econonist
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 23,925
- 37,122
KUONDOKEWA MAFAO YA KUJITOA NI KWA MANUFAA YA WANACHAMA
Nimesoma yote yaliyoandikwa na wadau na kugundua kwamba wote hawafahamu DHANA YA HIFADHI YA JAMII. Kwa sisi tuliopiya IFM, ninvyema tukatoa elimu kidogo kwa ndani gu zetu ambao hawaelewi vizuri jambo hili. Kwa taarifa, dhana msingi ya Hifadhi ya Jamii ni:-
“Kumfanya mtu kuweka akiba kidogokidogo wakati ana uwezo wa kutengeneza mapato ili akiba hiyo imfae wakati atakapokuwa hana uwezo wa kuzalisha mapato”.
Kwa NSSF, Sheria inamtaka Mwanachama kuchangia 10% tu ya mshahara wake; na Sheria hiyo hiyo inamlazimisha Mwajiri kuchangia 10% ya ziada kukamilisha akiba ya Mwanachama huyo. Kwa maana nyingine, Mwanachama asingepata hiyo 10% ya Mwajiri bila ya Sheria hii.
Akiba hii inapaswa kuendelea kujaziwa kwa kipindi chote cha Mwanachama akiwa na uwezo wa kufanya kazi. Wakati mtu anapochangia 10% ya mshahara wake, anabaki na 90% ya mapato yake. Kudundiliza huku kutaendelea kwa kutumia waajiri mbalimbali atakaofanya nao kazi katika maisha yake.
Kama ni mjasiriamali mzuri, atatumia kiasi kingine kidogo kutoka 90% ili kudunduliza mtaki kwa muda fulani na kuanza biashara. Kama atashindwa kufanya hivyo hadi siku anakosa ajira ndiyo aanze kupambania 10% aliyokuwa anaweka ili aanzisjie biashara, huyo siyo mjasiriamali. Na uwezekano mkubwa ni kwamba hata akizipata hazitamfikisha mbali na itambidi atafute kazi tena ya kuajiriwa.
Sasa wakati akifikia utu uzima na uwezo wa kuchakarika kufanya kazi haupo, ndiyo sasa ataanza kupata pensheni ya kila mwezi hadi mauti yatakapomchukua. Kama aliwahi kuanzisha biashara na ikafanikiwa, maisha yake ya uzeeni yatakuwa mazuri. Kama hakuwahi kuanzisha biashara, basi atakuwa na uhakika wa kupata mahitaji yake muhimu.
Fursa za kuanzisha biashara ziko nyingi tu kwa wajasiriamali waziri. Tukumbuke Bilionea Reginald Mengi alianzisha IPP wakati yeye ni mwajiriwa wa PWC mpaka pale kampuni yake ya IPP ilipokuwa kubwa sana ndipo akaacha kazi. Unaweza ukachangia SACCOS au ikaweka fedha zako Benki na baadae ukachukua mkopo kuanzisha biashara. Kama haya yote huyawezi, kuwa na uhakika hata akiba yako ya NSSF ya 10% haitakusaidia kitu.
Kila mfumo umeanzishwa kwa makusudi yake na taratibu husika lazima zifuatwe. Kama kwa bahati mbaya makusudi haya hatyajui vizuri tuepuke kufanya kosa na kuongea bila elimu na kuanza kuwatukana watu matusi wasiyostahili.
No please, fao la kujitoa lipo kwaajili ya kumlinda mwaajiriwa pale anapo kosa ajira au pale ambapo mwajiri wake amefilisika. Fao la kujitoa ni haki ya mwajiriwa ila awe nje ya ajira. Kwa mfano Mtu amefukuzwa kazi, ameugua kwa mda mrefu au mkataba haujaongezwa kama kwenye sekta binafsi unaenda kwenye Fao la kujitoa kwaajili ya kukulinda kipindi chote ambacho utakosa ajira.
Rais alifikilie hili suala la fao la kujitoa kwa kina, waajiriwa wengi waliokoondolewa kwenye ajira hasa sekta binafsi, wanapata shida huku pesa zao zipo NSSF zinatumika kwenye Mambo ambayo si ya msingi kwa uanzishwajo wa mfuko huo.