Rais Samia Suluhu Hassan na mfumo wa 'contrarian approach'

Monica Mgeni

Member
Oct 7, 2021
82
134
15-scaled.jpg
Rais Mhe. SAMIA SULUHU HASSAN anatumia mfumo wa 'Contrarian approach' kwenye teuzi ambao kisiasa unawapa fursa Viongozi wa juu kufanya uamuzi ambao hautarajiwi na wananchi walio wengi, Mfumo huu umetajwa kuwa ni mzuri katika kupata matokeo ya haraka na yanayotarajiwa na kiongozi husika.

Hivi Karibuni tumeona Mhe. Rais akifanya teuzi za Viongozi Wakuu katika Vyombo vya Ulinzi, ambao ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Mkuu wa Jeshi la Polisi lengo likiwa ni kuboresha utendaji kazi wa Vyombo husika kwa maslahi ya Taifa.

Katika teuzi hizi mpya za Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa nimeona dhamira kuu ya Rais kwa kuwa aliowateua ni watu wenye sifa stahiki za uongozi na uwajibikaji, hivyo pasipo na shaka yoyote naona namna kero mbalimbali za wananchi zinazokwenda kutatuliwa kupitia wateule hao.

Katika kipindi kifupi cha uongozi wake, tumeona Rais SAMIA amejipambanua kuwatumikia wananchi na kuwaletea maendeleo katika Nyanja zote ikiwemo kuboresha miundombinu na kuwapatia wananchi huduma mbalimbali za kijamii.

Wito wangu kwa wananchi katika mikoa mbalimbali nchini, tuwaunge mkono na kushirikiana vyema na wateule hao kwa kuwa wao wanamuwakilisha Rais.

Tudumishe Amani ya Nchi yetu na kwa pamoja tujenge Umoja wa kitaifa. Aidha, tujitokeze kuhesabbiwa Agosti 23, 2022 ili tuisaidie Serikali kupata takwimu sahihi zitakazoiwezesha kutuhudumia
 
Nitarudia baadae kusoma nione kama nitaelewa kuwa Peter Serukamba na Dk. Rapbael Chegeni wameteuliwa ili kuwetea maendeleo wananchi!
 


Hivi Karibuni tumeona Mhe. Rais akifanya teuzi za Viongozi Wakuu katika Vyombo vya Ulinzi, ambao ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Mkuu wa Jeshi la Polisi lengo likiwa ni kuboresha utendaji kazi wa Vyombo husika kwa maslahi ya Taifa.
Hayo uliyoandika ni mawazo yako yasiyo na uhalisia wowote.

Mkuu wa Majeshi CDF, Gen Venance Mabeyo, na hata Mkuu wa Polisi IGP, Simon Sirro walikuwa wamefikia umri wa kustaafu kwa mujibu wa sheria.

Hivyo msukumo wake katika mabadiliko hayo katika vyombo hivyo ni orderly succsession ambayo ilikuwa inategemewa na wengi.
 
Teua tengua aliifanya mtangulizi wake ikawa mbaya, wachumia tumbo mkasema sema weeeee.

Tozolian ana teua tengua, mnaita nini, "contrarian approach"😆

Mnakumbuka kuwa nchi ishachukua zaidi ya Trilioni 8 shillings za watu na hatuzioni mtaani?

Eti anaowateua wana sifa za uongozi, wakina nani hao? Kutokea chamani?

Mnakumbuka kuwa nchi ishachukua zaidi ya Trilioni 8 shillings za watu na hatuzioni mtaani?

Tozo ziendelee.
 
Rais Samia Suluhu anafanya maamuzi yake kwa akili kubwa nimependa sana hii situation ya kuteua mala kwa mala ili viongozi wasirelax wafanye kazi kwa ushindani
 
Back
Top Bottom