Rais Samia siyo wote walioachishwa kazi kipindi cha Magufuli walighushi vyeti, wasaidie

HAKI KWA WOTE

JF-Expert Member
Nov 30, 2022
607
553
Habari Rais Samia,

Nianze kwa kukupongeza kwa uamuzi wako wa kuwalioa waliofukuzwa kazi kwa kughushi vyeti, ila napenda utambue kuna wengine hawaghushi vyeti bali waliachichwa kazi kwa sababu tofauti kabisa na hiyo.

Mimi nitazungumzia wale walioachishwa kazi kwakuwa tu walibadili kada zao baada ya kujiendeleza kisha wakafanya mchakato huo na kukubaliwa kubadili kada zao hasa baada ya kujiendeleza ila wanavyeti halali na wamesomea nafasi au ujuzi huo.

Mfano, ni walimu wa Voda Faster ambao kiuhalisia wao walimaliza kidato cha 6 na kupewa mafunzo ya muda mfupi ya ualimu kwa makubaliano ya kujiendeleza katika fani ya ualimu lakini kutoka na sababu na changamoto au nafasi mbalimbali zilizokuwepo walijiendeleza kwenye kada nyingine na kufanikiwa kubadilisha kada zao.

Ni wazi walimu hawa wengi wao hawakuwa na mapenzi na huo ualimu wa Voda Faster bali walitafuta njia ya kuingilia serikalini na ndicho kilichotokea.

Sasa kumekuwa na sintofahamu juu ya watumishi kama hawa nao kulipwa stahiki zao ambapo wanaambiwa kuwa hawawezi kulipwa kwani wao siyo wahanga wa vyeti feki.

Nikuombe kwa busara zako uwaangalie hawa watumishi pia kwa kuweka utaratibu wa wao pia kulipwa haki zao au kurejeshwa kazini kwenye kada walizojiendeleza na kubadilishwa.

Ni matumaini yangu kuwa utalifanyia kazi.

Nakala:

- Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

- Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu.
 
Mmmh em subiri, kwamba huyu huyu jpm wetu aliwatumbua na hao waliobadilisha kada kwa kujiendeleza kwa vyeti vyao halali?

Mbona mimi kuna mtu namjia alikuwa voda fasta akaenda chuo kusomea kitu kingine na JPM wetu hakumgusa yupo kazini kawaida?

Nachojua JPM wetu alidili na akina Makrina ila vyeti vinasoma frida. Anyway.......
 
Acha mambo ya ajabu ajabu hapa JF

Unafahamu maana ya kuwa na vyeti feki?

Hivi wewe una miaka mingapi?

Mimi mfano Nilisoma labda Bachelor of Econonomics na vyeti vyenye majina yangu ya Tonight Yohanne Halafu nikaenda kusoma tena Bachelor of engineering kwa majina yangu Tonight Yohanne, Sasa kwa ujinga wako unasema huyo mtu ana vyeti feki

Be Serious, Hao ndugu zako wanakudanganya

Waulize hivyo vyeti vyao vya form four au Six walivichukua kwa nani na walimlipa kiasi gani?

Waulize kama na wao waliazimisha vyeti vyao kwa watu walipata kiasi gani?

Vyeti feki ni vyeti ambavyo sio halali au mtu alitumia vyeti vya mtu mwingine

Zamani watu walikuwa wanatafuta vyeti vya form four mitaani waende ualimu au Jeshi

Na ilikuwa kawaida ukisikia watu wakisema yule anatumia vyeti vya kaka yake alikuwa na akili kweli

Kuna walimu wa shule ya msingi wamesoma sheria wengi tu na bado wanafundisha

Kuna walimu wa shule za Sekondari wamesoma mambo ya Journalism au Habari na bado wanafundisha

Hakuna siku serikali imemkatalia mtu kusoma anachohitaji maishani mwake

Muhimu
Inakuwaje cheti cha mwalimu huyo huyo pia kinapatikana kwa askari polisi na namba zinafanana

Namba ya cheti cha mtu mmoja kina wafanyakazi watatu, Mungine Polisi, Mwingine Mwalimu, Mwingine Afisa wa TRA wote cheti cha form four kinasoma S0105/001
 
Acha mambo ya ajabu ajabu hapa JF

Unafahamu maana ya kuwa na vyeti feki...
Kama huelewi mtu alichoandika uwe unaHULIZA mbwa wewe na siyo kila mtu ansyekuja hapa jf anabahatisha alichokileta.

Mimi hadi kuleta swala hili swala hapa ni wazi nimekuta na watumishi waliofanyiwa hivyo vyeti vyao vikiwa na majina yao sahihi tangu darasa la kwanza hadi chuo kikuu,akiwa mwalimu wa leseni aliomba ruhusa kwenda kusomea kozi tofauti na ualimu akaruhusiwa na alipomaliza kusoma fani nyingine na kupata shahada yake akabadilishiwa kada kutoka ualimu kwenda fani aliyosomea na akafanyakazi kwa muda na kuthibitishwa ila lilipokuja sakata la vyeti feki aliondolewa kwa maelezo kuwa alikiuka masharti ya ajira ya mwalimu wa leseni kwa kusomea fani nyingine na siyo ualimu na kaomba kulipwa mafao yake kanyimwa kwa maelezo kuwa yeye siyo wa vyeti feki sasa nakushangaa unabisha nini..

Acha kimbelembele kama goli la kwanza na kujiona uko sahihi kwa kila unachofikiria wewe siyo kila kilichoandikwa hapa umeandikiwa wewe au umjibie MH. RAIS labda kama amekutuma ufanye hivyo ila naamini yeye na watu wake ni waelewa atalifanyia kazi na kupata ukweli.

Inamaana na darasa la saba waliokuwa wameondolewa na kurudishwa pia walikuwa wametumia majina tofauti au vyeti feki?
 
Mmmh em subiri, kwamba huyu huyu jpm wetu aliwatumbua na hao waliobadilisha kada kwa kujiendeleza kwa vyeti vyao halali?

mbona mimi kuna mtu namjia alikuwa voda fasta akaenda chuo kusomea kitu kingine na jpm wetu hakumgusa yupo kazini kawaida?

Nachojua jpm wetu alidili na akina Makrina ila vyeti vinasoma frida. Anyway.......
Mbona akina bashite na wengi tu wengine Mawaziri wapo wanadunda tu.
 
'Waalimu wa leseni'. Maana yake ni nini?! Elimu ya Tz, haishangazi watoto wanashindwa mitihani kwa kiwango cha kutisha!
 
Nina broza ninae mfuata alisoma butimba vodafasta akapangwa kufindisha shule x, akaenda kujiendeleza nursing mpaka naandika ni nurse mkuu hospt mojawapo ya rufaa.

Na kuna ticha namfaham, alipata leseni 2005, akajisajiri open 2015 na amehtm 2018. Wakati wa uhakik wote hakuondolewa.

Kesi zako ipoje mkuu, unawafaham vzr waliopata changamoto au umesimuliwa?

Wapo wengine data base inasoma point 25 lakin karatasi ina 16 hao ndo wengi.
 
Acha mambo ya ajabu ajabu hapa JF

Unafahamu maana ya kuwa na vyeti feki...
Nimejaribu kuwaza tu. Anachoongelea huyu jamaa amepotoshwa ipo hivi;

Anayemwongelea scenario yake imekaa kama ifuatavyo; Ana cheti cha form four halali. Baada ya kusikia kazi akaenda kughushi cheti cha form six ili apate credibility ya ajira, na kweli akapata.

Baada ya muda akaenda kujiendeleza kwa kutumia cheti feki cha form six ili kuihama kada ya ualimu. Let say akaenda kusomea mambo ya HR.

Sasa ametumbuliwa analalamika. Kisa ana cheti cha form four halali na cha chuo halali. This is insane.
 
Kuna wengine hawakuwa na tsd number ila majina yalikuwepo kwenye payrall na mshahara walikuwa wanapata. Hawa nao waliondolewa kwenye payrall na kuhesabika ni wafanyakazi hewa wakati wapo hai na kazi wanafanya.

Wakati vyeti feki wanazungumzwa wapewe stahiki zao kwa kuitumikia serikali, waliotupwa kwenye dampo la wafanyakazi hewa hao hawazungumzwi kabisa.

Kwa ujumla zoezi la kuhakiki wafanyakazi lilifanyika hovyo sana.
 
Ninaunga mkono hoja ya wafanyakazi waliogushi vyeti kufukuzwa kazi ,yani watu wasote kusoma nakufaulu wenyewe wagushi vyeti halafu wanalalamika,mzilankende aliwahurumia sana kuwafukuza ilibidi awafunge kabisa.
 
Mmmh em subiri, kwamba huyu huyu jpm wetu aliwatumbua na hao waliobadilisha kada kwa kujiendeleza kwa vyeti vyao halali...
Anachoongea mleta mada kiko sahihi. Kuna Mtu aliajiriwa 1985 Kwa jina la kiasili, ilivyofika 1989 akabatizwa na kuanza kutumia jina la Kwanza la kikristo.

Lakini Kwa vile hakuwa na kiapo na alikubaliwa kubadilisha kipindi hicho Kwa barua tu, aliondolewa kazini.
 
Nimejaribu kuwaza tu. Anachoongelea huyu jamaa amepotoshwa ipo hivi;

Anayemwongelea scenario yake imekaa kama ifuatavyo; Ana cheti cha form four halali. Baada ya kusikia kazi akaenda kughushi cheti cha form six ili apate credibility ya ajira, na kweli akapata.

Baada ya muda akaenda kujiendeleza kwa kutumia cheti feki cha form six ili kuihama kada ya ualimu. Let say akaenda kusomea mambo ya HR.

Sasa ametumbuliwa analalamika. Kisa ana cheti cha form four halali na cha chuo halali. This is insane.
Usilazimishe kila mtu aamini unachojibu humu nimesma huyu mtu alisoma voda faster na akajiendeleza kwa majina yake yaleyale katika fani ya ushirika SUA na kuhitimu shahada hiyo na barua yake ya kuachishwa inaeleza alikiuka masharti ya ajira ya ualimu wa leseni kusoma kitu tofauti na ualimu.

Nakushangaemi mnapopinga hili utadhani nyie ndiyo mlizunguka tanzania nzima kufanya uhakiki na kuwaondoa wenye vyeti feti.

Naomba msiharibu maana halisi ya uzi huu sijaongelea VYETI FEKI nimeongelea aliye na vyeti sahihi na barua yake haisemi kuwa anaondolewa kwa vyeti feki bali kwa kukiuka masharti ya leseni ya ualimu.

Tuache wenye uwezo wa kuchangia uzi huu wachangie mawazo yao kwaajili ya ufumbuzi wa jambo hili kwani mhanga alifika hadi PSSF akajibiwa wanalipa waliokuwa na vyeti feki.

Muwe mnaelewa basi.
 
Anachoongea mleta mada kiko sahihi. Kuna Mtu aliajiriwa 1985 Kwa jina la kiasili, ilivyofika 1989 akabatizwa na kuanza kutumia jina la Kwanza la kikristo.

Lakini Kwa vile hakuwa na kiapo na alikubaliwa kubadilisha kipindi hicho Kwa barua tu, aliondolewa kazini.
Mie sielewi wanachobisha ni kipi,ina maana kila scenerio ya watumishi wanaoachishwa kazi eidha kwa uonevu humu nchi wanazijua?
 
Soma hiyo
20230224_104450.jpg
 
Mmmh em subiri, kwamba huyu huyu jpm wetu aliwatumbua na hao waliobadilisha kada kwa kujiendeleza kwa vyeti vyao halali?

Mbona mimi kuna mtu namjia alikuwa voda fasta akaenda chuo kusomea kitu kingine na JPM wetu hakumgusa yupo kazini kawaida?

Nachojua JPM wetu alidili na akina Makrina ila vyeti vinasoma frida. Anyway.......
Sahihi na wale ambao hawakujiendeleza Yaani walienda crush programs halafu hawakujiendeleza na Shule na wale waliokua na supplementary halafu hawakukuclear ndo waliondolewa

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom