Waasalam!
Hili ni ombi muhimu sana kwa Rais wetu mpendwa, anairudisha nchi katika muelekeo sahihi basi na sie vijana tulio sekta binafsi ambao tunatamani kujiajiri tunatamani sana fao la kujitoa lirudi ili angalau tupate mtaji wa pa kuanzia.
Sio wote tunatamani kuajiriwa mpaka miaka 55 - 60+ huko, wengine tuna “entrepreneurial spirits” lakini mitaji ndio kikwazo na mifumo ya fedha ya nchi haiamini kuwekeza katika mawazo bunifu, ndio maana wengi tunakubali kuajiriwa kwa miaka 5 - 10 kwa ujira mdogo tuweze kuwekeza kwenye mafao yetu ili baada ya ajira tukaanzishe biashara zetu.
Lilipopitishwa suala la kuzuia fao la kujitoa “kibabe” pasipo kishirikisha wananchi, wengi tuliumia sana kwani mfumo huo unanyima vijana wenye mawazo ya kujiajiri nafasi ya kufanya hivyo na unawalizimisha kuajiriwa kwa maisha yao yote. Mfumo uliopo sasa hivi umetengeneza mwanya mkubwa sana wa rushwa ili mtu kupata hata hicho kiasi kidogo cha fao la kukosa ajira, kama hutoi rushwa utasugua sana soli NSSF na “maafisa” wanakuchora tu, mpaka unakata tamaa.
Tukilazimisha vijana wote kuajiriwa miaka 50+ pasipo kuwa na mbadala wa kufikiria kuanzisha biashara/kujiajiri ni kivipi tutaweza kuanzisha biashara mpya na kuongeza ajira zaidi nchini?
Ushauri wangu ni kurudisha uhuru wa fao la kujitoa ili kama kijana amechoka na ujira mdogo kibaruani, anaweza akajiajiri mwenyewe kwa kuwa tayari ana mtaji wa kuanzia.
Hoja ya kuwa vijana hawa wakizeeka watakua mzigo kwa serikali, inaweza kutazamwa upya kwa kuwndelea kuwawekea vijana hao waliojiri mazingira rafiki ya kuchangia mafao yao wakiwa kama wajasiriamali.
Shukrani.
Nakubaliana na wewe,mfano mimi ni aged
na nimeajiriwa ila katika maisha yangu sijawahi kuajiriwa na serikali.
lakini nimenufaika na fao hili la kujitoa kila nilipobadilisha ajira,kabla ya mfumo huu wa sasa
na matokeo yake nayaona nikiangalia nilipotoka na mahali nilipo.Kwa kweli anayebeza fao la kujitoa nawezasema
bila uoga kuwa ni mnufaika wa kifisadi wa mifuko hiyo,ndo maana hawataki fedha hiyo itoke.
mbona zamani tulipewa tukafanya mambo yetu na maisha yakaendelea?
Ok,tuseme wana uchungu na maisha ya wazee baada ya kustaafu wasijekosa kujikimu,
niulize swali,je wanafanya nini kuhusu wakulima ambao ni asilimia 80 ya wananchi wote
ili wakizeeka wasihangaike,au hao hawazeeki? Kama wanazeeka kwao inakuwaje? au nao wapo kwenye mifuko
ya hifadhi ya jamii?
Mimi ningeshauri,vijana waruhusiwe kunufaika na fao hilo kama itaonekana
wana uchungu na maisha yao ya baadae,wawashauri wakifikisha umri wa miaka 45
wafikilie kutojitoa tena ili kuweza kufikisha michango 180 pindi wafikishapo miaka 60 ya kustaafu
waingie kwenye scheme ya wastaafu.
Pili waweke vivutio,kama vile kukopesha wanachama nyumba,viwanja na kuwajengea
na waweke utaratibu kwamba ukishakopeshwa wewe unajisajiri kwenye mfumo wa kutohusika na fao la kujitoa.
Lakini kuwanyima kabisa fedha zao kwa vigezo kandamizi ni kuwaonea na kuwafanya wengi waliokazini wawe wezi
kwa kisingizio cha kutafuta mitaji ya kipato cha ziada.
Ikumbukwe unawezakuwa kazini na ukawa una kitu kingine kinakuingizia kipato maana siku zote mshahara hautoshi.