Rais Samia, Mwanza: Uteuzi wa Wakuu wa Wilaya utatoka hivi karibuni, wote ni vijana. Mkipata fursa hizi mkafanye kama ilivyotarajiwa

Isitoshe hili ni dili la UVCCM tu. Nashangaa watu wamefurahi kweli kweli. UVCCM wenyewe hawa wengi pasua kichwa tu!
Mkuu mtanzania kucheza na akili yake ni rahisi sana. Si ajabu ukakuta vijana wengi kabisa wakisifia ujinga kama huu. Tatizo la vijana wa Tanzania siyo vyeo, iwe u-DC au u-RC. Kwanza hizo nafasi ni chache mno na zitachukuliwa na wapiga domo wa chama ''twawala''. Je mamilioni yaliyobaki yatafaidika? Huyu mama anaanza kuchemka mapema kweli kweli.
 
Hizi ni ”teuzi ajira” kwa UVMaCCM , hamna jipya hapo , leteni ajira kwa vijana , Mwendawazimu amevuruga nchi maisha ni magumu sana .
 
Hizi ni ”teuzi ajira” kwa UVMaCCM , hamna jipya hapo , leteni ajira kwa vijana , Mwendawazimu amevuruga nchi maisha ni magumu sana .
Mkuu hakuna cha mwenda wazimu wala nini nature inatake place. Kweli mwendazake ana mapungufu yake mengi ila nakuhakikishia there is no temporary solution eti kwa wanasiasa kutoa matamko. wanasiasa wawe wakweli tu sio kutoa kauli za kufurahisha watu mkuu.
 
Mkurugenzi ni mtumishi wa umma, Sasa anapotumbuliwa mshahara unabadilika? Kwa sababu kutumbuliwa sio kufukuzwa kazi, Kama mshahara unabakia uleule kubadilisha wakurugenzi ovyo ni mzigo kwa serikali
 
Una funza kichwani badala ya akili kama huyu Rais!Unaelewa maana ya long-run and sustainable employment policies?Unataka Taifa liendeshwe kwa vitimbi vya kisiasa badala ya strategy ambazo ni sustainable?
mkuu Vilainishi vyenu bajeti ijayo vitapunguziwa Kodi,naona mmechachamaa ,ili iwe wantelezea yakheee
 
Rais amesema Leo kuwa Ma-DC wote wapya watakuwa vijana maana karibuni anataka kufanya mabadiliko makubwa na wote watakaochukua nafasi ni vijana.

Kama ni kweli hii basi Natoa pongezi kwake.
Sasa Mzee wangu Kasesera itakuwaje ?
 
Rais amesema Leo kuwa Ma-DC wote wapya watakuwa vijana maana karibuni anataka kufanya mabadiliko makubwa na wote watakaochukua nafasi ni vijana.

Kama ni kweli hii basi Natoa pongezi kwake.
Wakina Ole Sabaya, Bashite, Hapi n.k ndio anaowataka?

Amandla...
 
Mama Samia akiwa Live mkoani Mwanza kwenye kongamano la vijana amesema tayari kuna mkeka wa MaDC na wakurugenzi wa mashirika mbali mbali ya serikali na vijana wakae mkao wakula kwani teuzi zitawahusu moja kwa moja kwa kiwango kikubwa.

====

"Vijana tunaomba mjitambue kuwa niyi vijana ndio wenye maoni ya taifa hili kwa sasa na karibu wateuliwa wote ni vijana na kuna mkeka wa maDC utakaotoka hivi karibuni. Nataka kuwaambia kuwa wote ni vijana, lakini vijana baadhi mnapopata fursa hizi mnatuangusha. Napenda kuwaambia kuwa mkipata fursa hizi mkafanye kama ilivyotarajiwa.", amesema Rais Samia

View attachment 1819491
Rais Samia akihutubia Wananchi waliohudhuria mkutano wake na vijana katika Uwanja wa Michezo wa Nyamagana, Mwanza.

View attachment 1819494
Vijana wa Mkoa wa Mwanza wakihudhuria mkutano huo kusikiliza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Vijana gani hao kina joketi au kina Gondwe. acha graduates wapambane na hali zao
 
Back
Top Bottom