Rais Samia ikiwezekana kwepa kuwalenga Wasukuma moja kwa moja kwenye hotuba zako

Ni leo tena.

Mheshimiwa Rais amewatupia lawama Wasukuma kwa kuharibu vyanzo vya maji katika maeneo mbalimbali hapa nchini kwa sababu ya ufugaji wao wa ng'ombe wengi.

Nia yangu bayana kwenye andiko langu ni kumshauri Rais ikiwezekana ajizuie kuwataja moja kwa moja Wasukuma kwenye hadhira kwa sababu hali ile pengine inaweza kutafsirika tofauti na walengwa hasa ukizingatia ndani ya muda mchache wa Utawala wake tuhuma nyingi za kubaguliwa walengwa zi bayana.

Ingetosha mheshimiwa Rais angetoka kauli ya jumla tu kwamba wafugaji ni sehemu ya wanaoharibu vyanzo vya maji

Sasa unapowataja Wasukuma moja kwa moja ilhali wapo wamasai na makabila mengine mengi yanayofuga maelfu ya mifugo ni sawa na kuwabagua watajwa

Mungu ibariki Tanzania.
Wasukuma ni wapambanaji wanaojua kutumia rasilimali za nchi yao tanzania
 
Ni leo tena.

Mheshimiwa Rais amewatupia lawama Wasukuma kwa kuharibu vyanzo vya maji katika maeneo mbalimbali hapa nchini kwa sababu ya ufugaji wao wa ng'ombe wengi.

Nia yangu bayana kwenye andiko langu ni kumshauri Rais ikiwezekana ajizuie kuwataja moja kwa moja Wasukuma kwenye hadhira kwa sababu hali ile pengine inaweza kutafsirika tofauti na walengwa hasa ukizingatia ndani ya muda mchache wa Utawala wake tuhuma nyingi za kubaguliwa walengwa zi bayana.

Ingetosha mheshimiwa Rais angetoka kauli ya jumla tu kwamba wafugaji ni sehemu ya wanaoharibu vyanzo vya maji

Sasa unapowataja Wasukuma moja kwa moja ilhali wapo wamasai na makabila mengine mengi yanayofuga maelfu ya mifugo ni sawa na kuwabagua watajwa

Mungu ibariki Tanzania.
Waandishi wa hotuba za Madam President wanapaswa kuwa makini mno na maudhui yaliyomo ndani yake. Anapaswa kuzungumzia mambo ya msingi kwa kutaja tu sekta husika wala si kwa kutaja kabila.

Wasukuma ni moja ya kabila kubwa na lenye watu wengi hapa nchini. Kutaja tatizo mojawapo linalopelekea uhaba wa maji unaoendelea hapa nchini kunaendana na shughuli zao za ufugaji ni kutokuwatendea haki.

Lazima tuwe wakweli, chanzo cha uhakika cha maji katika nchi yetu kinategemea misimu ya mvua. Mvua zikiwa za kutosha hutasikia kelele kuhusu uhaba wa maji.

Nakumbuka kuna nyakati Mh. Ngoyayi akiwa Waziri Mkuu aliwahi kuleta wazo kutoka Vietnam la kutengeneza mvua ili kukabiliana na changamoto ya uhaba wa maji. Kwa hiyo basi uhaba wa mvua si kitu kigeni hapa nchini, huwa kinajirudia kutoka kipindi kimoja kwenda kingine. Hakuna haja ya kuwanyooshea kidole Wasukuma.
 
Niliogopa mno aliposema "tena Wasukuma!"
Wasukuma ni AKILI KUBWA hata mama anajua hivo.
Mama Samia bado anahangaishwa na mzimu wa Marehemu Magufuli.
Ni Bora akaacha kuwasakama Wasukuma akawa mpole maana Uchaguzi wa 2025 hauko mbali sana. Asije akaikosesha CCM kura za Urais 2025.
Huu ni ushauri wa bure kabisa.
 
Niliogopa mno aliposema "tena Wasukuma!"
Wasukuma ni AKILI KUBWA hata mama anajua hivo.
Mama Samia bado anahangaishwa na mzimu wa Marehemu Magufuli.
Ni Bora akaacha kuwasakama Wasukuma akawa mpole maana Uchaguzi wa 2025 hauko mbali sana. Asije akaikosesha CCM kura za Urais 2025.
Huu ni ushauri wa bure kabisa
 
Back
Top Bottom