Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,842
- 31,073
Umeandika vitu vya maana sana tena sana....Watanzania ni watu wenye bahati mbaya sana maana mara nyingi wanaaminishwa kuwa wao ni bora katika kila kitu. Wengi wao, kwa ujinga tu, nao wameyabeba maneno hayo na kuyaweka katika vichwa vyao.
1.Wapo Watanzania wanaoaminishwa kuwa Tanzania ina dhahabu nyingi kuliko nchi yoyote Duniani, ambao ni uwongo, lakini wao wanaamini
2. Wapo Watanzania wanaoamini kuwa tuna gas nyingi kuliko nchi yoyote, ambao ni uwongo
3. Wapo Watanzania wanaoaminishwa kuwa Tanzania ina madini ya kila namna na ina madini mengi kuliko nchi yoyote Duniani/Afrika, ambao ni uwongo
4. Wapo Watanzania wanaoamini kuwa Tanzania ni nchi yenye amani kuliko nchi zote za Afrika, ambao ni uwongo
5. Wapo Watanzania wanoamini kuwa nchi yetu ina demokrasia, utawala wa sheria na uongozi mzuri kuliko nchi yoyote ya kiafrika, nao ni uwongo lakini wanaamini
6. Wapo Watanzania wanaoaminishwa kuwa Tanzania ni nchi nzuri sana ambayo kila mwanadamu angependa kuja na kuishi, nao ni uwongo lakini wengi wanaamini hivyo
7. Wapo Watanzania wanaoamini kuwa Tanzania ni nchi yenye vivutio vingi na mazingira mazuri ya utalii ambayo hayapo mahali pengine popote Duniani, ambao ni uwongo mkubwa.
Takwimu za mwaka 2014 kuhusu utalii wa kimataifa (International tourist arrivals) inaonesha kuwa hakuna hata nchi moja ya Afrika ambayo ilikuwa miongoni mwa nchi 10 za juu katika kutembelewa na watalii. Hii inaonesha kuwa watalii hawa wa kizungu wanapendelea zaidi kwenda kwenye mabara mengine kuliko Afrika.
In 2014, there were 1.133 billion international tourist arrivals worldwide, with a growth of 4.3% as compared to 1.087 billion in 2013.[1] The top 10 international tourism destinations in 2014 were
1. France Europe 83.7 million
2. United States North America 74.8 million
3. Spain Europe 65.0 million
4. China Asia 55.6 million
5. Italy Europe 48.6 million
6. Turkey Europe 39.8 million
7. Germany Europe 33.0 million
8. United Kingdom Europe 32.6
9. Russia Europe 29.8 million
10. Mexico North America 29.1
Katika Afrika, Tanzania haipo hata katika 10 bora
In 2014, there were over 55.7 million international tourist arrivals to Africa, the top ten African destinations were
1. Morocco 10.2 million
2. Egypt 9.6 million
3. South Africa 9.5 million
4. Tunisia 6.0 million
5. Algeria — 2.7 million
6. Mozambique — 1.8 million
7. Zimbabwe 1.8 million
8. Kenya — 1.4 million
9. Uganda — 1.2 million
10. Namibia — 1.1 million
Jambo la kusikitisha ni kwamba, nchi inayoongoza kwa kutembelewa na watalii wageni katika Afrika ambayo ni Morocco, idadi ya watalii inaowapokea ni chini ya watalii wanaotembelea nchi ya mwisho ya 10 bora ya Ulaya.
In 2014, there were over 582 million international tourist arrivals to Europe, an increase of 3.0% over 2013. In 2014, the top ten destinations were
1. France 83.7 million
2. Spain 65.0 million
3. Italy 48.6 million
4. Turkey 39.8 million
5. Germany 33.0 million
6. United Kingdom 32.6 million
7. Russia 29.8 million 28.4
8. Austria 25.2 million
9. Greece 22.0 million
10. Poland 16.0 million
Ukija kwenye mapato ya utalii, Tanzania na Afrika si lolote na si chochote. Idadi kubwa ya watalii inawianika kwa kiwango kikubwa na mapato ya utalii. Hayo maneno ya kusema kuwa unaweza kuwa na watalii wachache halafu mapato yakawa makubwa ni ndoto za alinacha zinazootwa na maprofesa wa Tanzania pekee.
International tourism receipts grew to US$1,245 billion in 2014, corresponding to an increase in real terms of 3.7% from 2013.[11] The World Tourism Organization reports the following countries as the top ten tourism earners for the year 2014, with the United States by far the top earner.
1United States North America $177.2 billion![]()
2Spain Europe $65.2 billion![]()
3China Asia $56.9 billion![]()
4France Europe $55.4 billion![]()
5Macau Asia $50.8 billion![]()
6Italy Europe $45.5 billion![]()
7United Kingdom Europe $45.3 billion![]()
8Germany Europe $43.3 billion![]()
9Thailand Asia $38.4 billion![]()
10Hong Kong Asia $38.4 billion![]()
Kwa mapato ya utalii wa kimataifa katika Afrika, nchi inayoongoza ni Afrika Kusini ($9.4 billion) ikifuatiwa na Misri ($7.2 billion), Morrocco ($7.1 billion) na Tunisia ($2.3 bilion). Kwa ujumla yule anayeongoza kwa mapato ya utalii katika Afrika hayupo katika 10 bora za Dunia, na ni chini ya mapato ya nchi ya mwisho ya 10 bora katika mabara mengine.
Mapato ya utalii ya Tanzania kwa mwaka 2014 yalikuwa $1.95 billion, chini kuliko mapato ya Singapore ($19.20 billion), Turkey ($37.37 billion), Qatar (10.58 billion) au Misri ($7.21 billion). Singapore, Turkey, Qatar na Misri hawana twiga wala tembo lakini wanatuzidi kwa idadi ya watalii na kimapato mara dufu.
Profesa Maghembe, Rais wetu na Watanzania, wanatakiwa kufahamu kuwa vivutio vya utalii ni zaidi ya idadi ya tembo, fisi, twiga, pundamilia na ngiri tulio nao. Utalii mkubwa ni akili, yaani unaweza kufanya nini kwa kutegemea mazingira yako ili watu wa mataifa mengine waje kushuhudia na kustarehe katika mazingira yako.
Watanzania, kwa ujinga wetu, tunaamini kuwa kwa sababu tu tuna nyumbu wengi, twiga na tembo basi watu wengi, Dunia nzima wanahangaika ili waje watazame sura ya twiga. Watalii hawana haja na sura ya pundamilia wala mbwa mwitu bali wanataka kuona mazingira ya kuvutia yaliyo tofauti na mahali pengine, na sisi tunaweza kuwatumia wanyama hao kuweza kuyafanya mazingira yetu kuwa ya kuvutia zaidi kuliko Misri ambako mapiramidi na chuo kikuu cha kwanza cha Alexandria, vimetosha kuizidi Tanzania kimapato.
Ushauri wangu kwa Rais, fukuza kazi prof. Maghembe maana amekupotosha kwa kueleza kuwa hakuna uhusiano wa mapato katika utalii na idadi ya watalii. Waziri unayetakiwa kuwa naye ni yule ambaye ataihakikishia Tanzania inapata ongezeko kubwa la watalii na siyo upungufu wa watalii. Bila ya kujali kama ongezeko la idadi ya utalii na mapato ya utalii vitategemea kupungua kwa kodi au kuondoa baadhi ya kodi, au kuongeza mbinu za kujitangaza au kuboresha miundombinu na huduma za kitalii, ukweli ni kwamba tunahitaji ongezeko la idadi ya watalii na mapato yatokanayo na utalii ambavyo vinaenda sambamba hata kama siyo kwa uwiano 1:1
Rais Magufuli hatutakuelewa kama pamoja na vyote tulivyo navyo, lakini mapato ya utalii yataendelea kuwa chini kuliko ya Afrika Kusini, Misri, Morocco, Tunisia na Kenya, huku wewe mwenyewe ukisema tuna vivutio vingi vya utalii. Tuna vivutio vya utalii visivyovutia watalii.
Mheshimiwa Rais, hotuba zako za mara kwa mara za kuelezwa nchi hii imeibiwa sana tumekwishazisikia kiasi cha kutosha, sasa tunahitaji kusikia kutoka kwako juu ya mbinu za kuongeza mapato ya utalii (siyo kodi za utalii bali mapato), mbinu za kuongeza mauzo ya mazao yetu nje ya nchi, mkakati wa kujenga uchumi wa viwanda, na namna rasilimali nyingine kama gas na madini zinavyoweza kubadilishwa kuwa mapato ya wananchi na Taifa. Mheshimiwa Rais tunataka mbinu na mikakati ya kuongeza mapato ya Watanzania.
Sisi wengine daima tutazidi kueleza pale tunapoona mbinu siyo sahihi. Tunaamini una dhamira njema lakini tuna mashaka makubwa katika mbinu.
Binadamu tuna miaka michache Duniani, hatuna muda wa kufanya majaribio bali tunatakiwa kuenenda kwa namna na mbinu zilizosahihi katika kuibadilisha nchi hii iliyo maskini kupindukia lakini iliyo na fursa nyingi zilizofunikwa. Fursa ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kitalii ni kubwa sana lakini hatuna watu wa kuweza kufungua fursa hizo ili jamii iweze kuziona kwa sababu waliopewa mamlaka ya kuzifunua kwa umma wanafanya kila mbinu ya kuzifunika ili wananchi wasizione na wala wasizifaidi.
Lakini wasiwasi wangu ni kuwa hizo 'nondo' ulizoshusha zitafall under deaf ears za watawala wetu.....
Nimewasikia Profesa Maghembe na Rais Magufuli wakitoa kauli za kushangaza sana kuhusiana na ongezeko hilo la VAT kwa huduma zote za kitalii kuanzia Julai Mosi mwaka huu.
Alianza Profesa Maghembe ambaye aliongea kwa kiburi cha hali ya juu kuwa Tanzania haihitaji watalii 'malofa' wabeba mabegi migongoni mwao!
Akaendelea kutamba kuwa Tanzania inahitaji watalii wachache lakini wenye 'pesa zao' na hao watalii wabeba mabegi ni bora wabaki huko huko kwao Ulaya!
Naweza kuiita kauli hiyo ni ya masikini jeuri!
Kwa kuwa haiingii akilini kwa hao hao wazungu ambao siku zote sisi huwa tunatembeza bakuri la omba omba kwao, leo tukajigeuza sisi ndiyo matajiri na hatuna haja ya hao wazungu 'malofa' waje kutalii nchini kwetu!
Rais wetu naye katoa kauli jana inayofanana na ya Waziri wake kwa kusema yeye anachotaka watalii hao walipe hiyo kodi iliyokuwa introduced July mosi bila kutoa visingizio vyovyote na Rais akaenda mbali zaidi kwa kusisitiza kuwa ni bora kuwa na watalii laki 5 wanaolipa kodi kubwa kuliko kuwa na watalii milioni 2 wanaolipa kodi kidogo!
Hivi Rais anataka kusema kuwa keshasahau ile principle inayosema haba na haba hujaza kibaba?
Hata hivyo hii serikali ya awamu ya 5 inaelekea kuwa si sikivu hata kidogo......
Tukumbuke hoja ya msingi kabisa waliyotoa Tour Operators ni kuwa hizo bookings za hao watalii ambao walikuwa waanze kuja mwezi huu wengi wao bookings zao walizifanya zamani toka mwaka jana wakati hiyo VAT ilikuwa bado haijawa introduced.
Tukumbuke kuwa mifumo ya maisha ya wenzetu wazungu huwa wanapenda wakati wote kufanya bajeti ya mambo yao mapema.
Sasa wanaiona nchi hii ya ajabu sana kwa staili yake ya kukurupuka....
Hivi serikali hii ilishindwa nini kuintroduce hiyo VAT yao kuanzia July mwaka 2017, na kipindi chote hiki hadi mwakani Tour Operators wetu wafanye kazi ya kuwajulisha watalii wetu ili wajiandae na mabadiliko hayo yatakayoanza mwakani?
Sasa hivi ndiyo naelewa ni kwa nini serikali yetu imepiga STOP kuonyeshwa Bunge LIVE, sababu kuu kumbe ni kuwa serikali hii haitaki kabisa mawazo yoyote mbadala nje ya 'fikra sahihi' za watawala wetu, kwa kuwa wamejipa uwezo wa kiMungu mtu!
