima Kilimanjaro ndo vinatutoa kimasomaso.
Kwingine ni uozo mtupu.
 
Hivi hao watalii matajiri tunaowafikiria watakuja Tanzania kuangalia vivutio gani? Au utalii wetu ni mbuga na milima tu?
 
Hao watalii matajiri serikali inatafuta ni wale wanaokuja kwenye hotel za nyota tano zilizo mbugani. Wengi wao hawataki bughda ya kufanya shoping ya vinyago na hakuna biashara ndogondogo zitakazofaidi na watalii wa aina hiyo. Serikali haijuii tu jasho wakala analotoka kuleta mtalii moja tz. Wakati mwingine unajaza box file za email za mawasiliano na bado usimpate.

Sio watalii matajiri wote wanaopenda kuangalia wanyama au kupanda mlima kilimanjaro.
Wengine wanapenda kupumzika tu. Kwahiyo hapo tunajilimit kwenye utalii.
 
Msumbiji na Afrika kusini wanashirikiana bega kwa bega kwenye suala la utalii. Kuna la kujifunza hapo. Mara nyingi utaskia waziri wa utalii wa Msumbiji yupo Afrika kusini. Na pia ukiwa Msumbiji utayaona magari with South African license plates. Ni mengi unaweza ukajisahau ukadhani bado umo Afrika kusini. Hawa washirika wawili tunaona hapo kwenye takwimu wapo juu kwa Afrika. Naamini tunalo la kujifunza hasa kutoka kwa Msumbiji.
 
Facts kama hizi humsaidia mtu kufanya maaamuzi. Hivyo endapo sera au sheria ya utalii kwa sasa inatekelezwa bila ya kuwepo na takwimu zozote basi tutegemee maumivu.
 
Hata miye nilisikiliza hotuba ya rais. Nilishatuka sana aliposema hao watalii kama hawataki kulipa VAT na wasije. Akaenda mbali zaidi na kusema hata meli bandarini nazo zisije. Kama tunawahimiza watu wetu waongeze uzalishaji ili tuweze kuuza nje zaidi, je hizo bidhaa tutabeba kichwani kama hizo meli haziji? Namshauri sana sana rais wetu awe anaandika hotuba zake kuepuka kutoa matamshi ambayo hayatoi mwelekeo wa tunakotaka kwenda. Baba wa taifa aliwahi kuonya juu ya wananchi kutokujua rais wao akiamka asubuhi atasema nini. Uchumi wetu unatawaliwa na sekta binafsi na hakuna mwekezaji makini atakayewekeza kama hana hakika na mkuu wa nchi atatoa amri gani akiamka asubuhi.
Hiyo VAT inavyopigiwa kelele utafikiri ndiyo source pekee ya pesa Tanzania .....!!

Ndiyo maana mleta mada kasema Tanzania tunaaminishwa vitu vingi kuwa viko bora au ni vingi hapa kuliko kwingine .... Yaani ni Propaganda mbele kwa mbele kama enzi za Mwalimu!!

Yaani tulishaaminishwa kwamba Tanzanite iko Tanzania tu kumbe siyo kweli!!
 
Tufungue macho ndugu yetu na hizo mbinu mpya,naona umejikita kulalamika na kulaumu!

Yaani nchi yetu hii watu wake ni majanga kabisa. Sasa mtu kaanza kwa kulalamika, kaandika zaidi ya maneno 10000 kukosoa na mwisho eti Rais ampe mbinu za kuongeza mapato na kuifanya nchi kivutio kikuu cha utalii. Kweli?????!!!!!!
Hivi nguvu yote hiyo aliyotumia mpaka kutafuta takwimu za nani anaongoza ktk utalii, ameshindwa kabisa kutafuta hata wazo moja la kushauri nini kifanyike??
Siku hii nchi watanzania tutaacha kulalamika na kuanza tumia akili zetu kutoa mawazo boresho hakika tutasonga mbele.
 
Back
Top Bottom