Rais Samia jumba bovu analilea mwenyewe

Rais Samia jumba bovu analilea mwenyewe

Msimpangie...

Hakuna anapopangiwa. Uzi wala haumhusu kwa maana hauko addressed kwake.

Haya mbona ni mazungumzo ya wanaoiona hali kutokea nje?

Aliita Trump - hizi ni Locker room talk tu.
 
Mbona mbowe mnapiga kelele kuna wafungwa wangapi magerezani subiri mahakama iamue hatma ya mbowe ile ni mhimili mwingine
Sio kelele,ushahidi unaokuja MAHAKAMAN unaonesha kabis hakuna la maana,uzuri ata wewe unajua hilo
 
jana niliyafeel maumivu ya rais samia japo sikumkubali, kuna kitu hajakijua hilo kundi linalomuunga wanamchezesha mchezo wa kisiasa ili awaone sukuma gang ni maadui zake wao wanufaike kisiasa, mama anapaswa kua makini sana na kundi linalomuunga mkono kuliko hata sukuma gang.

Ni siasa chafu zinazotokana na mfumo mchafu na Katiba isiyofaa.
Viongozi wa kiafrika wametiwa upofu kwa maovu yao na nia zao zilizoja ubinafsi.
Yesu Masihi alisema watazama Lakini hawataona.
Katiba iliyopo hata akitawala malaika ,atatengemezewa Michezo michafu na wale waliomzunguka ili wao ama waibe au wajihakikishie Kuwa maharaka ni Yao na watoto wako.
Wakati wa JPM ana Pole pole walimuaminisha Kuwa adui wa nchi hii ni wapinzani ,ikatumika nguvu kubwa na Haramu kinyuma cha sharia ili kuua na hata kuwapoteza wapinzani. Zilitumika fedha nyingi kuwahonga watu ili kuua upinzani . Wakurugenzi na PolisI wakavuruga uchaguzi matokeo yake leo Tanzania hakuna wawakilishi wa wananchi. Kila kitu kinapangwa na dola na kusimamiwa na dola kwa nguvu ya dola Kuanzia kwenye mitaa mpaka Juu.
JPM akapotoshwa na Kuanza kupambana na akina Lisu na wabunge na madiwani. Matokeo yake Wahuni wakajikeza wakaanza kujizolea mapesa kwa wafanyabiashara kwa vitisho.
Serikali ya awamu ya Tano ilitumia Mwanya wa kutafuta kundi na kulisukumizia lawama za Mabaya kama ilivyokua ya nne,ya tatu,ya pili na ya Kwanza ambayo nayo ilitumia muda kulaumu wakoloni huku Serikali ikishindwa kusimamia kila kilichoachwa na mkononi mpaka migodi ya madini na Mashamba yaliyokuwa bora katiba wakati wa mkojani.

CCM wakiikumbatia katiba hii watambue Wazi kua ZambI ya kutengenezeana mizengwe ,fitina na uzushi haitawaacha wakistaafu au akija wa awamu nyengine
 
Ni siasa chafu zinazotokana na mfumo mchafu na Katiba isiyofaa.
Viongozi wa kiafrika wametiwa upofu kwa maovu yao na nia zao zilizoja ubinafsi.
Yesu Masihi alisema watazama Lakini hawataona.
Katiba iliyopo hata akitawala malaika ,atatengemezewa Michezo michafu na wale waliomzunguka ili wao ama waibe au wajihakikishie Kuwa maharaka ni Yao na watoto wako.
Wakati wa JPM ana Pole pole walimuaminisha Kuwa adui wa nchi hii ni wapinzani ,ikatumika nguvu kubwa na Haramu kinyuma cha sharia ili kuua na hata kuwapoteza wapinzani. Zilitumika fedha nyingi kuwahonga watu ili kuua upinzani . Wakurugenzi na PolisI wakavuruga uchaguzi matokeo yake leo Tanzania hakuna wawakilishi wa wananchi. Kila kitu kinapangwa na dola na kusimamiwa na dola kwa nguvu ya dola Kuanzia kwenye mitaa mpaka Juu.
CCM ni wajaa laana, tunapaswa kuwang'oa madarakani kwa nguvu maana wanaliharibu taifa lenye raslimali za kutosha kwa maslahi yao binafsi.
 
Kama binadamu ni muhimu kukumbuka ulikotoka, kuelewa ulipo na kujua unakokwenda.

View attachment 2033861

Kwamba ni sasa ndiyo anaangushiwa Jumba bovu? Mbona bado?

Asipoangalia mbona hata la Mbowe nalo atangushiwa yeye?

Bora angejikita (japo kwa kuchelewa) kwenye haki na maridhiano kuurejesha uungwaji mkono uliopotea.

Legacy ya kuiachia hii nchi Katiba mpya ingempa heshima kubwa zaidi kuliko hata ya urais 2025 anaoonekana kuutaka mno.

-----------
Matumaini yote ya siku 100 aliyowapa Wananchi yazikwa na kauli ya dk 1
Alitakiwa kwanza kuomba radhi watz kwa matendo ya awamu ya 5, pia ilibidi atubu KWA mola Toba ya dhati, ya moyo Ili tuondolewe laana aliyoileta magufuli. Vinginevyo hakuna atakalofanya likaonekana,
 
CCM imebakia ni kundi dogo la watawala lisilo na support yeyeote na wananchi.. wanajua kuruhusu mikutano ya hadhara, kufanya uchaguzi huru na haki watakuwa wamejikatia tiketi yao ya kuwa chama cha upinzani.
 
Mbowe issue yake ipo mahakamani ,kama hana hatia ataachiwa,msimlazimishe rais Samia kuingilia Uhuru wa Mahakama.
Haya nakumbuka mliyapinga kwa Magufuli iweje sasa kwa Samia?
Mbona Sabaya kala 30yrs in prison na mkashangilia na kukenua meno ya kwamba mahakama imetenda haki,sasa na huyo gaidi mtuhumiwa haki itatendeka
Kwani Rugemarila aliachiwa na mahakama?Jibu ni hapana.
Lakini kesi yake si ilikuwa mahakamani? Kwa kifupi Rais hashindwi jambo ndani ya nchi yake.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom