Rais, Tanzania si chochote katika utalii

Rais, Tanzania si chochote katika utalii

Una mawazo mazuri lakini sijaona pale unapoleta suluhisho nini kifanyike bali umelalamika tu kama ilivyokawaida ya watanzania wengi ni hodari kwa kulalamika lkn wavivu kutoa suluhisho
Hajasema kuwe na miundo mbinu mizur kwa ajili ya utalii? Hajasema kuwe na mbinu za kuutangaza utalii zaidi kulikoni kusubir tu waje? Au wewe umesoma kichwa cha habari tu boss.
 
Hivi Magufuli anayajua haya?!
Hata kama majuzi wakati ameongelea kuhusu issue ya Luhende wa Hotel ya Sinza, tumegundua kuwa anapita mara kwa mara humu JF, lakini inaonekana Tatizo kubwa la huyo jamaa ni kuwa anaendesha nchi kwa staili ya ONE MAN SHOW, kwa hiyo amejipa uwezo wa Mungu mtu katika kuliongoza Taifa letu, hasikii ushauri wala mawazo ya mtu yeyote, anajiona yeye ndiye each and everything, kwa hiyo hapaswi kukosolewa wala kusahihishwa kwa maamuzi yake..

Hebu nitaje baadhi ya matatizo makubwa yaliyosababishwa na maamuzi yake ambayo hataki kabisa yakosolewe.

1. Tulishuhudia maamuzi yake ya kupiga marufuku uagizaji sukari nje namna ulivyopaisha bei ya sukari nje hadi kufikia zaidi ya shilingi 5,000 kwa kilo, ambapo hadi leo bei ya sukari haijastabilize.....

2. Tumeshuhudia Mkuu akivunja Katiba ya nchi waziwazi kabisa kwa kupiga marufuku shughuli zozote za kisiasa kufanywa na vyama vya upinzani na wakati huo huo kutoa 'ruksa' kwa chama chake cha CCM kuendelea kufanya shughuli za kisiasa bila kubughuziwa na Polisi, ambapo ni kuisigina Ibara ya 3 ya Katiba ya nchi ambapo inabainisha wazi kuwa hii nchi itaendeshwa kwa mfumo wa vyama vingi.

Zipo kila dalili kuwa Mkuu wetu anataka kuturejesha enzi za Mao za zidumu fikra za Mwenyekiti.....

Kwa maana hiyo Jenerali Ulimwengu hajakosea pale akipobainisha kuwa kidemokrasia nchi yetu imerudi nyuma miaka 50!!
 
Hivi Magufuli anayajua haya?!
Hivi Magufuli anayajua haya?!
Hivi Magufuli anayajua haya?!
Kwa nchi hii inavyokwenda sasa ipo haja kwa Umma wa watanzania kuchukua ujasiri wa yule mtoto kwenye hadithi ya yule Mfalme, ambapo aliuvaa ujasiri wa kumwambia Mfalme kuwa anatembea uchi ambapo watu wazima wote waliogopa kumpasulia ukweli huo yule Mfalme, kutokana na alivyokuwa anatisha enzi za utawala wake.....

Iwapo watanzania hatutachukua sasa hatua ya ujasiri ya kumwambia Mkuu wetu kuwa unakoenda is the wrong way, upo wasiwasi mkubwa huko mbele ya safari tutalia na kusaga meno na wakati huo tutaishia tu kujilaumu wenyewe kwa kuwa tayari itakuwa TOO LATE............
 
Naamini wewe ni mdau mkubwa wa utalii na umenena vyema sn lkn jambo moja pamoja na mwanga wa kutoa suluhisho la kufukuza waziri, bado halitoshi kuleta mabadiliko maana takwimu ulizoleta ni zinahusu kabisa awamu iliyopita kumhusisha waziri wa sasa kwa makosa yaliyofanyika nyuma kwa maoni yangu sio sahihi. Jambo kubwa nililojifunza hapa kuwa bado tuna kazi kubwa ya kufanya na kuweka ubuniufu wa hali ya juu ili kukuza na kuvutia watalii. Maana kutokuwepo tu kwenye 10 bora kama destination ya watalii kwa miaka ya nyuma inaonesha kuwa hili tatizo sio la leo tafakari
 
Hivi Magufuli anayajua haya?!
Hivi Magufuli anayajua haya?!
Hivi Magufuli anayajua haya?!
Watanzania wengi hivi sasa ndiyo wataanza kufunuliwa akili zao na kuanza kupata tafsiri ya Mkuu wakati wa kampeni mwaka jana kuwa alikuwa akimaanisha nini pale kwenye kampeni zake nyingi alipokuwa hajinadi kwa kusema serikali ya CCM itafanya hili na lile, badala yake alikuwa akijinadi kuwa Tanzania ya Magufuli itafanya hili na lile.......

Kumbe alichokuwa akikimaanisha ndiyo hiki tunachokiona sasa cha kuua utawala wa Power seperation ya Executive, Legislature na Judiciary na mahala pake 'amereplace' na kile kitu kinachoitwa ONE MAN SHOW.........
 
Hoja ya mtoa mada ni nzuri sana na very analytical pia.

Lakini pia sioni tatizo la VAT kuongezwa katika utalii.

Kwanza wanalipa pesa nyingi sana kwa agents, zinazobakia huko huko kwao zaidi ya 18% ya huduma atakayopata akiwa tayari nchini.

Si vibaya sisi tukiongeza kodi ya ongezeko la thamani kwao kama walaji wa huduma ya kitalii pia hapa nyumbani, haiwezi kumzuia mtalii hata kidogo.

Kazi kubwa na ambayo mtoa mada kaigusia, ni sisi kujiaminisha tuna vivutio lakini mbona hawaji angalau kama Kenya, Uganda na kufikia Morocco kabla ya hata hizo zingine?

Ndipo pa kujiuliza, ndipo penye tatizo na ndipo pa kufanyia kazi.

Hatuna haja ya kutukanana ama kubezana. Mtoa mada hata kama hana suluhisho, tayari mchango wake umezua mada muhimu sana na serious debate na ianze tufanye nini haswa?
 
Kuna kitu kidogo sana ambacho hamuelewi na hili siyo kosa lenu bali ni uwezo wenu mdogo wa kufikiri na kutatua matatizo,

idadi ya watalii ≠ Mapato ya fedha za utalii
Hivyo kama ungekuwa na akili ungeweka hapa pia na mapato ya nchi yanayotokana na Utalii, yaani Utalii unachangia asilimia (%) kwenye pato (GDP) la nchi husika? Na siyo unakuja tu na namba tu zilizo uchi, inawezekana kabisa nchi kama Austria au Uswisi ambazo hazimo hata kwenye orodha yako mchango wa utalii kwenye GDP yao ni mkubwa klk hata Ufaransa au USA!
Hujaelewa boss!
Hayo mapato ni zao la shughuli za utalii na si GDP ya taifa husika!
 
Una mawazo mazuri lakini sijaona pale unapoleta suluhisho nini kifanyike bali umelalamika tu kama ilivyokawaida ya watanzania wengi ni hodari kwa kulalamika lkn wavivu kutoa suluhisho
Hii ni hatua muhimu sana ktk kufikia suluhisho!
Mleta mada hajalalamika, yeye ameonesha kuwa kuna tatizo somewhere, na ameenda mbali kuonesha mifano kadhaa inayoonesha kuwa hatuko sawa!
Na kumbuka amemuaddress mtanzania namba 1, ambaye ana machinery zote zinazoweza ku analyse hii taarifa na kutengeneza strategies!
Sio lzm ukiwa detective uwe pia hodari ktk kukamata!
Vitengo hutegemeana!
So are the thinkers!
 
Ndugu umeandika kinyodo saana,kusema tz tuna bahati mbaya na wajinga ni upuuzi mtupu. Maendeleo ni process na makosa nisehemu ya izo process...tunavyo vyetu vya kujivunia na vya kipekee ambavyo huvikuti kwingine. Yawezekana hujatembelea vivutio tofautitofauti ndomana unaishambulia nchi yetu Tz kwamaneno ya mkata tamaa,shame on You!!
Ziko tafiti za kuaminika kuwa tunavivutio vingi vya kipekee tukiwafuatia Brazili,ni swala la kubuni na kutekeleza sera nzuri ili tufaidi utalii. Tuanzie hapo nasio tujidharau na kusifia wengine.
Next time unapoandika epuka kuidharau nchiyako,jifunze uzalendo na kujikubali pia kujiamini. Leta mawazo constractive badala ya destructive nahapo utakuwa umeonesha kukuwa kiakili. Pole
 
Binafsi nimeipenda huu uchambuzi ni wa kina, nilishangaa waziri wa utalii alisema hawataki watalii masikini, wakati wale watalii anaowaita masikini wanalipa vingiilio vikubwa kuliko watalii matajiri wa hapa Tanzania, na wengi wao ni wanafunzi kule ulaya, sasa ndiyo tunapata watalii matajiri watatu badala ya watalii masikini kumi, haya masuala ya utalii yatizamwe kwa makini, lakini nina mashaka na maprofessor wetu.
 
Naamini wewe ni mdau mkubwa wa utalii na umenena vyema sn lkn jambo moja pamoja na mwanga wa kutoa suluhisho la kufukuza waziri, bado halitoshi kuleta mabadiliko maana takwimu ulizoleta ni zinahusu kabisa awamu iliyopita kumhusisha waziri wa sasa kwa makosa yaliyofanyika nyuma kwa maoni yangu sio sahihi. Jambo kubwa nililojifunza hapa kuwa bado tuna kazi kubwa ya kufanya na kuweka ubuniufu wa hali ya juu ili kukuza na kuvutia watalii. Maana kutokuwepo tu kwenye 10 bora kama destination ya watalii kwa miaka ya nyuma inaonesha kuwa hili tatizo sio la leo tafakari
Waziri aliyeko madarakani alisema hawataki watalii masikini, sasa hii ndiyo kauli ya kuendesha?
 
Good Advice But We Cannot Build Tz OverNight.
Mistakes Are Inevitable.
Waziri aliyeko madarakani alisema hawataki watalii masikini, sasa hii ndiyo kauli ya kuendesha?
Wewe hukumsikia Mkulu akisema watalii kama hawataki kulipa VAT wakae huko huko kwao, wasije huku, wakija tunawatumbua.
Sijui ni nani anamshauri huyu bosi wa wadanganyika. Hivi anafikiri hayo anayoyasema yanaishia Lumumba na Kigamboni?
Na sio kweli kwamba watalii hawataki kulipa VAT. Lililofanyika ni "hapa kodi tu" ya kustukizia/ ya mwendokasi wakati watalii walishafanya bookings zao.
 
Hongera kwa mtoa mada umeleta tafakuri nzuri kwa wenye akili.Ukweli ni kwamba wenye dhamana ya utalii wana uelewa mdogo sana kuhusu dhana ya utalii wa karne ya digital.kuna mbinu nyingi wanaweza ku capitalize mfano kutumia ofisi zetu za ubalozi,mikutano yote ya ndani na nje ya nchi,usafiri,mitandao ya kijamii,kuboresha miundombinu ya utalii,kuweka matangazo ya hali ya maendeleo,GDP,Utamaduni,Miradi mikubwa ya kitaifa,kutumia taarifa mbalimbali chanya kuhusu Tzn timely na kujenga image chanya ya nchi wakati wote and the likes
 
Hajasema kuwe na miundo mbinu mizur kwa ajili ya utalii? Hajasema kuwe na mbinu za kuutangaza utalii zaidi kulikoni kusubir tu waje? Au wewe umesoma kichwa cha habari tu boss.

Msomi kuandika suluhisho kijumla jumla hivyo anaonyesha alivyo na upeo mdogo.Alitakiwa aeleze kivipi? atoe takwimu kuwa hali ilivyo sasa ya miundombinu ikoje au utangazaji ulivyo sasa ukoje na una mapungufu yepi na atoe vithibitisho kuwa upungufu uko wapi.Aeleze nchi sasa inafanya hivi katika kutangaza mfano inatakiwa ifanye hivi na vile.Lakini kueleza tu kama mnywa kiroba kuwa serikali iweke miundo mbinu na iwe na mbinu za kutangaza BULLSHIT!! Angekuwa mshauri wangu ningemfukuza kazi siku hiyo hiyo na huo ushauri wake ningeutumbukiza kwenye shimo la choo.
 
Una mawazo mazuri lakini sijaona pale unapoleta suluhisho nini kifanyike bali umelalamika tu kama ilivyokawaida ya watanzania wengi ni hodari kwa kulalamika lkn wavivu kutoa suluhisho
Unahitaji step by step tutorial!
 
Na sio kweli kwamba watalii hawataki kulipa VAT. Lililofanyika ni "hapa kodi tu" ya kustukizia/ ya mwendokasi wakati watalii walishafanya bookings zao.

Una maana gani unaposema kodi ya VAT imeshtukizwa kwa watalii waliokwisha fanya booking?

Dunia nzima hata huko wanakotoka watalii wanajua kuwa kipindi cha bajeti ya serikali huwa yanakuweko mabadiliko mbali mbali yakiwemo ya kodi.Ni kitu kinachotarajiwa kwenye bajeti zote duniani.

Huyo aliyewafanyia booking kabla ya bajeti ilibidi awaambie wazi kuwa pesa yenu nachukua lakini siwezi kuwapa guarantee kuwa bei itakuwa ni hii sababu kutakuwa na bunge la bajeti hivyo bei zaweza badilika.

Huwezi kumwahidi mtalii kuwa bei itakuwa ni hiyo wakati hujui kwenye bajeti kuna nini.
Bajeti ikishapita unakuwa na uhakika sasa na unaweza endelea kupokea hizo pesa zao za booking.

Bajeti ya nchi sio kitu cha kushtukiza hata wao wanajua hadi miezi ya bajeti
 
Back
Top Bottom