Nimeshangazwa sana kwa kitendo ulichofanya jana mkoani Arusha kuugeuza mkutano wa hadhara wa Rais wa JMT kuwa mkutano wa kisiasa wa CCM.
Ninakukumbusha kwamba gharama zilizotumika jana ni kodi zinazotolewa na Watanzania wote na yamkini waliokuwepo uwanjani ni watanzania wa vyama vyote na wasiokuwa na vyama waliokuja kumsikiliza Rais wao.
Kuugeuza mkutano ule kuwa ni wa CCM ni kinyume kabisa na haupaswi kurudia tena kwani ni kuisigina katiba yetu waziwazi jambo ambalo halipaswi kurudiwa.
Ikumbukwe huko nyuma mwendazake aliwahi kufanya hivyo mara kadhaa hapo hapo jijini Arusha.
Hata hivyo Mzee Dialo juzi ametueleza ni kwanini hayo yalikuwa yanafanyika hivyo.
Sina hakika kama una nia ya kuwekwa kwenye fungu hilo.
Ahsante.
Ninakukumbusha kwamba gharama zilizotumika jana ni kodi zinazotolewa na Watanzania wote na yamkini waliokuwepo uwanjani ni watanzania wa vyama vyote na wasiokuwa na vyama waliokuja kumsikiliza Rais wao.
Kuugeuza mkutano ule kuwa ni wa CCM ni kinyume kabisa na haupaswi kurudia tena kwani ni kuisigina katiba yetu waziwazi jambo ambalo halipaswi kurudiwa.
Ikumbukwe huko nyuma mwendazake aliwahi kufanya hivyo mara kadhaa hapo hapo jijini Arusha.
Hata hivyo Mzee Dialo juzi ametueleza ni kwanini hayo yalikuwa yanafanyika hivyo.
Sina hakika kama una nia ya kuwekwa kwenye fungu hilo.
Ahsante.