Rais Samia Kumbuka Fao la Kujitoa

Rais Samia Kumbuka Fao la Kujitoa

Haya ni mawazo ya waajiriwa wa hiyo mifuko ya hifadhi ya jamii ndo maana wachangiaji wengi wanasema mna kiburi.Na ni ukweli mtupu
Mnasahau kwamba sisi wanachama wa mifuko hii ndio waajiri wenu.

Unataka kuniambia hiyo 10% anayochangia mwajiri hainihusu? are you serious?
Kama hainihusu mbona hakuchangii wewe usiyemfanyia kazi? Ikumbukwe mwajiri kama simzalishii faida
akafirisika anaruhusiwa kufunga biashara na tukaachana,ndo maana tunapambana kuhakikisha
kazi zinafanyika kwa kiwano ili kampuni zipate faida tulipwe mishahara na marupurupu mengi ikiwemo hilo la 10%
ya mifuko ya hifadhi ya jamii,bima,WCF n.k

Kwa wenye upeo mdogo wa mawazo wanadhani mwajiriwa anapewa kama hisani,
kama ni hisani basi wangepewa wananchi wote kwa kigezo cha kuwa ni watanzania.
Kuna watu wachache,mnajisikia vibaya hata kuona housegirl wako anashiriki kula mkate
mezani kwako au kunywa chai unadhani ni hisani wakati ndiye kapika hiyo chai
na akiamua kukuwekea sumu,unaweza kufa wewe na familia yako yote kama panya.

Badilika
OVER
Huyo anateswa na hofu. Hofu ya kuona kwamba pesa zitakuwa hazikai kwenye mifuko muda mrefu hivyo ulaji wao usio rasmi utatoweka.

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Mfano, mtu anafanya kazi ya Ulinzi au vibarua migodini na viwandani?

Kwahiyo, kwa AKILI zenu nzito huyo mtu atafanya kazi mpaka kufikisha miaka 60 ili muanze kumpa pension?

Kama pension Ni kitu muhimu hivyo, mbona hata hao wanaostahili tunaona wanahangaika tu kupata pesa zao?

Mbina wastafu hali zao Ni tete vile vile?
Watu wahuni sana!

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Leo hii nimeona clip whatsap ya mh.mbunge msukuma ikisema "Mtu mnaongea anakuambia habari za masters,n.k mwisho wa mazungumzo anakuomba buku kumi...'' mwisho wa kunukuu
hivi watu wote wanaoshtakiwa kwa kutumia ofisi zao vibaya wote hawajaenda shule?
Kama wameenda shule,imewasaidiaje,mbona niwezi kuliko wasiosoma?
Hapa namaanisha,mliosoma msifikirie wasiosoma ni mbumbumbu,kiasi
kwamba unaweza kufanya yasiyofaa kwa kuwadanganya kwamba ni usomi wakakuelewa.

Sasa nikuulize,tulionufaika na fao hilo la kujitoa miaka hiyo ya nyuma,
inamaana waliokuwa wanaendesha mifuko hiyo hawakuwa na uelewa wa kutosha
wa kuendesha mifuko hiyo? kama jibu ni ndiyo,effect yake kwa sasa ni kiasi gani?
mbona tunaona wazee na watu wa makamo wana maisha mazuri,na sheria iliwaruhusu
wakachukua fedha zao pindi walipotaka.

Nimeishasema hapo juu,na niseme tena kuwa asilimia kumi
anayokuchangia mwajiri siyo hisani,sheria inamtaka afanye hivyo kama mimi
inavyonitaka nilipe PAYE na nisipolipa ni kosa kisheria.Na mimi kama mwajiriwa nina wajibu wa kutimiza ili anichangie hiyo 10%
nisipofanyakazi kiwanda kikafungwa hawezi kunichangia kutoka kwenye akiba yake binafsi.Sasa huu ujasiri wa kusema mwajiliwa fedha ya kwake ni 10% mnaupata wapi? Ndo maana nilimpongeza Magu alipomfukuza yule mama aliyekuwa anakomaa na hoja hii
Sijui kwanini mnaoitwa wasomi hamlioni hili?
Ubinafsi hupofusha mkuu. Kuliona hili hadi na wao wawe wahanga.

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Nina jamaa yangu yuko anafia kitandani. Anaumwa sana na matibabu yake yanahitaji hela nyingi. Anapofanya kazi hakuna bima na ni miezi mitatu yuko kitandani kazini kwake wameshasitisha mshahara. Ameomba barua ya kuacha kazi amepewa. Amepeleka NSSF ili alipwe mafao yake eti wanamwambia mpaka atimize miaka sijua 55. Anawambia sina hata uhakik wa kuiona wiki ijayo naombeni mafao yangu yanifae sasa ili nipate matibabu nipone nianze upya lkn wamekataa. Niliumia sana yani jamaa anakufa na hela anayo alaf watarithi na kufaidika wengine.

Walioondoa fao la kujitoa laana hii iwafikie popote walipo
Fanya mkamrekodi video kisha irusheni

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Miongoni mwa mambo yaliyonifanya niichukie serikali yà awamu ya tano hasa yule dada wa peramiho alivyolishupalia hilo suala.kwanza kulikuwa hakuna haja ya kuanzisha fao la kujitoa pili ulikuwa ungumbaru wa kiwango cha reli kuunganisha mifuko ya hifadhi ya jamii leo psssf umechoka imechakaa kazi kutesa wastaafu
Cha ajabu waliopitisha hiyo sheria (Wabunge) wao wanalo fao la kujitoa, baada ya miaka yao mitano ya Ubunge wanakomba kila kilicho cha kwao wanasepa nacho, mbona sheria haijawaangalia kwamba na wao wasipewe hilo fao ili pesa hizo ziwasaidie uzeeni wasiwe mzigo kwa Serikali? Hiyo huruma kwa sisi Wananchi wengine imetoka wapi kama si upigaji wa pesa zetu?
 
Baada ya kusoma postings zote hapa, nimeona nichangie yafuatayo:

1) Wakulima hawapati Mafao ya Uzeeni kwa sababu hawachangii ktk Mfuko wowote.

Ninaamini Serikali iko katika maandalizi ya kuwafanya waanze kuchangia na hivyo kupata Mafao stahiki.

2) Hakuna aliyesema kuwa Mchango wa Mwajiri siyo stahili ya Mfanyakazi; bali hiyo sheria iliyomlazimisha Mwajiri kuchangia 10% ndiyo yenye Kanuni ya kutokuwa na Mafao ya kukitoa.

Hiwezi kuchukua bipande vya sheria fulani unavyovipenda na kuacha vingine. Kama siyo hiyo sheria mchango wa Mwajiri usingekuwepo.

3) Mchango wa Mwanachama hauwezi kukupa Mkopo kwa ajili ya kijengea nyimba, mtaji wa biashara na kusomeahea watoto au wewe mwenyewe.

Ila ikijipanga vizuri unaweza kutumia 90% unayobaki nayo, pamoja na fursa zingine za mitaji zilizopo kuanzisha biashara.

4) Kama kuna mapungufu ya kibinasamu ya mfanyakazi fulani wa Mfuko wa Hifadi ya jamii, soyo busara kurukia na kusema kuwa fedha za wanachama haziko salama. Hiyo ni generalisation isiyokuwa na busara. Wajenha wanasemanjoyo mo sweeping statement.

5) Suala la kusema “Mimi nipewe pesa zangu tu zote, kitakachotokea baadaye ni jukumu langu, siyo la Serikali” siyo la busara.

Serikali yenye kujalinwatu wake haifanyi kazi namna hiyo kama mambo ya kimtaani.

6) Hoja za watu wengi walioandoka zinaonyesha kuwa hawajui sheria ya hifadhi ya jamii. Wanatumia zaidi hisia na utashi binafsi kusema maneno mengiii ambayo hayana msingi wa sheria au kanuni. Haya siyonrahisinkuzingatiwa na Serikali.

Nashauri watu wazame zaidi katika kuelewa mantiki ya sheria zilizoanzisha mifuko ya hifadhi ya jamii.

Nahitimisha mchango wangu
 
Nahisi kuna watumishi wasiowaminifu zile pesa wanajikopa. Ndio maana hawaziingizi mpaka ukapige kelele
Hilo nalo neno,na ndo maana ukienda kufuatilia
unakutana na nyodo kama zote(hasa NSSF) mifuko mingine sijui, Na siku hizi kuna mamlaka ya kusimamia
hii mifuko sijui kazi yake nini?,wanalipwa mishahara minono utendaji kazi zero.

Ni kwa nini hao watumishi wa mifuko ya hifadhi ambao sisi ndio waajiri wao
hawafuatilii michango yetu kutoka kwa waajiri wetu
badala yake,ukienda wanaishia kukupatia fomu ukafuatilie wewe mwenyewe,

Tunaofanya kazi kwenye makampuni ya kigeni,ukipeleka zile fomu
wakakuonyesha ushahidi walivyowasilisha michango yako kwa wakati
unaona aibu ni jinsi gani watumishi wetu wanadharilisha mamlaka
zilizowaweka kazini kwa ajili ya maslahi binafsi.
 
Hakuna fao la kujitoa ktk mifuko ya hifadhi ya jamii duniani kote.
Mifuko hyo ni kwa ajili ya kumlinda mfanyakazi na majanga baada ya kustaafu ndo maana wewe unachangia only 10% ili hali mwajiri nae anaweka 10%.
Kama unataka kujiajiri jiwekezee 10% kwenye kibubu tuone kama utaweza kuwekeza baada ya miaka kumi.

Fao la kujitoa liliwekwa mwaka 1998 wakati wa ushindani kwenye kusaka wanachama kwa kua kulikua na mifuko 5,
Mwaka 2012 liliondolewa kina ZZK wakatetea likabaki kiaina ila ni kinyume na maana ya kuanzishwa mifuko hyo.na mwaka 2018 IRENE ISAKA alilifuta rasmi lakini mwendazake ktk kutafuta sifa akamfukuza kazi nanyi mkachekelea kizuzu.

Hakuna fao la kujitoaaa

Over
Umeandika ujinga.
 
Lengo la mifuko ya hifadhi ya jamii ni kutatua majanga baada ya kustaafu all over the world.

Sasa kama sisi tanzania ni tofauti lalama utalipwa fao la kujitoa.

Otherwise kimbia nchi
Achana na mambo ya dunia nzima.ina maana wewe huna akili zakufikiria ukaweka kitu chako vizuri hadi ukariri mambo ya watu wengine.Hizo ni sheria tu zinazowekwa kulingana na wakati ila zikijadiliwa zinaweza kurekebishwa kikafaa kwa manufaa ya watu.Hili lakusema mtu akiachishwa au kuacha kazi hawezi kupewa hayo mafao hadi afikishe miaka ya kustaafu ni matumizi mabovu ya akili na muda.sasa kama wewe unaona hilo ni sawa utakua na shida.
 
Nashauri watu wazame zaidi katika kuelewa mantiki ya sheria zilizoanzisha mifuko ya hifadhi ya jamii.
Kwahiyo kama mtu ana Laki 6 huko NSSF na ana miaka 25, maana yake anatakiwa kusubiri mpaka afikishe miaka 60 ndio apewe hiyo Laki 6???

Hao wabunge waliopita hiyo Sheria na wenyewe huu upuuzi unawahusu?
 
2) Hakuna aliyesema kuwa Mchango wa Mwajiri siyo stahili ya Mfanyakazi; bali hiyo sheria iliyomlazimisha Mwajiri kuchangia 10% ndiyo yenye Kanuni ya kutokuwa na Mafao ya kukitoa.

Hiwezi kuchukua bipande vya sheria fulani unavyovipenda na kuacha vingine. Kama siyo hiyo sheria mchango wa Mwajiri usingekuwepo.
Umechangia hoja kama wengine tunavyofanya,naomba unijibu
Swali hili, Je,sheria iliyomtaka mwajiri achangie mwajiliwa 10% kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii ilianza kufanya kazi mwaka gani?
na wakati huo fao la kujitoa lilikuwepo au ilipoanzishwa na fao hilo likafutwa?
 
Kiukweli,watumishi waliotumikia mifuko hii miaka ya nyuma walikuwa na uadilifu,waliridhika na mishahara yao
waliogopa laana ya kuiba kisichochao na unayemuibia ni mzee anayehitaji kuhudumiwa.
Watumishi wa sasa hivi wanataka mtu umeajiliwa juzi,uwe na gari na nyumba nzuri ya viwango ndani ya miaka miwili ya kuajiriwa
alafu tunashangaa eti,mbona vijana wengi siku hizi wanaongoza kufa kwa ajali?
Naomba niseme hivi kwa herufi kubwa ''GARI UNALOLINUNUA KWA FEDHA YA DHURUMA,INAYOWAACHIA WENGINE UCHUNGU NA KULIA MACHOZI,NI KABURI LINALOTEMBEA"
Hali kadharika nyumba iliyopatikana kwa njia hiyo hiyo, usippoiuza wewe kwa kupigwa na maisha,wataiuza wanao tena kwa bei poa
soma Mithali 13:22 na Mithali 21:6
habari ndo hiyo
hii inafanya kazi kwa wote,uwe unaamini au usiamini.
 
Otherwise kimbia nchiHii
Kiongozi,hii ni jeuri
na kwa kuwa midomo hailipiwi kodi,unaweza kusema lolote kwa sababu hakuna bill kama ya umeme wa Tanesco
ila ninachoweza kukuambia waangalie waliotangulia waliojibu jeuri kwa kudhani wapo salama.
Wengine tuliwashuhudia wakifagia hospitali kwenye utu uzima wao,sijui kama walikumbuka kuwa ni laana waliyoichuma ujanani.
Mambo hayo yanatokea ili walimwengu wengine tujifunze
 
For the first time umekuja Uzi naunga mkono Kwa asilimia 100. I am rare user of this forum but this is Post Touches me personally and direct.

Nimefanya kazi miaka 5 in 2 diff companies na nikakutana na retreachment. Nina zaidi ya 10mils but I only need 5 mils za mtaji na kuendeleza maisha.

Nimepambana Sana hata Kwa rushwa nipate hizi accumulations zangu but things get so complex.

Hapa Kwa hiili pamoja na kikokotoo inabidi turudi mezani aisee Mheshimiwa Rais na mamlaka husika tukigusa hapa tutatengeneza Ajira nyingi Sana.

Kilichoniumiza ni kuna wengine wanapata na kuna wengine hata tupambanaje ni mpaka 55+ years plus. Which is not certain.

That money is worth me now big time than the allocated time.
Asante.
 
Waasalam!

Hili ni ombi muhimu sana kwa Rais wetu mpendwa, anairudisha nchi katika muelekeo sahihi basi na sie vijana tulio sekta binafsi ambao tunatamani kujiajiri tunatamani sana fao la kujitoa lirudi ili angalau tupate mtaji wa pa kuanzia.

Sio wote tunatamani kuajiriwa mpaka miaka 55 - 60+ huko, wengine tuna “entrepreneurial spirits” lakini mitaji ndio kikwazo na mifumo ya fedha ya nchi haiamini kuwekeza katika mawazo bunifu, ndio maana wengi tunakubali kuajiriwa kwa miaka 5 - 10 kwa ujira mdogo tuweze kuwekeza kwenye mafao yetu ili baada ya ajira tukaanzishe biashara zetu.

Lilipopitishwa suala la kuzuia fao la kujitoa “kibabe” pasipo kishirikisha wananchi, wengi tuliumia sana kwani mfumo huo unanyima vijana wenye mawazo ya kujiajiri nafasi ya kufanya hivyo na unawalizimisha kuajiriwa kwa maisha yao yote. Mfumo uliopo sasa hivi umetengeneza mwanya mkubwa sana wa rushwa ili mtu kupata hata hicho kiasi kidogo cha fao la kukosa ajira, kama hutoi rushwa utasugua sana soli NSSF na “maafisa” wanakuchora tu, mpaka unakata tamaa.

Tukilazimisha vijana wote kuajiriwa miaka 50+ pasipo kuwa na mbadala wa kufikiria kuanzisha biashara/kujiajiri ni kivipi tutaweza kuanzisha biashara mpya na kuongeza ajira zaidi nchini?

Ushauri wangu ni kurudisha uhuru wa fao la kujitoa ili kama kijana amechoka na ujira mdogo kibaruani, anaweza akajiajiri mwenyewe kwa kuwa tayari ana mtaji wa kuanzia.

Hoja ya kuwa vijana hawa wakizeeka watakua mzigo kwa serikali, inaweza kutazamwa upya kwa kuwndelea kuwawekea vijana hao waliojiri mazingira rafiki ya kuchangia mafao yao wakiwa kama wajasiriamali.

Shukrani.
Kama JF tungekua tunabadilishana maarifa mawazo na maarifa kwa mabandiko kama hili nahisi pamoja na mengine tungepata baraka pia.

Hongera mleta bandiko.
 
Back
Top Bottom